SAKHO MGUU NDANI,MGUU NJE NDANI YA LIVERPOOL
Slider

Maisha ya mlinzi wa kati wa Liverpool Mamadou Sakho yanaonekana kuanza kuwa magumu baada ya kocha wa klabu hiyo Jurgen Klopp kuamuru nyota huyo arudi nchini England kutoka Calfonia Marekani ambapo timu hiyo imeweka kambi kujiandaa na msimu mpya wa ligi kuu ya nchini England inayoanza kutimua vumbi mwezi ujao. Kwa mujibu wa vyombo vya habari vya uingereza kocha Jurgen Klopp hajafurahishwa na mwenendo wa kitabia wa nyota huyo mwenye umri wa miaka 26 kwenye kambi yao huko Marekani nakuagiza...

Like
266
0
Tuesday, 26 July 2016
NEC YATAKA TUME HURU
Local News

Dar es Salaam. Baada ya kukamilisha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba mwaka jana kwa mafanikio, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (NEC) imetoa mapendekezo saba kwa Serikali ili iyashughulikie kwa lengo la kuboresha uchaguzi ujao. Mapema mwezi huu, Mwenyekiti wa NEC, Jaji mstaafu, Damian Lubuva akiwa sambamba na wajumbe wengine wa taasisi hiyo na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC), walikabidhi ripoti ya uchaguzi huo kwa Rais John Magufuli. Licha ya kueleza mafanikio yaliyopatikana katika kipindi chote cha mchakato huo, kuanzia...

Like
242
0
Tuesday, 26 July 2016
SUMTRA KUISHTAKI UDART KWA KUTOZA NAULI ZAIDI
Local News

Dar es Salaam. Mamlaka ya Udhibiti wa Usafiri wa Majini na Nchi Kavu (Sumatra), imesema wakati wowote kuanzia sasa itaufikisha mahakamani uongozi wa Mabasi ya Kwenda Haraka (Udart) kwa tuhuma za kuwatoza abiria nauli zaidi kinyume na matangazo yao. Mkurugenzi Mkuu wa Sumatra, Gilliard Ngewe alisema jana jijini Dar es Salaam kuwa, mashtaka dhidi ya uongozi huo yameshaandaliwa na kilichobaki ni kuyafikisha mahakamani. Ngewe alisema Udart inatoza nauli ya Sh650 badala ya 400 kwa ruti ya kutoka Mbezi hadi Kimara...

Like
387
0
Tuesday, 26 July 2016
LALIGA: HUU NDIO MKWANJA ULIOVUNWA NA BARCELONA KATIKA MSIMU WA 2015/16
Slider

Machampion wa kandanda nchini Hispania klabu ya Fc Barcelona imetangaza kuvuna kitita cha Euro million 679 katika msimu uliopita 2015/16 wa ligi kuu ya huko ‪#‎Laliga‬. Katika makusanyo hayo yaliyovunja rekodi klabu hiyo imetangaza kupata faida ya Euro milioni 29 baada ya makato ya kodi. Katika hatua nyingine klabu hiyo imetangaza mipango yake ya upanuzi wa dimba la Camp Nue kwa siku za usoni kupitia faida...

Like
387
0
Tuesday, 26 July 2016
SPORTPESA YA KENYA KUDHAMINI KLABU YA EPL
Slider

Kampuni ya mashindano ya bahati nasibu inayodhamini Ligi Kuu ya Kenya imetia saini mkataba wa kuwa mdhamini wa klabu ya Hull City ya Uingereza. Kampuni hiyo ya SportPesa, ambayo huandaa mashindano ya kubashiri matokeo ya mechi nchini Kenya, imetia saini mkataba wa kudhamini Hull City kwa misimu mitatu. Klabu ya Hull City ilifanikiwa kurejea kwenye Ligi ya Premia msimu utakaoanza mwezi ujao. Hull City watafungua msimu kwa mechi ya nyumbani dhidi ya mabingwa Leicester City. Kwa mujibu wa taarifa kutoka...

Like
289
0
Monday, 25 July 2016
DEBI YA MANCHESTER YATIBUKA
Slider

Mechi ya kirafiki kati ya miamba wa Uingereza, Manchester City na Manchester United, imefutiliwa mbali kutokana na mvua kubwa. Mechi hiyo ilikuwa imepangiwa kuchezewa uwanja waBirds Nest, Uchina na ingekuwa ya kwanza kwa mameneja wapya Pep Guardiola na Jose Mourinho. Jumapili, Mourinho alikuwa amedokeza kwamba hali katika uwanja huo ilikuwa mbaya. Hata kabla ya mechi kuahirishwa rasmi, Guardiola alikuwa amesema matumaini yake ni kwamba wachezaji wake wasiumie. City na United wamesema “waandalizi wa mchuano huu pamoja na klabu zote mbili”...

Like
246
0
Monday, 25 July 2016
INDIA: WATU WAPEWA LIKIZO KWENDA KUSHUHUDIA UZINDUZI WA FILAMU
Entertanment

Wafanyakazi wengi kusini mwa India leo wamepewa likizo kwa sababu ya filamu ya mwigizaji filamu inayoanza kuonyeshwa kwenye kumbi za sinema leo.Filamu hiyo ni ya mwigizaji nyota wa asili ya Tamil, Rajinikanth. Hatua hiyo imechukuliwa kuzuia watu kutumia visingizio kama vile kwamba wanaugua ili wasifike kazini. Inahofiwa wengine huenda hata wangezima simu zao au kutofika kazini bila kueleza sababu. Filamu hiyo kwa jina Kabali inaonyeshwa katika kumbi 12,000 za sinema leo. Rajinikanth, ni mmoja wa waigizaji wanaolipwa pesa nyingi sana...

Like
305
0
Friday, 22 July 2016
CAF YAPATA MDHAMINI MPYA
Slider

Shirikisho la Soka barani Africa (CAF) limepata mdhamini mpya baada ya kumalizika kwa mkataba wake na kampuni ya mawasiliano ya Orange. Orange imekuwa mdhamini mkuu wa mashindano makubwa ya CAF kwa miaka minane tangu 2009. Kabla ya hapo, kampuni nyingine ya mawasiliano ya MTN ndiyo iliyokuwa mdhamini kwa miaka minne. Sasa, mdhamini mpya atakuwa kampuni ya mafuta na gesi ya Total kutoka Ufaransa. Kampuni hiyo itaanza kwa kudhamini michuano ya Kombe la Taifa Bingwa Afrika mwaka 2017 ambayo itaandaliwa nchini...

Like
401
0
Friday, 22 July 2016
ANALIPWA KUBIKIRI WATOTO ILI KUONDOA MIKOSI MALAWI
Global News

Katika tamaduni nyingi kote duniani mwanamke anapoolewa huwa ni fahari kubwa sana akiwa ni bikira. Mathalan ni dhihirisho la mwanamke kuwa amelelewa na kutunzwa vyema. Ni dhihirisho la usafi. Hata hivyo jamii moja nchini Malawi haithamini ubikira wa watoto wao wa kike. Amini usiamini wazazi huwa wanamlipa ”Fisi” kumbikiri binti yao punde tu anapopata hedhi yake ya kwanza. Wanaamini kuwa binti ambaye ni bikira ni mkosi kwa jamii! Malimwengu haya. Wazazi na jamii kwa jumla katika maeneo mengi ya kusini...

Like
443
0
Thursday, 21 July 2016
POGBA AOMBA KUHAMIA MAN UNITED
Slider

Mshambulizi wa Ufaransa na Juventus Paul Pogba ameomba kuihama klabu hiyo ya Italia.Magazeti ya michezo nchini Italia yamechapisha habari hiyo kama kichwa kuwa Mfaransa huyo mwenye umri wa miaka 23 ameomba aruhusiwe kuondoka kwani posho lake linavutia. La Gazzetta dello Sport liliongoza na kichwa ”Pogba ameamua kuondoka Juventus”Gazeti hilo linadai kuwa mfaransa huyo amekwisha kubaliana posho lake na Mashetani wekundu huku ikisisitiza kuwa sababu kuu iliyomfanya makamu wa mwenyekiti wa klabu hiyo bwana Ed Woodward asiandamane na...

Like
247
0
Wednesday, 20 July 2016
WABUNIFU WA NDEGE WATAKIWA KUOMBA VIBALI
Local News

Licha ya kuwapo kwa wabunifu kadhaa za ndege na magari, huku wananchi wakitaka Serikali iwaunge mkono kwa kuwawezesha, huenda wengi wao wasifikie ndoto zao. Tayari mkazi wa Tunduma mkoani Songwe, Adam Kimikile (34) aliyetengeneza helikopta ni kama amepigwa ‘stop’ na Mamlaka ya Usafiri wa Anga Tanzania (TCAA) kujihusisha na utengenezaji au ubunifu wa ndege bila kufuata taratibu. TCAA imesema anayetaka kutengeneza ndege ama vifaa vyake, azingatie kanuni za usafiri wa anga na kupata kibali cha mkurugenzi wake mkuu na hatua...

Like
520
0
Wednesday, 20 July 2016
« Previous PageNext Page »