Rais John Magufuli amewataka watendaji wanaosimamia mradi wa mabasi ya mwendo kasi jijini Dar es Salaam (Dart) kuhakikisha unaingiza faida kinyume na hapo hasara itakuwa kwao. Aidha, Rais Magufuli aliwataka mawaziri wanaosimamia mradi huo, George Simbachawene (Tamisemi) na Profesa Makame Mbarawa (Ujenzi) kumpatia taarifa inayoeleza kiasi cha fedha kilichoingia tangu mabasi hayo yaanze kufanya...
Kocha wa Ghana Avram Grant amesema anataka kufika mbali zaidi katika fainali za mwaka huu tofauti na ilivyokuwa mwaka 2015 walipofungwa na Ivory Coast kwa njia ya penalti. Mshambuliaji Asamoah Gyan na kiungo wa West Ham Andre Ayew walikuwa miongoni mwao miaka miwili iliyopita na uzoefu wao unatarajiwa kuwasaidia katika mchezo wa leo. Wachezaji wa Uganda Murushid Juuko na Khalid Aucho wote hawatakuwepo katika mchezo huo. Cranes wanaingia katika michuano hiyo tokea mwaka 1978 walipopoteza dhidi ya Ghana katika hatua...
Rais wa Ufaransa Francois Hollande amepuuzilia mbali hatua ya Rais mteule wa Marekani Donald Trump kukosoa sera ya Ujerumani kuhusu wahamiaji barani Ulaya. Bw Hollande alisema hatua hiyo ya Bw Trump si ya busara. “ haihitaji ushauri kutoka nje, kuambiwa inafaa kufanya nini,” Bw Hollande alisema. Bw Trump alikuwa amesema Kansela wa Ujerumani Angela Merkel alifanya “kosa kubwa” kwa kuwaruhusu wahamiaji kuingia nchini mwake kwa wingi. Bi Merkel kwa upande wake, akijibu tamko hilo la Trump, alisema bara Ulaya linafaa...
Mwana anga wa Marekani Gene Cernan, aliyekuwa binadamu wa mwisho kutembea kwenye Mwezi, amefariki dunia akiwa na miaka 82. Shirika la anga za juu la Marekani Nasa limesema limehuzunishwa sana kumpoteza mwana anga huyo mstaafu. Cernan alikuwa mmoja wa watu watatu pekee waliowahi kwenda Mwezini mara tatu na ndiye binadamu aliyeukanyaga Mwezi mara ya mwisho kabisa, mwaka 1972. Maneno yake ya mwisho aliyoyasema kabla ya kuondoka kwenye Mwezi yalikuwa: “Tunaondoka jinsi tulivyokuja na, Mungu akitujalia, tutarejea na amani na matumaini...
Marekani imesitisha sera ya muda mrefu ambayo ilikuwa inawapa raia wa Cuba hadhi maalumu ya kuingia na kuishi nchini Marekani bila ya visa. Serikali ya Cuba imekuwa ikilalamika kwamba, sera hiyo, ijulikanayo kama “wet foot, dry foot,” imewafanya maelfu ya raia wa Cuba kukimbia nchini humo kila mwaka. Rais Obama amesema hatua ya kuondolewa kwa sera hiyo, ni hatua muhimu katika kurudisha uhusiano na Cuba. Mahasimu hao wa muda mrefu wamerudisha uhusiano wa kidiplomasia mnamo mwaka 2015 baada ya karne...
Waziri wa ulinzi wa Ufaransa, amesema mitandao ya idara za ulinzi za nchi zilishambuliwa mara 24,000 mwaka jana peke yake lakini udukuzi huo ulizimwa. Jean Yves-Le Drian, alisema udukuzi kama huo unaongezeka mara dufu kila mwaka. Alionya kuwa miundo mbinu ya taifa iko kwenye hatari, na kwamba kunaweza kufanywa jaribio la kuchafua uchaguzi wa mwaka huu. Bwana Le Drian amekuwa akisimamia mabadiliko makubwa katika mifumo ya mitandao ya Ufaransa, ambapo mkuu wa jeshi ataongoza operesheni mpya za komputa, Cybercom. Waziri...
Waziri wa Mambo ya Nje wa Uingereza Boris Johnson amekutana na washauri wakuu wa rais mteule wa Marekani Donald Trump mjini New York, Marekani. Johnson alikuwa na shemejiye Trump, Jared Kuchner, na afisa mkuu wa mikakati wa Bw Trump Steve Bannon. Huo ulikuwa mkutano wa kwanza wa ana kwa ana kati ya maafisa wa Trump na waziri wa Uingereza. Maafisa wanasema kwenye mkutano huo, sera ya Marekani kuhusu Syria, China na Urusi ilijadiliwa. Jumatatu, Bw Johnson atakuwa mjini Washington D.C,...
Mshambuliaji wa Real Madrid Cristiano Ronaldo amemshinda mpinzani wake Lionel Messi na kupata tuzo ya mchezaji bora wa dunia Ballon d’Or hii ikiwa ni kwa mara ya nne. Ronaldo mwenye miaka 31 sasa anahitaji tuzo moja tu kumfikia Messi ambaye mwaka jana alipata tuzo ya tano. Mshambuliaji wa Atletico Madrid na timu ya taifa ya Ufaransa Antoine Griezmann amemaliza katika nafasi ya tatu. Ronaldo aliisaidia Madrid kushinda ligi ya mabingwa ulaya msimu uliopita sambamba na kuisaidia nchi yake ya Ureno...
Mpango wa uuzwaji wa klabu ya Ac Milan wasogezawa mbele hadi mwakani mwezi wa tatu. Klabu hiyo ya nchini Italy inayomilikiwa na aliyewahi kuwa waziri mkuu wa nchi hiyo Bwana Silvio Berlusconi ilitajwa kuuzwa kwa wawekezaji wa China mwezi huu wa kumi na mbili lakini mpango huo umesogezwa mbele hadi mwakani mwezi wa...
Waamuzi waliochezesha mchezo namba 49 kati ya Yanga na Simba, Martin Saanya na Samweli Mpenzu wametolewa kwenye ratiba ya Ligi Kuu ya Vodacom Tanzania Bara, huku suala lao likipelekwa kwenye Kamati ya Waamuzi ili ishughulikie tatizo lao kitaalam. Maamuzi hayo yamefanyika baada ya Kikao cha Kamati ya Usimamizi na Uendeshaji ya Bodi ya ligi, kuwaita na kuwahoji na kuangalia mkanda wa mchezo husika. Kamati imebaini mapungufu mengi ya kiutendaji yaliyofanywa na waamuzi hao, na hivyo kuitaka kamati ya waamuzi ishughulikie....
Kiongozi wa Sudan Omar el Bashir amempongeza rais mteule wa Marekani Donald Trump akisema kuwa itakuwa rahisi kushirikiana naye, kulingana na gazeti la Emirati al Khaljee. ”Bw Trump anaangazia maslahi ya raia wa Marekani, ikilinganishwa na wale wanaozungumzia kuhusu demokrasia ,haki za kibinaadamu na uwazi”,alisema rais Bashir katika mahojiano na gazeti hilo. Aliongezea kwamba: Tunaweza kushirikina na watu wenye sura mbili lakini huyu hapa mtu mwenye uwazi wa anajua anacholenga. ”Nina hakika itakuwa rais kushirikiana na Trump...