Slider

SYRIA: MASHAMBULIZI MAPYA KUCHUNGUZWA
Global News

WAZIRI wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry amesema madai yote ya kuvunja muafaka wa kusitisha mashambulizi nchini Syria yatachunguzwa. Hata hivyo Kerry amesisitiza kwamba Marekani na Urusi wameafikiana kutojadili madai hayo hadharani. Ameongeza kuwa pande hizo zimekubaliana kuhakikisha mashambulizi yanalenga ngome za wapiganaji wa Islamic State na Al-Nusra Front pekee....

Like
197
0
Tuesday, 01 March 2016
SENETA WA NEBRASKA AKATAA KUMUUNGA MKONO TRUMP
Global News

SENETA wa Nebraska- Ben Sasse amesema hatamuunga mkono mgombea urais anayeongoza miongoni mwa wagombea wa chama cha Republican Donald Trump. Sasse ndiye mwanachama wa kwanza wa ngazi ya juu wa chama cha Republican aliyejitokeza kutangaza hadharani kwamba hatamuunga mkono Trump. Amesema amesikitishwa sana na kuvunjwa moyo na mfanyabiashara huyo na kwamba atamtafuta mgombea mwingine wa kumuunga mkono iwapo Trump atashinda uteuzi wa Republican....

Like
232
0
Tuesday, 01 March 2016
TRA YANASA CD NA DVD ZA MUZIKI NA FILAMU ZISIZOLIPIWA KODI
Local News

MAMLAKA ya Mapato Tanzania-TRA-kwa kushirikiana na Jeshi la Polisi imefanya ukaguzi wa stempu za kodi kwenye kazi za wasanii na kufanikiwa kukamata CD na DVD za Muziki na filamu 7, 780 ambazo hazina stempu za kodi. Mkurugenzi wa huduma na Elimu kwa mlipa kodi Richard Kayombo ameyasema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa Habari ofisini kwake. Kayombo amesema kuwa msako huo ulioanza Februari 26 katika maeneo mbalimbali ya mkoa wa Dar es salaam umebaini ukiukwaji wa sharia kutoka kwa...

Like
278
0
Tuesday, 01 March 2016
KIPINDUPINDU BADO NI CHANGAMOTO
Local News

JUMLA ya Wagonjwa wapya 473 wamegundulika kuwa na vimelea vya Ugonjwa wa kipindupindu huku Watu 9 wakipoteza maisha kutokana na ugonjwa huo katika kipindi cha wiki iliyoanza Februari 22 hadi 28 huku ripoti ikionesha kuwa ugonjwa huo bado umeendelea kusambaa kwa kasi. Akizungumza na Wanahabari Jijini Dar es salaam Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya jamii, Jinsia, Wazee na Watoto Dokta Hamisi Kigwangala amewata Wananchi kuongeza juhudi za usafi wa afya zao na mazingira kwa kuhakikisha kuwa wanazingatia kanuni za...

Like
195
0
Tuesday, 01 March 2016
ZUMA ALAANI MATUKIO YA KUCHOMA MOTO VYUO AFRIKA KUSINI
Global News

RAIS wa Afrika Kusini Jacob Zuma amelaani matukio ya kuchomwa moto kwa vyuo vikuu nchini humo.   Rais Zuma amesema hasira haipaswi kuwafanya baadhi ya  wanafunzi kufanya vitendo vinavyoweza kuwakosesha kupata huduma ya elimu pamoja na wenzao.   Kauli hiyo ya Rais Zuma inafuatia matukio ya hivi karibuni yanayodaiwa kufanywa na wanafunzi nchini humo ya  kuyachoma moto majengo ya vyuo kadhaa kwa madai ya kupinga ongezeko la ada za masomo pamoja na masuala ya...

Like
187
0
Friday, 26 February 2016
BAGHDAD: SHAMBULIZI LA KUJITOA MUHANGA LAUA WATU 15
Global News

  KIASI cha watu 15 wameuawa kufuatia shambulizi la kujitoa muhanga linalodaiwa kufanywa na watu wawili wanaoshukiwa kuwa   na mahusiano na wanamgambo wa  kundi la itikadi kali la Dola la Kiisilamu katika eneo la msikiti wa kishia mjini Baghdad.   Kwa mujibu wa vyanzo vya habari vya madaktari na polisi   watu wengine 50 wanadaiwa kujeruhiwa katika tukio hilo.   Duru zinaarifu kuwa mtu wa kwanza  alijitoa muhanga na kufuatiwa  na wa pili ambaye pia alijilipua baada ya maafisa usalama kufika...

Like
224
0
Friday, 26 February 2016
WAZIRI MBARAWA AZITAKA TAASISI ZILIZO CHINI YA WIZARA YAKE KUFANYA KAZI KWA WELEDI
Local News

WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Prof. Makame Mbarawa amezitaka taasisi zote zilizo chini ya wizara hiyo kufanya kazi kwa uwazi, weledi na uaminifu ili kuongeza mapato na kutimiza adhma ya Serikali ya kufikia uchumi wa kati ifikapo 2025.   Prof. Mbarawa ametoa wito huo mkoani Kilimanjaro katika majumuhisho ya ziara yake ya mikoa ya Manyara, Arusha na Kilimanjaro iliyolenga kukagua miradi ya ujenzi wa barabara, viwanja vya ndege, Posta, TTCL, TBA na TEMESA.   Waziri Mbarawa amewataka mameneja na...

Like
171
0
Friday, 26 February 2016
JAMII IMETAKIWA KUUNGA MKONO UKUZAJI WA VIPAWA
Local News

JAMII nchini imetakiwa kuunga mkono jitihada mbalimbali zinazofanya na baadhi ya taasisi zinazo jihusisha na utoaji wa ujuzi na uendelezaji wa vipawa vya watoto na vijana ili kujenga jamii yenye tabia ya kujitegemea . Hayo yamebainishwa na Mkude Kilosa ambaye ni  mkurugenzi msaidizi wa kituo cha kulelea watoto na vijana cha baba watoto kilichopo jijini Dar es salaam wakati akizungumza na efm  juu ya maandalizi ya tamasha la wazi la sarakasi tamasha lililolenga kukuza na kuendeleza ujuzi wa vijana katika...

Like
200
0
Friday, 26 February 2016
WFP LATOA MSAADA DEIR EL-ZOUR
Global News

MKUU wa Umoja wa Mataifa anayehusika na utoaji wa misaada ya kibinaadamu, Stephen O’Brien, amesema shirika la Mpango wa Chakula duniani, WFP, limedondosha chakula kutoka angani katika mji wa Deir el-Zour, ambao umekuwa ukizingirwa na kundi la Dola la Kiislamu. O’Brien ameliambia baraza la usalama la umoja huo mjini New York kwamba tani 21 za msaada zilidondoshwa. Hata hivyo msemaji wa WFP Bettina Luescher amesema katika taarifa yake kwamba operesheni nzima ilikabiliwa na changamoto za...

Like
198
0
Thursday, 25 February 2016
WANAJESHI 180 WA KENYA WALIUAWA NA AL-SHABAB
Global News

RAIS wa Somalia Hassan Sheikh Mohamoud ametoa maelezo kuhusu idadi ya wanajeshi wa Kenya waliofariki kufuatia shambulio la al-Shabab katika kambi yao huko el-Adde mwezi uliopita.   Rais huyo ametoa idadi hiyo kuwa kati ya wanajeshi 180 na 200 katika mahojiano na runinga moja ya Somali ,Cable TV.   Wapiganaji hao wa al-Shabab wamesema kuwa wanajeshi 100 walifariki na Kenya bado  haijatoa idadi yoyote ya wanajeshi wake...

Like
192
0
Thursday, 25 February 2016
SERIKALI YATAKIWA KUWEKEZA ZAIDI KATIKA UBORA WA ELIMU
Local News

SERIKALI ya awamu ya tano imetakiwa kuwekeza zaidi katika ubora wa elimu na sio katika kutanua upatikanaji na nafasi ya elimu ili kutekeleza sera ya Elimu bure kwa Shule za Serikali kwa kuwa tafiti zinaonesha kuwa kiwango cha ufaulu katika miaka 10 iliyopita kimeshuka katika Shule za Msingi na Sekondari licha ya mfumo huo kutumika katika elimu ya msingi.   Hayo yamesemwa leo jijini Dar es salaam wakati wa uwasilishaji wa ripoti iliyotolewa na Twaweza kuhusu maoni ya Wananchi juu...

Like
224
0
Thursday, 25 February 2016