Slider

DK. SHEIN: TOFAUTI ZA KISIASA ZISIVURUGE AMANI
Local News

RAIS wa  Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Dokta  Ali Mohamed Shein  ametaka tofauti za kisiasa zilizopo Visiwani humo zisitumike kuvuruga amani na utulivu ambayo ndiyo siri kubwa ya maendeleo yaliyopatikana katika visiwa vya Unguja na Pemba.   Dokta Shein ambaye alikuwa akizungumza na wananchi wa Wete waliokwenda kumsalimia mara baada ya kukagua ujenzi wa soko na Ofisi ya Baraza la Mji wa Wete, amesema kuwa suala la amani halina mbadala huku akiahidi kuendelea kuisimamia amani ya Zanzibar na...

Like
140
0
Thursday, 07 January 2016
IVORY COAST: OUATTARA AKUBALI KUJIUZULU KWA WAZIRI MKUU
Global News

RAIS Alassane Ouattara wa Ivory Coast amekubali kujiuzulu kwa Waziri Mkuu na Serikali yake.   Akituma ujumbe kupitia mtandao wa Twitter, Outtarra amesema waziri mkuu aliwasilisha hati ya kujiuzulu na ile ya serikali naye akairidhia.   Ouattara, mwanauchumi mwenye umri wa miaka 74, aliyewahi kulitumikia shirika la fedha la kimataifa na  amechaguliwa kwa muhula wa pili wa miaka mitano kama rais, mwezi Oktoba mwaka...

Like
732
0
Thursday, 07 January 2016
UN YAANZA MIKAKATI KUIWEKEA VIKWAZO KOREA KASKAZINI
Global News

SIKU moja baada ya Korea Kaskazini kufanya jaribio la bomu la haidrojeni, Baraza la Usalama la Umoja wa Mataifa limekubaliana kuanza mikakati ya kuiwekea vikwazo. Hata hivyo baadhi ya Wataalamu wameonyesha kuwa na wasi wasi kuhusu jaribio la sasa la nyuklia la Korea Kaskazini ambalo ni la nne katika mwongo mmoja, wakisema huenda lisiwe la haidrojeni kutokana na mlipuko uliotokea. Bomu la hydrojeni ni moja ya mabomu hatari ya jamii ya atomiki au nyuklia yenye nguvu zaidi. Wataalam wanasema bomu...

Like
179
0
Thursday, 07 January 2016
BODI YA UTALII IMETAKIWA KUTUMIA VYOMBO VYA HABARI VYA KIMATAIFA KUITANGZA TANZANIA
Local News

WAZIRI wa Maliasili na Utalii Profesa Jumanne Maghembe ameitaka Bodi ya Utalii Tanzania- TTB, kuendelea kutumia vyombo vya habari vya Kimataifa kama vile CNN na BBC  kuitangaza Tanzania kama eneo la Utalii duniani sambasamba na kuweka makala na matangazo ya utalii katika majarida ya Kimataifa yanayoandika habari za Utalii na usafiri (Travel Magazine) ambayo ndiyo husomwa na watalii wengi duniani. Waziri Maghembe amesema hatua hiyo itasaidia kuongeza idadi ya watalii nchini.   Waziri Maghembe ameyasema hayo alipotembelea Bodi ya Utalii...

Like
194
0
Thursday, 07 January 2016
IRINGA: VIONGOZI WA VYAMA VYA USHIRIKA VYA ZAO LA TUMBAKU WASIMAMISHWA
Local News

WAZIRI wa kilimo,mifugo na uvuvi mheshimiwa Mwigulu Nchemba amewasimamisha viongozi wa vyama vya ushirika vya zao la tumbaku mkoani Iringa. Akizungumza kwenye mkutano uliofanyika katika ukumbi wa siasa na kilimo, Mheshimiwa Mwigulu amemuagiza mrajisi wa mkoa kuivunja bodi hiyo na kuwachunguza viongozi wa vyama hivyo. Aidha, ameiomba serikali ya mkoa kufuatilia na kutathimini ubadhirifu uliofanywa na viongozi hao na kuwachukulia hatua ili kukomesha vitendo...

Like
365
0
Thursday, 07 January 2016
NIGERIA: MHUBIRI WA KIISLAM AHUKUMIWA KIFO
Global News

MAHAKAMA moja ya Kiislamu nchini Nigeria imemhukumu kifo mhubiri anayetuhumiwa kukufuru kwa kumtukana Mtume  Muhammad.   Abdul Inyass amehukumiwa katika kikao cha faragha cha mahakama katika mji wa Kano, kaskazini mwa Nigeria.   Afisa wa mashtaka Lamido Abba Soron-Dinki ameliambia shirika la AFP kuwa Kikao hicho kimefanyika faraghani kuzuia “fujo kutoka kwa umma” sawa na ilivyoshuhudiwa wakati wa kikao cha...

Like
193
0
Wednesday, 06 January 2016
KOREA KASKAZINI YATHIBITISHA KUFANYA JARIBIO LA BOMU LA HAIDROJENI
Global News

KOREA KASKAZINI imesema kwa mara ya kwanza imefanikiwa kufanya majaribio ya bomu la nguvu ya maji, maarufu kama bomu la haidrojeni.   Tangazo hili limetolewa na runinga ya taifa baada ya kusikika mitetemeko ya ardhi ya kipimo cha tano nukta moja, karibu na eneo kuliko na kinu cha nyukilia.   Wataalamu wa Marekani wanafanya uchunguzi ikiwa yalikua majaribio ya bomu hilo au ilikua zana nyingine ya nyuklia isiyokuwa na nguvu....

Like
298
0
Wednesday, 06 January 2016
TRA YAKUSANYA TRILIONI 1.4 KATIKA KIPINDI CHA MWEZI DESEMBA 2015
Local News

JUMLA ya shilingi trilioni 1.4 zimekusanywa na Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) katika kipindi cha mwezi Desemba mwaka uliopita wa 2015.   Kiasi hicho ni sawa na ongezeko la wastani wa shilingi  bilioni 490 kwa mwezi ikilinganishwa na wastani wa makusanyo ya kuanzia Julai hadi Novemba ambapo ,TRA ilikuwa imekusanya wastani wa shilingi bilioni 900 kwa mwezi.   Takwimu hizo zimetolewa leo jijini Dar es salaam na Kaimu Kamishna Mamlaka ya Mapato  Tanzania (TRA) Alphayo Kidata wakati wa mkutano na...

Like
203
0
Wednesday, 06 January 2016
RAIS MAGUFULI ATUMA SALAMU ZA RAMBIRAMBI KUFUATIA KIFO CHA INSPECTA GERALD RYOBA
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dokta. John Pombe Magufuli amemtumia salamu za rambirambi Mkuu wa Jeshi la Polisi hapa Nchini IGP Ernest Mangu kufuatia kifo cha msaidizi wake Inspekta – Gerald Ryoba aliyepoteza maisha katika ajali ya kusombwa na mafuriko ya maji wakati akikatiza katika eneo la Kibaigwa, Wilaya ya Kongwa Mkoani Dodoma.   Katika ajali hiyo iliyotokea Januari 3 mwaka huu, Inspekta Ryoba akiwa na Mkewe na watoto wake wawili, pamoja na watu wengine wawili walikuwa wakisafiri...

Like
299
0
Wednesday, 06 January 2016
MAREKANI YAWEKA MIKAKATI YA KUDHIBITI SILAHA
Global News

RAIS wa Marekani Barack Obama ametangaza hatua kadhaa zinazonuwiwa kukabiliana na matumizi mabaya ya silaha nchini humo, zikiwemo upatikanaji wa lazima wa leseni kwa wauzaji silaha na kufanya ukaguzi wa historia za wateja.   Obama ametangaza hatua hizo katika ikulu ya White House akiwa amezungukwa na manusura wa mashambulizi ya silaha yanayouwa karibu Wamarekani 30,000 kila mwaka.   Hata hivyo Obama amekiri kuwa hatua hizo alizozipitisha mwenyewe bila kulishirikisha bunge la Congress, hazitomaliza kabisa tatizo la matumizi mabaya ya...

Like
127
0
Wednesday, 06 January 2016
MZOZO WA RIYADH NA TEHRAN WATAJWA KUTOATHIRI MAZUNGUMZO YA AMANI SYRIA
Global News

WAZIRI wa Mambo ya nje wa Saudi Arabia amesema kuwa mzozo unaozidi kufukuta kati ya Riyadh na Tehran hautaathiri mazungumzo ya amani ya Syria.   Taarifa yake ilikuja wakati Kuwait nayo ikimrudisha balozi wake kutoka Iran, kuiunga mkono Saudi Arabia.   Saudi Arabia pamoja na mataifa mengine kadhaa ya Kiarabu, yamechukuwa hatua dhidi ya Iran, baada ya ubalozi wake kushambuliwa na kuchomwa moto na waandamanaji waliokuwa wanapinga kuuawa kwa kiongozi wa Kishia na mkosoaji wa serikali ya Saudi Sheikh Nimr...

Like
137
0
Wednesday, 06 January 2016