Slider

SERIKALI IMEOMBWA KUBORESHA UPATIKANAJI WA HUDUMA YA AFYA KWA WATU WENYE ULEMAVU
Local News

SERIKALI imeombwa kuboresha upatikanaji wa huduma ya afya kwa watu wenye ulemavu na mahitaji maalum kwenye hospitali zake. Rai hiyo nimetolewa jijini Dares salaam na Katibu Mkuu wa chama cha watu wenye ulemavu wa ngozi –Albinisim, bwana Gaston Mcheka alipokuwa akizungumza na kituo hiki kuhusiana na changamoto wanazokutana nazo wanapokwenda kupata huduma hizo. Mcheka amesema, kumekuwa na unyanyapaa mkubwa kwa watendaji wa hospitali hizo na kuonekana kutokuwa na thamani ya kuhudumiwa kwa haraka suala linalowafanya wajione...

Like
235
0
Wednesday, 16 March 2016
UEFA: MAN CITY YATINGA ROBO FAINALI
Slider

Manchester City wamefika robofainali Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya kwa mara ya kwanza licha ya kutoka sare na Dynamo Kiev mechi ya marudiano. City, waliokuwa mbele 3-1 kutokana na ushindi wa mechi ya kwanza, walidhibiti mechi ingawa waliwapoteza mabeki Vincent Kompany na Nicolas Otamendi kutokana na majeraha mapema. Kipindi cha kwanza hakuna aliyetishia mwenzake lakini kipindi cha pili Jesus Navas aligonga mlingoti kwa kombora la chini naye Yaya Toure akatoa kombora ambalo lilitua mikononi mwa kipa. Manuel Pellegrini, atakayeondoka mwisho...

Like
200
0
Wednesday, 16 March 2016
PUTIN AAGIZA MAJESHI YA URUSI KUONDOKA SYRIA
Global News

RAIS wa Urusi Vladimir Putin ametoa amri kwa wanajeshi wake waliopo Syria kurejea nyumbani haraka kwa sababu tayari wametekeleza asilimia kubwa ya malengo yao. Tangazo lake hilo limewaacha wachambuzi wengi wakiwa na mshangao kwani hakukuwa na dalili zozote za kuwepo kwa tukio kama hilo. Aidha Putin ametangaza hilo katika siku ambayo mazungumzo ya amani yameanza upya mjini Geneva Uswisi....

Like
238
0
Tuesday, 15 March 2016
KOREA KASKAZINI YATANGAZA KUFANYA JARIBIO LA NYUKLIA
Global News

KIONGOZI wa Korea Kaskazini Kim Jong-un ametangaza kwamba Taifa hilo litafanya majaribio ya silaha zake za nyuklia na makombora ya masafa marefu hivi karibuni. Kim Jong-un ametoa Tangazo lake alipokuwa akiongoza maonesho ya teknolojia ambayo inahitajika kuwezesha kombora lenye kilipuzi cha nyuklia kuingia tena ardhini baada ya kurushwa anga za juu. Shirika hilo limemnukuu kiongozi huyo akisema kuwa majaribio hayo yatafanyika na yataisaidia Korea Kaskazini kujiimarisha katika utekelezaji wa mashambulio ya...

Like
227
0
Tuesday, 15 March 2016
KAGERA :AFISA MIFUGO ANUSURIKA KUFUKUZWA KAZI
Local News

AFISA MIFUGO wa kata ya Kakunyu, wilayani Misenyi mkoani Kagera, Eric Kagoro amenusurika kufukuzwa kazi kwenye mkutano wa hadhara kutokana na sakata la kuruhusu ng’ombe 291 kulishwa kwenye ranchi ya mifugo ya Misenyi. Tukio hilo limetokea jana baada ya Waziri Mkuu Mheshimiwa Kassim Majaliwa kuhoji juu ya malalamiko aliyoyapata kutoka kwa wananchi kuwa Afisa huyo ndiye aliyeruhusu mifugo hao kuingia kwenye eneo hilo. Katika mkutano huo Waziri Mkuu amewaasa watendaji wa kata na vijiji kutotumia nafasi zao kuleta migogoro baina...

Like
374
0
Tuesday, 15 March 2016
RAIS MAGUFULI AWAAPISHA RASMI WAKUU WA MIKOA 26
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dokta John pombe Magufuli amewaapisha rasmi wakuu wa mikoa 26 wa Tanzania Bara aliowateua machi 13 mwaka huu. Hafla ya kuwaapisha wakuu hao wa mikoa imefanyika Ikulu Jijini Dar es salaam na kuhudhuliwa na viongozi mbalimbali wa kitaifa akiwemo makamu wa Rais Bi. Samia Suluhu Hassan. Baadhi ya wakuu wa mikoa walioapishwa leo ni pamoja na Mheshimiwa Said Meck Sadiki ambaye amekuwa mkuu wa mkoa wa Kilimanjaro, Mheshimiwa Paul Makonda mkuu wa mkoa...

Like
197
0
Tuesday, 15 March 2016
ANGELA MERKEL ACHEMKA UCHAGUZI WA MAJIMBO
Global News

CHAMA cha Chansela wa Ujerumani Angela Merkel kimeshindwa katika uchaguzi wa majimbo, matokeo ya utafiti wa baada ya uchaguzi yanaonesha. Chama cha AfD kinachowapinga wahamiaji, kimeimarika kwa kiwango kikubwa katika majimbo yote matatu. Uchaguzi huo ulitazamwa na wengi kama kigezo cha uungwaji mkono wa sera ya kansela Merkel ya kuwapokea wakimbizi, ambapo zaidi ya wakimbizi na wahamiaji milioni moja waliingia Ujerumani mwaka 2015....

Like
222
0
Monday, 14 March 2016
ISRAEL YATOA WITO KWA MATAIFA YENYE NGUVU KUIADHIBU IRAN
Global News

ISRAEL imetoa wito kwa mataifa yenye nguvu duniani kuiadhibu Iran kwa jaribio lake la hivi karibuni la kurusha makombora ya masafa marefu.   Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Israel inapeleka dai hilo kwa Marekani, Urusi, China, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani-mataifa ambayo yamesaini mpango wa kuiondoshea Iran vikwazo kwa makubalino ya taifa hilo kuachana na mpango wake wa nyuklia.   Netanyahu amesema Iran imekwenda kinyume na maazimio ya Umoja wa Mataifa kuhusu majaribio ya makombora, na mataifa hayo yenye...

Like
289
0
Monday, 14 March 2016
HUDUMA YA USAFIRI YAREJEA RELI YA KATI
Local News

HUDUMA ya usafiri wa reli ya Kati iliyokuwa imesimama kwa takribani miezi miwili sasa imerejea kufuatia kukamilika kwa ukarabati wa reli hiyo katika eneo la kidete wilayani kilosa, mkoani Morogoro. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema hayo baada ya kukagua na kuridhika na ukarabati uliofanywa katika maeneo ya Magulu, Munisagara, Mzaganza na kidete Wilayani Kilosa.  ...

Like
229
0
Monday, 14 March 2016
SERIKALI YAIPANDISHA HADHI ZAHANATI YA MSOGA KUWA HOSPITALI YA WILAYA
Local News

SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeipa hadhi ya kuwa Hospitali Wilaya iliyokuwa Zahanati ya Msoga ambayo tayari imekamilisha jengo lake jipya la Hospitali hiyo inayotarajia kuanza kazi Mwezi Aprili mwaka huu.   Akitoa maagizo hayo baada ya ukaguzi wa timu ya wataalam kutoka Wizara hiyo ya Afya , Naibu Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla waliofanya hivi karibuni katika Hospitali hiyo, ameeleza kuwa kuanzia Mwezi Aprili...

Like
672
0
Monday, 14 March 2016
KEDRICK LAMAR AITENDEA HAKI BEAT YA PHARELL WILLIAMS
Entertanment

Kwa mujibu wa taarifa zilizotoka hivi karibuni inadaiwa kuwa producer Pharell Williams na mwenzie walitengeneza beat ya ngoma ya Kendrick Lamar ilioshinda Award kibao na kisha kutiwa vokali na rappa mwengine mkubwa mwaka moja kabla ya rappa lamar kupewa na kufanya alichofanya. Mwaka 2014 katika party moja baada ya grammy ilidaiwa kuchezwa clip moja ambayo ilisikika kama wimbo huo alisema shahidi mmoja, akasema aidha ilikua ni sauti ya pusha T au fabolous ndie alirap katika biti hiyo. je kwako unadhani...

Like
407
0
Monday, 14 March 2016