Slider

TEMEKE: WANANCHI WATAKIWA KUFICHUA WAUZAJI WA DAWA ZA KULEVYA
Local News

JESHI la Polisi mkoa wa Kipolisi Temeke limewaomba wakazi wa maeneo hayo kutoa taarifa juu ya watu wanaohusika na uuzaji wa dawa za kulevya kwakuwa kimekuwa ni chanzo cha vijana kushindwa kujishughulisha. Akizungumza na EFM Kamanda wa Polisi wa mkoa wa Temeke  Andrew Satta amesema kuwa kutokana na oparesheni inayoendelea ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya, jeshi hilo limegundua wauzaji wakubwa wa dawa hizo kukimbia na kwenda kujificha katika maeneo ya nje ya mkoa huo wa...

Like
261
0
Monday, 15 February 2016
WAKURUGENZI WANNE MSD WASIMAMISHWA KAZI KWA TUHUMA ZA UBADHIRIFU WA FEDHA
Local News

WAZIRI wa afya maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Mheshimiwa Ummy Mwalimu amewasimamisha kazi wakurugenzi wanne kutoka Bohari ya Dawa ya Taifa-MSD- kwa tuhuma za ubadhilifu wa fedha takribani shilingi Bilioni 1.5.   Akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam leo katika kitengo cha Afya ya mama na mtoto baada ya kupokea vifaa kutoka Bohari kuu ya Taifa ya dawa, waziri Ummy amesema amefanya maamuzi hayo kufuatia kupokea taarifa ya uchunguzi ofisini kwake juu ya ubadhilifu wa...

Like
223
0
Monday, 15 February 2016
TAMASHA LA MCHIZI WANGU LAFANA JIJINI DAR ES SALAAM
Entertanment

93.7 Efm Radio,kuadhimisha tamasha kubwa la Mchizi wangu lililofanyika siku ya wapendanao tarehe 14/02/2016, likiongozwa na mziki wa mchiriku na singeli. Tamasha hilo lilisheheni Wasani kibao wakitumbuiza huku wakiongozwa na msaga sumu na skide mtoto wa mama shante. Umati wa watu ukisheheni katika tamasha la mchizi wangu concert   Raisi wa singeli Suleiman Jabir a.k.a Msaga Sumu akitumbuiza mashabaki waliofika kwenye tamasha la Mchizi Wangu. Amsha amsha kutoka kwa baadhi ya mashabiki wakionyesha nyuso za furaha wakati wakipata burudani....

Like
511
0
Monday, 15 February 2016
MUSEVENI: NINA IMANI NITASHINDA UCHAGUZI
Global News

RAIS wa Uganda Yoweri Museveni amesema ana imani atashinda urais kwenye uchaguzi mkuu utakaofanyika siku ya Alhamisi wiki hii. Hata hivyo, amesema yuko tayari kukabidhi madaraka kwa mtu mwingine iwapo chama chake kitashindwa. Akijibu maswali ya waandishi wa Habari  wakati wa kikao kilichofanyika Ikulu jana Jumapili, Bwana Museveni amesema kwa sasa haoni chama chochote ambacho kinaweza kuondoa chama cha National Resistance Movement (NRM)...

Like
352
0
Monday, 15 February 2016
KURA ZAHESABIWA AFRIKA YA KATI
Global News

MAAFISA wa uchaguzi wanaendelea kuhesabu kura baada ya Jamhuri ya Afrika ya Kati kuandaa jana awamu ya pili iliyocheleweshwa ya uchaguzi wa rais na wabunge, ikiwa na matumaini ya kupatikana amani baada ya kutokea machafuko makubwa ya kidini kuwahi kushuhudiwa nchini humo tangu uhuru mwaka wa 1960. Upigaji kura ulifanywa chini ya ulinzi mkali huku maelfu ya wanajeshi wa kulinda amani wa Umoja wa Mataifa wakiwekwa kote nchini humo, lakini uchaguzi huo ulikamilika kwa amani. Matokeo ya mwanzo yanatarajiwa kutangazwa...

Like
154
0
Monday, 15 February 2016
PROF. MBARAWA: SERIKALI BADO INA MASHAKA NA WATENDAJI ATCL
Local News

WAZIRI wa ujenzi, uchukuzi na mawasiliano Profesa  Makame Mbarawa amesema Serikali bado ina mashaka na watendaji wa shirika la ndege la taifa ATCL na ili kuondoa dukuduku hilo inaendelea na uchunguzi wa kuwabaini watendaji wote waliohusika kulihujumu shirika hilo. Profesa Mbalawa ameyasema hayo jijini Mwanza kwenye mkutano wa sita wa sekta ya uchukuzi  katika ukanda wa Afrika ya kati kwa lengo la kutathmini maendeleo katika sekta hiyo pamoja na changamoto zake  uliowakutanisha mawaziri wa sekta hiyo kutoka nchi tano za...

Like
193
0
Monday, 15 February 2016
NJOMBE: UONGOZI WA HOSPOTALI YA HALMASHAURI UMEPEWA SIKU 90 KUREKEBISHA MAPUNGUFU YA UTOAJI WA HUDUMA ZA AFYA
Local News

UONGOZI wa Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Njombe umepewa muda wa siku 90 kurekebisha mapungufu ya utoaji wa huduma za afya, vinginevyo  hospitali hiyo itafungwa.   Kauli hiyo imetolewa na Naibu Waziri wa Afya,Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dkt. Hamisi Kigwangalla wakati akizungumza na viongozi, Mganga Mkuu wa Mkoa, Samwel Mgema na Mkurugenzi wa halmashauri hiyo, Imelda Mwenda na watumishi wa hospitali hiyo. Dkt. Kigwangalla alitoa agizo kufuatia ziara yake ya ukaguzi wa hospitali, vituo vya afya...

Like
312
0
Monday, 15 February 2016
SYRIA: MATAIFA YAAFIKIANA KUSITISHA MAPIGANO
Global News

MATAIFA yenye ushawishi duniani yameafikiana kuhusu mkataba wa kusitisha mapigano nchini Syria ambao utaanza kutekelezwa katika kipindi cha wiki moja ijayo. Makubaliano hayo yamefikiwa baada ya mazungumzo nchini Ujerumani. Mwafaka huo hata hivyo hautahusisha makundi ya kijihadi ya Islamic State (IS) na al-Nusra Front. Aidha, Mawaziri wa mataifa wanachama wa Kundi la Kimataifa la Kusaidia Syria pia wamekubaliana kuharakisha na kuongeza juhudi za kutoa...

Like
174
0
Friday, 12 February 2016
ICC: HATMA YA RUTO KUFAHAMIKA LEO
Global News

MAHAKAMA ya jinai ya kimataifa -ICC leo inatarajiwa kutoa uamuzi ambao huenda ukakuwa na athari kwa kesi inayomkabili naibu rais wa Kenya William Ruto. Bwana Ruto na mushtakiwa mwenzake, mwana Habari, Joshua Arap Sang wameshitakiwa kwa makosa ya uhalifu dhidi ya binadamu kuhusiana na ghasia zilizotokea nchini Kenya baada ya uchaguzi mkuu wa 2007. Mashtaka kama hayo yaliyomkabili rais Uhuru Kenyatta yalifutiliwa mbali na mwendesha mkuu wa mashataka ya ICC, Fatou Bensouda kwa ukosefu wa...

Like
241
0
Friday, 12 February 2016
KIGWANGALLA: TUTAENDELEA KUTUMBUA MAJIPU
Local News

NAIBU Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Watoto na Wazee Dk. Hamisi Kigwangalla amesema kwamba wao kama viongozi wataendelea kumsaidia Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, MheshimiwaDkt. John Pombe Magufuli kutumbua majibu yanayokwamisha kutokupatikana kwa huduma bora za afya ,bila kuogopa wala kumwonea mtu kwa ajili ya maslahi ya  taifa.   Dokta Kigwangala ameyasema hayo  wakati wa maadhimisho ya 24 ya ibada maalum ya kuwaombea  wagonjwa Duniani ambayo Kitaifa yamefanyika katika jimbo Kuu la Tabora  na baadae kwenye...

Like
184
0
Friday, 12 February 2016
TRA YANASA SHEHENA KUBWA YA BIDHAA ZA MAGENDO
Local News

MAMLAKA ya Mapato Tanzania (TRA) imefanikiwa kukamata bidhaa za magendo kwenye maeneo mbalimbali ya Ukanda  wa Bahari ya Hindi, Ziwa Victoria na mipakani.   Taarifa hiyo imetolewa na Mkurugenzi wa Huduma na Elimu kwa Mlipa Kodi (TRA) Bw. Richard Kayombo katika mahojiano maalum yaliyofanyika  ofisini kwake Jijini Dar es Salaam kuhusu juhudi za operesheni ya kutokomeza bidhaa za magendo nchini.   Amesema kuwa katika operesheni hiyo, TRA imefanikiwa kukusanya kodi ya zaidi ya shilingi milioni kumi kutoka katika bidhaa zilizokuwa...

Like
254
0
Friday, 12 February 2016