Klabu ya Chelsea ya Uingereza imemsajili mshambuliaji wa Ubelgiji mwenye asili ya Jamhuri ya Kidemokrasia ya Congo.Michy Batshuayi amehamia Chelsea kutoka klabu ya Marseille ya Ufaransa na kutia saini mkataba wa miaka mitano. Mamake ni Viviane Leya Iseka na babake Pino Batshuayi. Michy alikuwa na fursa ya kuchezea timu ya taifa ya DR Congo kutokana na asili ya wazazi wake lakini mwaka jana aliamua kuwa mchezaji wa Ubelgiji. Aliwachezea mechi ya kwanza dhidi ya Cyprus Machi 2015 na kufunga bao....
Waziri mkuu wa Israeli Benjamin Netanyahu ametua nchini Uganda katika ziara ya kwanza kabisa kwa kiongozi wa taifa hilo la kiyahudi kuzuru Afrika tangu mwaka wa 1987. Ziara hiyo ya siku 5 imeanzia Uganda, na kisha waziri Netanyahu anatarajiwa kuzuru Kenya, Rwanda na kisha Ethiopia. Ilikuwa kihoja kwa wageni waalikwa kuingia kwenye uwanja huo wa ndege kwani usalama uliimarishwa huku maafisa wa usalama wa Israeli wakishika doria na mbwa na walenga shabaha, mbali na upekuzi wa kawaida wa maafisa wa...
Kampuni ya Apple inadaiwa kutaka kuchukua umiliki wa huduma ya kusikiliza muziki ya moja kwa moja ya mwanamuziki Jay Z Tidal. Kampuni hiyo imeripotiwa kwamba inaangazia wazo la kuinunua huduma hiyo kutokana na ushirikiano wake na wanamuzika bingwa kama vile Kanye West na Madonna. Duru zimearifu jarida la Wall Street kwamba mazungumzo yameanza na huenda yakasababisha kupatikana kwa makubaliano. Msemaji wa Tidal amekana kwamba imefanya mazungumzo na Apple. Jay Z alizindua huduma hiyo mnamo mwezi Machi mwaka uliopita kama mpinzani...
Saudia inatarajiwa kuwapatia bangili za kielektroniki mahujaji wanaoelekea Mecca kwa Hajj ya mwaka huu ambalo ni kongomano kubwa la Waislamu kutoka kote duniani. Hatua hiyo inafuatia mkanyagano uliotokea mwaka uliopita ambapo zaidi ya mahujaji 750 wanaaminikia kuuawa huku wengine 900 wakijeruhiwa. Bangili hizo zitakuwa na habari za kibinafsi za kila hujaji pamoja na zile za matibabu kusaidia mamlaka ya Saudia kuwatambua na kuwalinda mahujaji hao. Takriban kamera 1000 pia zimewekwa. Bangili hiyo ya utambulisho itukuwa na habari muhimu kama vile...
Mbunge wa Jimbo la Mbeya Mjini, Joseph Mbilinyi amesimamishwa kuhudhuria vikao kumi vya bunge kuanzia leo June 30 mwaka huu baada ya kubainika kunyosha kidole cha kati kwa wabunge baada ya kukiri mbele ya Kamati ya Haki, Maadili na Madaraka kwamba alifanya kitendo hicho. Hata baada ya kuhojiwa Mbunge Mbilinyi alishindwa kumtaja Mbunge wa CCM aliyedaiwa kumtukana ili nae achukuliwe hatua na kamati hiyo. Bunge limeridhia adhabu hiyo iliyotolewa na kamati. Nae Mbunge wa Ubungo Chadema Saed Kubenea amesimamishwa kuhudhuria...
Waandalizi wa tuzo za Oscar wametangaza kuwa wamewaalika wanachama wapya zaidi kupiga kura ya maamuzi ya washindi wa mwaka huu, baada ya malalamishi makubwa ya mwaka uliopita ambapo walilaumiwa kwa kuyabagua makundi mengine ya watu. Waandalizi hao wa The Academy of Motion Picture Arts and Sciences wanasema wamewaalika karibu watu 700, wakiwalenga hasa wanawake na watu kutoka jamii za watu wachache. Miongoni mwa wale ambao wamealikwa kushiriki katika uteuzi wa washindi wa tuzo hizo ni wacheza filamu weusi, na vilevile...
Uingereza imezuia kuhudhuria mkutano wa viongozi wa Jumuiya ya Ulaya ambapo itakuwa mara ya kwanza kufanyiwa hivyo kwa miaka 40. Waziri Mkuu, David Cameron, hatakuwa mezani wakati viongozi wengine 27 wa mataifa wanachama wa Jumuiya ya Ulaya watakuwa wakihudhuria mkutano usio rasmi juu ya hatma ya muungano huo baada ya kuondoka kwa Uingereza. Uingereza imeambiwa ianzishe mpango wake wa kuondoka katika jumuiya hiyo bila kuchelewa. Rais wa Jumuiya ya Ulaya, Jean-Claude Junker, amesema kuwa shughuli za kutegua kujiondoa kwa Uingereza...
Profesa mmoja wa chuo kikuu amesifiwa nchini Ivory Coast kwa kumbeba mtoto wa mmoja wa wanafunzi wake mgongoni wakati wa masomo. Picha za Honore Kahi wa chuo cha Bouake, zimesambaa pakubwa kwenye mitandao ya kijamii. Alisema aliamua kumsaidia mwanamke katika darasa lake wakati mtoto alianza kulia. Picha zilizochukuliwa na mwanafunzi mwingine zinamuonyesha, bwana Kahi akifunza huku mtoto akiwa...
Suge Knight anamshtaki mwanamuzki mwenza wa R& B Chris Brown mahakamani pamoja na mmiliki wa kilabu moja ya usiku nchini Marekani kufuatia ufyatulianaji wa risasi uliotokea katika kilabu hiyo mwaka 2014. Mwanamuziki huyo wa zamani alipigwa risasi mara saba katika hafla ya Chris Brown. Kesi hiyo iliowasilishwa katika mahakama ya Los Angeles inamshtaki Chris Brown na kilabu ya West Hollywood Ckub 1 Oak kwa kushindwa kuweka usalama wa kutosha na kumruhusu mtu mmoja aliyejihami kuingia katika kilabu hiyo. Suge Knight...
Korea Kusini, Marekani na Japan zimefanya zoezi la ushirikiano la kukabiliana na makombora katika maji ya jimbo la Hawaii. Hatua hiyo inajiri kufuatia msururu wa majiribio ya makombora ya masafa mafupi katika miezi ya hivi karibuni inayofanywa na Korea kaskazini. Majaribio mengi hatahivyo hayakufanikiwa lakini ufanisi wa kombora la sita hivi majuzi ulilishangaza eneo hilo. Korea Kaskazini ambayo imefanya majaribio manne ya mokombora ya kinuklia imesema kuwa zoezi hilo ni la uchokozi wa kijeshi. Vyombo vya habari vimesema kuwa Marekani...
Tanzania ni miongoni mwa mataifa chache duniani yaliyojaliwa kuwa na rasilimali na madini mengi. Na baada ya kugunduliwa kwa gesi asili huko Mtwara na dhahabu sasa watafiti kutoka Uingereza wamegundua hifadhi kubwa zaidi duniani ya gesi adimu zaidi ya Helium nchini Tanzania. Watafiti kutoka chuo kikuu cha Oxford na kile cha Durham kwa ushirikiano na wataalumu wa madini kutoka Norway wamegundua uwepo wa takriban futi bilioni 54 za gesi hiyo ya barafu kama inavyofahamika. Ugunduzi huo umefanyika katika eneo la...