Local News

RAIS MAGUFULI AWAAPISHA MAWAZIRI WAPYA WANNE NA NAIBU WAZIRI MMOJA
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Dokta John Pombe Magufuli amewaapisha mawaziri wapya wanne  na Naibu waziri mmoja aliowateua Tarehe 23 Desemba, mwaka huu.   Mawaziri hao wapya ni Waziri wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe, Waziri wa Maji na Umwagiliaji Mhandisi Gerson Lwenge,  Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi Dkt. Joyce Ndalichako na Naibu Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi Mheshimiwa Hamad Yusuf Masauni.   Rais Magufuli pia alifanya uhamisho wa Waziri mmoja ambaye ni...

Like
319
0
Monday, 28 December 2015
MAKAPU YA SIKUKU HAYABEBEKI YALIVYOSHEHENI MAZAGAZAGA
Entertanment

Kituo bora cha radio 2015 E-fm leo kimekabidhi zawadi ya makapu yaliyosheheni bidhaa za vyakula kuelekea sikukuu ya Christmas Zoezi hili liliwataka wasikilizaji wa E-fm kusikiliza mlio wa Jingle Bells uliokuwa ukizunguka kwenye vipindi tofauti kisha kutambua muda ambao mlio huo umesikika, jina la kipindi husika na mtangazaji/watangazaji wa zamu waliokuwa studio muda huo. Akizungumza mara baada ya kukabidhi makapu hayo kwa washindi Meneja wa vipindi E-fm Bwana Dickson Ponela (Big Dad Dizzo) ameeleza kuwa, E-fm imekuwa ikishirikisha wasikilizaji...

Like
566
0
Thursday, 24 December 2015
UPOTEVU WA VYETI NA NYARAKA NI CHANGAMOTO ZINAZOIKABILI SEKRETARIETI YA AJIRA NA UTUMISHI WA UMMA
Local News

SEKRETARIETI ya Ajira katika Utumishi wa Umma katika kutekeleza jukumu lake la uendeshaji wa mchakato wa ajira serikalini, imekuwa ikikumbana na changamoto mbalimbali ikiwemo ya matukio ya upotevu wa vyeti vya kitaaluma na nyaraka nyingine za msingi kutoka kwa waombaji kazi. Taarifa iliyotolewa na Kitengo cha Mawasiliano Serikalini, Ofisi ya Rais Sekretarieti ya Ajira katika Utumishi wa Umma, imeeleza kuwa waombaji kazi laki 256,928 wamekosa nafasi ya kuitwa kwenye usaili ili kuweza kuajiriwa Serikalini kutokana na sababu mbalimbali zikiwemo...

Like
433
0
Wednesday, 23 December 2015
KAIMU MKURUGENZI WA TAASISI YA SARATANI OCEAN ROAD ASIMAMISHWA KAZI
Local News

WAZIRI wa afya , maendeleo ya jamii jinsia, watoto na wazee mheshimiwa UMMY MWALIMU amemsimamisha kazi Kaimu Mkurugezi wa Taasisi ya Saratani ya Ocean Road, Dokta Diwani Msemo ili kupisha uchunguzi wa kubaini iwapo mgongano wa kimaslahi umeathiri utendaji wa taasisi hiyo chini ya uongozi wake. Taarifa iliyotolewa na Wizara ya afya leo, inaeleza kuwa dokta Msemo amesimamishwa kazi kutokana na sababu mbalimbali  kama vile kuwepo kwa manung’uniko mengi kutoka kwa wapokea huduma hususani katika taasisi ya saratani ya ocean...

Like
387
0
Wednesday, 23 December 2015
ASILIMIA 14.3% WAFAULU MITIHANI YA BODI YA TAIFA YA WAHASIBU NA WAKAGUZI WA HESABU
Local News

JUMLA ya watahiniwa 813 ambao ni sawa na asilimia 14.3 wamefaulu mitihani ya Bodi ya Taifa ya Wahasibu na Wakaguzi wa Hesabu Tanzania (NBAA)  uliofanyika Novemba 2015 kote nchini.   Katika matokeo hayo, wahitimu wengine elfu 1,867 ambao ni sawa na asilimia 32.9 wamefaulu baadhi ya masomo katika ngazi mbalimbali kati ya watahiniwa elfu 6,404 waliosajiliwa katika mitihani hiyo.   Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi NBAA Bwana. Pius Maneno katika kikao cha wakurugenzi wa bodi hiyo kilichokaa kuidhinisha...

Like
250
0
Wednesday, 23 December 2015
KADCO YAOKOA BILIONI MBILI KWA KUZUIA WIZI WA NYARA ZA SERIKALI
Local News

KAMPUNI ya maendeleo ya viwanja vya ndege –KADCO,  inayosimamia uwanja wa ndege wa kimataifa wa Kilimanjaro (KIA) imesema imeokoa zaidi ya kiasi cha shilingi  Bilioni  mbili katika kipindi cha wiki moja ikiwa ni thamani ya nyara za serikali na vito vya thamani vilivyokuwa vitoroshwe kupitia uwanja huo.   Menejimenti ya uwanja huo kupitia kitengo cha usalama ilifanikiwa kukamata vipande 264 vya madini ya Tanzanite vikiwa na uzito wa kilograamu 2.04 ambavyo thamani yake inakadiriwa kufikia Bilioni 2.5.   Kwa mujibu...

Like
209
0
Wednesday, 23 December 2015
WAHITIMU 27005 WACHAGULIWA KUJIUNGA KIDATO CHA KWANZA ARUSHA
Local News

JUMLA ya wanafunzi, 27005  ambao wamehitimu elimu ya msingi mwaka2015 mkoani Arusha wamechaguliwa kujiunga kidato cha kwanza mwaka 2016.   Akitangaza matokeo hayo Kaimu katibu tawala mkoa wa Arusha, Hamdouny Mansour, amesema jumla ya wanafunzi 33, 898 walifanya mtihani wa kuhitimu elimu ya msingi ambapo wavulana walikuwa ni 15, 868 na wasichana 18,030.   Mansour amesema waliofaulu wamepata  alama kati ya 100 hadi 250 ambapo wavulana ni12,563 na wasichana ni 14,442 na ufaulu huo ni sawa na asilimia 79.67 ikilinganishwa na mwaka...

Like
201
0
Tuesday, 22 December 2015
RAIS MAGUFULI ATOA ZAWADI KWA WATU WALIO KATIKA MAKUNDI MAALUM
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta John  Magufuli,  ametoa zawadi  ya vitu mbalimbali ikiwemo vyakula vyenye thamani   ya Shilingi  milioni  8  kwa watu walio katika makundi  maalum wakiwemo watoto wanaoishi katika  mazingira hatari. Akikabidhi msaada huo kwa niaba ya Rais, Kamishna wa Ustawi wa Jamii kutoka Wizara ya Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Rabikira  Mushi  amesema zawadi hizo zinalenga kuwasaidia makundi hayo kusherehekea sikukuu kwa furaha kama watu wengine. Amevitaja baadhi ya vituo hivyo...

Like
205
0
Tuesday, 22 December 2015
KUTANA NA WAPENZI WALIOFUNGA NDOA HOSPITALI
Local News

  Huko nchini Kenya Imetufikia ishu ya ndoa iliyofungwa hospitali huku bibi harusi akiwa amelazwa na kushindwa kutembea wala kukaa baada ya kupata ajali barabarani jumanne kabla ya harusi iliyosababisha kuvunjika kwa miguu yote miwili,kiuno na mkono wa kushoto ,mwanamke huyo alisindikizwa na waauguzi pamoja na wasimamizi kuelekea kwenye uwanja uliopo nje ya hospitali hiyo ulioandaliwa kwa ajiri ya sherehe huku machozi ya furaha yakimtililika baada ya kula kiapo cha ndoa na mume wake ambaye walipata ajari wote na kuumia...

Like
304
0
Tuesday, 22 December 2015
SERIKALI KUSHIRIKIANA NA WADAU KUTATUA KERO YA MAJI CHUNYA
Local News

SERIKALI WIlayani Chunya Mkoani Mbeya kwa kushirikiana na wadau wa maendeleo wameendelea na jitihada mbalimbali za kuhakikisha wanatatua changamoto ya ukosefu wa maji wilayani humo.   Hatua hiyo imekuja kufuataia kampuni ya Peak Resource inayojihusisha na utafiti wa madini adimu chini ya ardhi katika kata  ya ngwala wilayanii chunya mkoani mbeya kuchimba visima viwili vya maji vyenye thamani ya shilingi milioni 16.   Akizungumza wakati wa makabidhiano ya visima hivyo Mkuu wa Wilaya ya Chunya Elias Tarimo  amesema hatua ya...

Like
287
0
Tuesday, 22 December 2015
WAZIRI KAIRUKI AAGIZA WATUMISHI KUJENGEWA UWEZO
Local News

WAZIRI wa Nchi Ofisi ya Rais Utumishi na Utawala Bora mheshimiwa Angella Kairuki ameagiza kuzingatiwa kwa utaratibu wa kuwajengea uwezo watumishi ili waweze kumudu majukumu katika sehemu zao za kazi.   Waziri Kairuki ameyasema hayo wakati wa kikao kazi na Idara ya uendelezaji Rasilimali watu na kusisitiza kuwa waajiri wasitegemee serikali kuruhusu kuendelea kutoa mikataba kwa watumishi wakati mpango wa urithishanaji madaraka upo na watumishi wenye sifa stahiki wapo.   Mbali na hayo ameelekeza uchunguzi ufanyike kubaini watumishi...

Like
183
0
Tuesday, 22 December 2015