Slider

MIKAKATI YA DIWANI MANJI 2016  KWA WAKAZI WA KATA YA MBAGALA KUU
Local News

DIWANI WA KATA YA MBAGALA KUU YUSUPH MANJI DECEMBER 31 2015 AMEITUMIA KUWASHUKURU WANANCHI NA WAPIGA KURA WA KATA YA MBAGALA KUU KWA USHINDI ALIOUPATA MANJI AMBAYE KWENYE MIPANGO YAKE YA MWAKA 2016 ILIYOANZA  LEO JANUARY 01  AMESEMA ATABANDIKA NA KUSAMBAZA RATIBAYAKE  YA KUTEMBELEA KILA MTAA MARA MOJA KWA MWEZI ILI KUFUATILIA  UTENDAJI WA AHADI ZAKE NA KUTOA NAFASI KWA  KILA MWANANCHI WA KATA YAKE AWEZE KUONGEA NAE ANA KWA ANA NA  KUWAELEZA KILA JAMBO KUBWA LA MAENDELEO LITAKALOKUWA LINAJITOKEZA....

Like
532
0
Friday, 01 January 2016
SHULE 6 ZA SEKONDARI KUJENGWA KINONDONI
Local News

KUFUATIA Manispaa ya  kinondoni kukabiliwa na tatizo la upumgufu wa shule za sekondari lililosababishwa na ongezeko kubwa la wanafunzi  wanao faulu, Manispaa hiyo kwa kushirikiana na wadau mbalimbali wa elimu imepanga kujenga shule sita ili kusaidia kupunguza sehemu ya tatizo hilo. Mkuu wa wilaya ya kinondoni PAUL MAKONDA amesema ni aibu kubwa kwa manispaa kubwa kama ya hiyo kuwa na upungufu wa shule za sekondari kutokana na manispaa hiyo kuwa na wadau wengi wenye uwezo wa kusaidia kuondoa tatizo hilo....

Like
300
0
Thursday, 31 December 2015
WANANCHI WATAHADHIRISHWA KUTOFANYA FUJO WAKATI WA MKESHA WA MWAKA MPYA
Local News

JESHI la Polisi Kanda maalum ya Dar es salaam limewatahadharisha wananchi kutokufanya fujo wakati wa  mkesha wa mwaka mpya kwa kuweka mikakati mikali kwa watakaokaidi amri hiyo.   Kamishna wa Polisi Kanda Maalum ya Dar es salaam Suleiman Kova amepiga marufuku uchomaji wa matairi ya gari,  upigaji baruti, risasi za moto na fataki ambazo zinaweza kusababisha madhara wakati wa mkesha wa mwaka mpya....

Like
278
0
Thursday, 31 December 2015
RAIS MAGUFULI KUONGOZA WATANZANIA KULIOMBEA AMANI TAIFA LEO
Local News

RAIS wa Jamuhuri ya Muungano wa Tanzania dokta JOHN POMBE MAGUFULI leo anatarajiwa kuwa mgeni rasmi katika Mkesha wa kuiombea amani Tanzania utakaofanyika katika uwanja wa Taifa Jijini Dar es salaam. Mwenyekiti wa Jumuiya ya Makanisa ya Pentekoste nchini -TFC GODFREY MALASSY amesema kuwa mkesha huo utakuwa kwa ajili ya kumshukuru Mungu kwa kuijalia Tanzania kumaliza Uchaguzi Mkuu uliofanyika mwezi oktoba mwaka huu kwa Amani na utulivu, pamoja na Dua maalum ya kumuombea Rais. Aidha ameeleza kuwa katika tamasha hilo...

Like
270
0
Thursday, 31 December 2015
EL NINO KUATHIRI MAMILIONI YA WATU 2016
Global News

MASHIRIKA ya misaada yamesema kuwa hali ya hewa ya El Nino ambayo imekuwa ndiyo kali zaidi katika historia itazidisha hatari ya njaa na maradhi kwa mamilioni ya watu duniani 2016.   Hali hii ya hewa inatarajiwa kusababisha ukame baadhi ya maeneo na mafuriko kwingine, ambapo baadhi ya maeneo yanayotarajiwa kuathirika sana yako Afrika, huku uhaba wa chakula ukitarajiwa kufikia kilele mwezi Februari.   Hali ya hewa ya El Nino, hutokana na kuongezeka kwa joto na huathiri hali ya hewa maeneo...

Like
165
0
Wednesday, 30 December 2015
AU YATISHIA MAKUNDI HASIMU BURUNDI
Global News

UMOJA  wa  Afrika  leo  umetishia  kuyawekea vikwazo makundi  hasimu  nchini  Burundi  iwapo  yatashindwa kuhudhuria  mazungumzo  ya  amani  mwezi  ujao, wakati ukiibana  serikali   kukubali jeshi  la  kulinda  amani. Serikali  ya  Burundi  na  upinzani, pande  zilizokutana nchini  Uganda  siku  ya  Jumatatu,  zinatarajiwa  kukutana tena  Januari  Mjini Arusha kwa  mazungumzo  yenye  lengo  la  kumaliza miezi  kadhaa  ya ...

Like
183
0
Wednesday, 30 December 2015
BARAZA LA TAIFA LA UJENZI LAPOKEA MIGOGORO 41 NA KUIPATIA UFUMBUZI 2015
Local News

BARAZA la Taifa la Ujenzi limepokea migogoro 41 na kufanikiwa kuitafutia ufumbuzi katika kipindi cha mwaka 2015 kwa kushirikiana na wadau wa sekta ya Ujenzi nchini.   Hayo yamesemwa leo na Mtendaji Mkuu wa Baraza hilo,  Mhandisi Dokta Leonard Chamuriho  wakati wa mkutano na waandishi wa habari Jijini Dar es salaam.   Akizungumzia majukumu ya Baraza hilo katika kutatua Migogoro inayojitokeza katika Sekta hiyo, Mhandisi Chamuriho amebainisha kuwa migogogoro iliyojitokeza imekuwa ikitegemea Ukubwa wa mradi, Hali ya eneo la mradi,...

Like
180
0
Wednesday, 30 December 2015
KESI YA WAFANYAKAZI TRA KUSIKILIZWA JANUARY 2016
Local News

KESI inayowakabili wafanyakazi wa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) inatarajiwa kusikilizwa  tena January 13, mwaka  2016   Akizungumza katika Mahakama ya Hakimu Mkazi Kisutu jijini dar es salaam Wakili wa Serikali Bi.Dianna Lukondo amesema kuwa kwa leo Kesi ilikuja kwa ajili ya kusikilizwa na kutoa dhamana kwa washtakiwa na hivyo imeshindikana kusikilizwa kutokana na upelelezi kutokamilika.   Washtakiwa hao wanatuhumiwa kwa kosa la uhujumu uchumi, wakidaiwa kuhusika na upotevu wa makontena 329 katika Bandari ya Dar es Salaam...

Like
174
0
Wednesday, 30 December 2015
UCHAGUZI WAANZA AFRIKA YA KATI
Global News

WANANCHI wa  Jamuhuri ya Afrika ya kati hii leo wanashiriki katika zoezi la uchaguzi wa Rais na wabunge  nchini humo.   Uchaguzi huo uliokuwa ufanyike tarehe 27 mwezi huu ulisogezwa mbele na tume ya uchaguzi nchini humo hadi  tarehe ya leo Desemba 30 kutokana na kasoro zilizojitokeza wakati wa kipindi cha maandalizi ya uchaguzi huo.   Msemaji wa Tume ya uchaguzi nchini humo Julius Rufin Ngoadebaba ameahidi kuwa uchaguzi huo utakwenda vizuri katika maeneo yote nchini humo  ambako Zaidi ya...

Like
177
0
Wednesday, 30 December 2015
MAREKANI YAFANYA MASHAMBULIZI YA ANGA DHIDI YA IS
Global News

MASHAMBULIZI ya angani yanayoongozwa na Marekani yamefanikisha kuwaua viongozi kumi wa kundi la itikadi kali la  Dola la Kiisilamu katika kipindi cha mwezi uliopita wakiwemo wanaodaiwa kuhusika  na shambulizi la mjini Paris au mashambulizi mengine ambayo yalipangwa kufanyika barani ulaya .   Afisa  mmoja  wa jeshi la Marekani nchini Iraq  Kanali Steve  Warren amesema wanamgambo hao waliuawa wakati wa mashambulizi ya anga yaliyofanywa nchini Iraq na Syria.   Kwa mujibu wa Warren mmoja wa walioua katika mashambulizi hayo ni...

Like
211
0
Wednesday, 30 December 2015
KAMPUNI ILIYOPEWA TENDA YA KUKUSANYA UCHAFU UPANGA MAGHARIBI KUVUNJIWA MKATABA
Local News

KUFUATIA kukithiri kwa uchafu katika kata ya Upanga Magharibi licha ya kuwepo kwa kampuni ya TIRIMA iliyochukuwa tenda ya kufanya usafi katika kata hiyo,  Uongozi  umekusudia kuvunja mkataba na kampuni hiyo.   Diwani wa kata ya Upanga Magharibi Adinani Kitwana Kondo amesema eneo lililopo hospitali ya Muhimbili limekithiri kwa uchafu kitendo ambacho kinahatarisha maisha ya watu wengi wanaoishi na wanaotembelea maeneo hayo.   Kondo  amesema  kampuni hiyo  ya TIRIMA imekuwa ikikusanya shilingi elfu kumi na tano kwa kila mkazi wa...

Like
389
0
Wednesday, 30 December 2015