Slider

JAMII IMETAKIWA KUSHIRIKISHA WANAWAKE KIKAMILIFU KWENYE VIKAO VYA MAAMUZI
Local News

MAKAMU wa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mheshimiwa Samia Suluhu Hassan, amewataka watanzania wote kutambua kwamba mafanikio na maendeleo yoyote ndani ya jamii na Taifa kwa ujumla hayawezi kupatikana endapo wanawake hawataweza kushirikishwa kikamilifu kwenye vikao vya maauzi.   Mheshimiwa Samia ameyasema hayo leo Jijini Dar es Salaam alipokuwa akizungumza kwenye ufunguzi wa kongamano la wanawake katika uongozi lililoandaliwa na taasisi ya uongozi na kuwakutanisha wanawake wa kitanzania wenye nyadhifa mbalimbali za uongozi nchini....

Like
266
0
Tuesday, 12 April 2016
JESHI LAPEWA JUKUMU LA KUTENGENEZA MADAWATI YENYE THAMANI YA SHILINGI BILIONI 6
Local News

JESHI La Magereza nchini na Jeshi la Kujenga Taifa wamepewa jukumu la kutengeneza madawati yenye thamani ya shilingi Bilioni 6 ambayo yatasambazwa katika Mikoa yote ya Tanzania Bara na Zanzibar.   Jukumu hilo kwa Vyombo vya Ulinzi na Usalama limetolewa jana na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika hafla fupi ya makabidhiziano ya mfano wa hundi ya shilingi Bilioni 6 kutoka Sekretarieti ya Bunge ya Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania fedha ambazo zimepatikana kufuatia...

Like
241
0
Tuesday, 12 April 2016
AFISA WA KIJESHI AHAMIA KOREA KUSINI
Global News

AFISA mmoja wa kijeshi wa cheo cha juu nchini Korea Kaskazini, ambaye alikuwa akisimamia masuala ya ujasusi ameihama nchi hiyo na kuelekea Korea Kusini. Afisa huyo hajatajwa jina lakini wizara ya ulinzi nchini Korea Kusini imesema kuwa alikuwa afisa wa cheo cha juu na aliondoka nchini Korea Kaskazini mwaka uliopita. Shirika la habari la Yonhap nchini Korea Kusini, limenukuu taarifa zilizosema kuwa kanali huyo alitajwa kuwa shujaa sambamba na wale walioihama Korea...

Like
246
0
Monday, 11 April 2016
OBAMA AKIRI KUSHINDWA KWA SERIKALI YAKE KWENYE UTATUZI WA MZOZO WA LIBYA
Global News

RAIS wa Marekani Barack Obama amekiri kwa mara ya kwanza kwamba serikali yake imefeli katika kutatua mzozo wa Libya. Amesema hilo huenda ndilo “kosa kubwa” zaidi alilolitenda wakati wa utawala wake. Obama pia amesema Marekani haikuwa na mpango mahususi wa jinsi Taifa hilo litakavyotawaliwa baada ya kuondolewa madarakani kwa Kanali Muammar...

Like
280
0
Monday, 11 April 2016
WAZIRI UMMY MWALIMU AZINDUA TAASISI YA BASILLA MWANUKUZI BMF
Local News

WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu leo amezindua rasmi taasisi ya Basilla Mwanukuzi BMF-yenye lengo la kushirikiana na Wadau ili kuwawezesha Wanawake kiuchumi. Hafla hiyo ya uzinduzi imeenda sanjari na uzinduzi wa mradi wa “Wezesha mama lishe Tanzania” ukiwa na lengo la kuwawezesha mama lishe kupata elimu ya ujasiriamali na upikaji wa chakula bora chenye kuzingatia virutubisho. Akizungumza katika hafla hiyo Waziri Mwalimu amesema kuwa wengi waliopo katika sekta ya mama lishe ni...

Like
204
0
Monday, 11 April 2016
MAGUFULI ATENGUA UTEUZI WA MKUU WA MKOA WA SHINYANGA MAMA ANNA KILANGO MALECELLA
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta John Pombe Magufuli ametengua uteuzi wa Mkuu wa Mkoa wa Shinyanga, Mama Anna Kilango Malecella kwa kubaini kuwa alimwambia uwongo kuwa Mkoa wake hauna wafanyakazi hewa wakati wapo wengi.   Rais Magufuli amesema kwamba hakuamini kwamba kuna mkoa ambao hauna wafanyakazi hewa, hivyo akatuma kikosi kazi ambacho hadi usiku wa kuamkia leo kimebaini kuwepo kwa wafanyakazi hewa 45 mkoani Shinyanya.   Akizungumza baada ya kupokea Ripoti ya TAKUKURU kutoka kwa Mkurugenzi Mkuu wa Takukuru...

Like
297
0
Monday, 11 April 2016
MWANAHABARI WA AL-SHABAAB AUAWA SOMALIA
Global News

MWANAHABARI aliyesaidia kundi la al-Shabaab kuua wanahabari wenzake nchini Somalia ameuawa.   Hassan Hanafi ameuawa kwa kupigwa risasi mapema asubuhi ya leo baada ya kuhukumiwa kifo na mahakama ya kijeshi nchini humo.   Hassan Hanafi, alipatikana na hatia ya kuwaua Sheikh Noor Mohamed Abkey (mhariri wa shirika la habari la SONNA), Sa’id Tahlil Warsame (mkurugenzi wa HornAfrik), na Mukhtar Mohamed Hirabe (mkurugenzi wa Radio Shabelle), na wanahabari wengine...

Like
487
0
Monday, 11 April 2016
DARFUR KUPIGA KURA YA MAONI LEO
Global News

JIMBO la magharibi mwa Sudan Darfur, leo linapiga kura ya maoni, miaka 13 baada ya kuanza kwa mzozo wa wenyewe kwa wenyewe uliosababisha watu laki 3, kupoteza maisha.   Kura ya maoni itaamua kama Darfur itakuwa na majimbo matano au jimbo moja, ambapo raia watakuwa na siku mpaka ya jumatano kuamua.   Marekani imeeleza hofu yake kuwa kura hiyo haitakuwa ya haki, lakini Rais Omar al-Bashir amesisitiza kuwa itakuwa huru na haki. Ikiwa ni hatua ya mwisho ya mchakato wa...

Like
203
0
Monday, 11 April 2016
SERIKALI YATAKIWA KUZINGATIA KASI YA ONGEZEKO LA WATU
Local News

SERIKALI nchini imetakiwa kuzingatia kasi ya ongezeko la idadi ya watu katika mipango yake ya maendeleo ikiwemo uwekaji wa mikakati bora na uboreshaji wa sera ili kuweka uwiano sahihi kati ya ongezeko la watu na maendeleo ya Taifa.   Hayo yamebainishwa jana Jijini Dar es salaam na wajumbe na mabalozi wa kikundi kazi kinachoundwa na wadau na watetezi wa masuala ya uzazi wa mpango na idadi ya watu-TCDAA– ambapo kwa upande wa mwakilisi mwandamizi wa kikundi kazi hicho Bi. Halima...

Like
257
0
Monday, 11 April 2016
WATUHUMIWA DAWA ZA KULEVYA WAZIDI KUBANWA
Local News

WAZIRI MKUU wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa, Kassim Majaliwa amemtaka Mkuu wa Magereza mkoa wa Lindi, kuhakikisha hakuna mtuhumiwa wa dawa za kulevya atakayetoweka katika gereza la mkoa huo.   Amesema kuna watuhumiwa wa dawa za kulevya ambao wanahifadhiwa katika gereza hilo, hivyo ni vema akajiridhisha kama ulinzi na usalama wa watuhumiwa hao umeimarishwa.   Waziri Mkuu, Majaliwa ameyasema hayo wilayani Ruangwa wakati akipokea taarifa ya maendeleo ya mkoa wa Lindi iliyowasilishwa kwake na Mkuu wa mkoa huo, Godfrey...

Like
258
0
Monday, 11 April 2016
MOURINHO AKATAA KAZI SYRIA
Slider

Aliyekuwa meneja wa klabu ya Chelsea Jose Mourinho amekataa ombi la kumtaka awe meneja wa timu ya taifa ya Syria, wakala wake amesema. Kupitia barua pepe iliyotumwa kwa shirika la habari la Associated Press, Jorge Mendes amesema Mourinho aliambia Shirikisho la Soka la Syria kwamba “ameshukuru sana kupokea mwaliko, lakini hawezi akaukubali kwa sasa”. Mreno huyo mwenye umri wa miaka 53 alifutwa kazi na Chelsea kwa mara ya pili Desemba. Mourinho, ambaye amewahi kuwa meneja Porto, Real Madrid na Inter...

Like
268
0
Monday, 11 April 2016