Kariu kwenye meza ya magazeti ya e-digital, leo jumatano tarehe 14, March tumekuwekea headline zote za magazeti ya udaku, hardnews na michezo...
Rais Donald Trump amemfukuza kazi waziri wake wa mambo ya nchi za nje Rex Tillerson na kumchagua mkurugenzi wa idara ya ujasusi ya CIA, Mike Pompeo kuchua nafasi yake. Nafasi ya Pompeo katika CIA itachukuliwa na aliyekua naibu wake Gina Haspel. Katika ujumbe wa twitter, Rais Trump alimshukuru Tillerson akisema, “Mike Pompeo, Mkurugenzi wa CIA atakua waziri mpya wa mambo ya kigeni. Atafanya kazi nzuri kabisa. Ahsante Rex Tillerson kwa huduma yako! Gina Haspel atakua mkurugeni mpya wa CIA na...
Waziri wa habari utamaduni sanaa na michezo Dr. Harison Mwakyembe amewaonya maofisa habari wa serikali ambao hawatangazi kazi za maendeleo zinazofanywa na serikali watachukuliwa hatua ikiwemo kufukuzwa kazi. Dr. Mwakyembe ametoa kauli hiyo wakati wa ufunguzi wa mkutano wa wananchama wa chama cha maafisa mahusiano serikalini unaofanyika mkoani Arusha, nakusema maafisa habari wa serikali ambao wanatumia vifaa walivyopewa kwa matumizi yao binafsi pamoja na wale wanaokaa maofisini bila kufanya kazi nakusubiri muda wakutoka. Kwa upande wa...
Hatua ya robo fainali ya Kombe la Shirikisho ‘Azam Sports Federation Cup’ inatarajia kuendelea Ijumaa ya Machi 30 2018 kwa mchezo mmoja kupigwa. Stand United itakuwa nyumbani kupambana na Njombe Mji katika Uwanja wake wa nyumbani, CCM Kambarage, mchezo utakaoanza saa 10 kamili jioni. Baada ya mchezo huo siku ya Ijumaa, michezo hiyo itaendelea tena Jumamosi ya Machi 31 2018 kwa mechi mbili, Tanzania Prisons itacheza na JKT Tanzania kwenye Uwanja wa Sokoine Mbeya majira ya saa 8 mchana. Na...
Tshitshimbi ametwaa tuzo ya mchezaji bora wa mwezi Februari na kuwashinda Emanuel Okwi wa Simba na Buswita. Ametwwa Tuzo hiyo baada ya kutupia mabao matatu na kukisaidia kikosi chake cha Yanga kuibuka na alama 12. Katika kinyang’anyiro hicho Tshitshimbi ameshindana na Pius Buswita wa Yanga SC na Emmanuel Okwi wa Simba SC. Kawaida mshindi wa tuzo hiyo huzawadiwa kitita cha milioni moja pamoja na king’amuzi cha Azam...
Mchezaji wa zamani wa Liverpool, Philippe Coutinho anasema kuwa angependelea mshambuliaji wa Brazil mwenye umri wa miaka 26 Neymar kurudi Barcelona. Neymar alijiunga na PSG kutokea Barca kwa dau lililovunja rekodi la £198m mwisho wa msimu uliopita na kupelekea Barcelona kumsajili Coutinho, amabapo kwa sasa ameweza kufiti katika timu hiyo ya Nou Camp....
Rais wa klabu ya TP Mazembe ya katika Jamhuri ya kidemokrasia ya Congo, Moise Katumbi amejitosa kwenye ulingo wa siasa, anazindua chama chake akiwa Afrika Kusini. Katumbi ni kiongozi wa upinzani ambaye yupo uhamishoni kutoka DR Congo baada ya kutengana na Rais Joseph Kabila. Katumbi ambaye amewahi kuwa Gavana wa jimbo tajiri zaidi nchini humo Katanga alijiuzulu na kumshtumu rais Kabila kwa uongozi duniani. Moise Katumbi ni kiongozi wa pekee wa upinzani nchini Congo ambaye ana ushawishi mkubwa na ufuasi...
Akifunga kikao kazi cha siku mbili kati ya Menejimenti ya HESLB na maafisa wanaosimamia madawati mikopo kutoka taasisi za elimu ya juu zaidi ya 70 mwishoni mwa wiki mjini Morogoro, Katibu Mkuu wa Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia Dkt. Leonard Akwilapo amewataka viongozi wa taasisi hizo kuhakikisha maafisa wao wana vitendea kazi vya uhakika na wanapata ushirikiano wa kutosha. Madawati hayo ya mikopo yalianzishwa mwaka 2011 katika taasisi zote za elimu ya juu kufuatia maelekezo ya Serikali ili...
Watu takriban 20 wamefariki dunia na wengine wengi kujeruhiwa baada ya mti mkubwa kuwaangukia wakiogelea katika maporomoko ya maji eneo la Kintampo, Ghana. Maporomoko hayo ni maarufu sana kwa watalii. Watu hao walikuwa wakiogelea pale upepo mkubwa ulipoangusha mti na kusababisha mkasa huo, maafisa wa huduma za dharura wamesema. Msemaji wa taifa wa huduma za dharura Prince Billy Anaglate alisema kisa hicho kilitokea katika maporomoko ya Kintampo, katika jimbo la Brong-Ahafo. Kikosi cha pamoja na polisi na wahudumu za dharura...
Mabingwa watetezi wa Kombe la FA Uingereza upande wa wawanawake Kina dada wa Arsenal waliwalaza wapinzani wao Tottenham 10-0 na kufika robo fainali Jumapili. Danielle van de Donk alifungia wenyeji hao mabao matatu, naye mshambuliaji wa zamani wa Sunderland Beth Mead akafunga bao pia mechi yake ya kwanza kuchezea Arsenal. Chelsea, ambao walishindwa na Arsenal fainali mwaka jana, pia walipata ushindi mkubwa, kwa kulaza Doncaster 7-0. Bristol City walilaza Millwall 5-0. Liverpool, Notts County, Birmingham na Sunderland pia walishinda kwenye...
Kampuni ya azimio estate iliyompa zawadi mkuu wa mkoa Dar es salaam, Paul Makonda inadaiwa kuhusika na wizi mkubwa wa pesa ya umma, baada ya kampuni hiyo kuingia mkataba na Shirika la taifa la hifadhi ya jamii (Nssf) wakuiuzia ardhi ekari 20,000 eneo la Dege Mbutu Kigamboni kwa makubaliano ya kila eka moja ni miloni ishirini na tano ( 25,000,000/=), serikali ikalipa pesa yote. Serikali imekuja kupewa eka 3,000 tu hali inayotafsiriwa kuwa sasa imeuziwa eka moja kwa zaidi milioni...