WATANZANIA HATARINI KUFA ZAIDI KWA MALARIA
Slider

Dar es Salaam. Taasisi ya Taifa ya Utafiti wa Magonjwa ya Binadamu (Nimr), imesema kutokana na mbu wa malaria kujenga usugu wa dawa yaPyrethroids  kwa baadhi ya maeneo nchini, ugonjwa huo sasa umeanza kurudi kwa kasi hasa sehemu zilizofanyiwa utafiti na kugawa vyandarua. Akizungumza katika kongamano la 30 la Kimataifa la Wanasayansi Watafiti jijini Dar es Salaam jana, Mtafiti katika Mradi wa Amani Medical uliopo chini ya Nimr, Said Magogo alisema kufuatia tatizo hilo kituo hicho kipo kwenye  mchakato wa...

Like
221
0
Monday, 17 October 2016
MOURINHO KUCHUNGUZWA NA FA
Slider

Matamshi ya Jose Mourinho kuhusu uteuzi wa mwamuzi anaeshabikia Manchester United Anthony Taylor kwa mchezo wa ligi kuu England kati ya Manchester United dhidi ya Liverpool utakaochezwa leo jumatatu yatachunguzwa na Shirikisho la Mpira wa miguu nchini humo FA. Mourinho amesema itakuwa vigumu kwa mwamuzi huyo kuchezesha vizuri baada ya uteuzi wake kukosolewa. ‘Mtu mmoja akiwa na lengo anaweka shinikizo kwake’ alisema Mourinho Kwa kawaida makocha hawatakiwi kuzungumza lolote kuhusiana na mwamuzi kabla ya mchezo. FA inataka kuchunguza...

Like
170
0
Monday, 17 October 2016
MASWALI KABLA YA KUMUONA DAKTARI YAWAKERA WAGONJWA
Slider

Wapokezi wa wagonjwa hospitalini wanao wahoji wagonjwa kuhusu ni kwanini wanahitaji kumuona daktari huenda yanawasababisha baadhi kutowatembelea madaktari wao , utaifiti umedhihirisha. Karibu watu wazima 2000 waliohojiwa na taasisi ya utafiti wa Saratani Uingereza, 4 kati ya 10 wamesema hawapendi kujadili magonjwa yao na maafisa wa ofisi ili kupata nafasi ya kumuona daktari. Wengi walikuwa na wasiwasi ya kupanda hamaki. Wataalamu wanasema ni lazima wagonjwa wasisitize kumuona daktari na wasikubali kuambiwa haiwezekani, iwapo wanakabiliwa na...

Like
297
0
Tuesday, 11 October 2016
BENTEKE AFUNGA BAO LA KASI ZAIDI
Slider

Mshambuliaji wa Ubelgiji Christian Benteke alifunga bao la kasi zaidi katika mechi za kufuzu kwa Kombe la Dunia, baada ya kufunga bao sekunde 8.1 dhidi ya Gibraltar. Mchezaji huyo wa Crystal Palace alifunga mabao matatu wakati wa mechi hiyo ya Kundi H ambayo Ubelgiji walishinda 6-0. Wafungaji wengine walikuwa Eden Hazard, Axel Witsel na Dries Mertens. Bao hilo la kwanza la Benteke pia ndilo la kasi zaidi kuwahi kufungwa na mchezaji wa Ubelgiji. Benteke alivunja rekodi ya awali ya bao...

Like
230
0
Tuesday, 11 October 2016
SAMSUNG “YASITISHA UTENGENEZAJI WA GALAXY NOTE 7”
Slider

Kampuni kubwa ya kutengeza simu aina ya smartphone Samsung,imeroptiwa kusitisha utengezaji wa simu aina ya Galaxy Note 7 kufuatia madai kwamba simu mpya zilizotengezwa kuchyukua mahala pa zile zilizo na matatizo ya betri pia zina matatizo. Vyombo vya habari vya Reuters na kile cha Yonhap kutoka Korea kusini vimewanukuu baadhi ya maafisa ambao hawakutajwa majina wakisema kuwa kampuni hiyo imesitisha kwa muda utengezaji wa simu hizo. Samsung imeambia BBC inaimarisha utengezaji wa simu hizo ili kuhakikisha ubora na usalama wake....

Like
303
0
Monday, 10 October 2016
CHINA YASHINDA TUZO YA KUTAMBUA MVINYO DUNIANI
Slider

Kundi moja la wataalam nchini China limeshinda tuzo la shindano la kuonja mvinyo nchini Ufaransa. Watalaam hao walitambua mivinyo waliopewa huku wakiwa wamefunikwa uso,wakibainisha asili, aina ya zabibu zilizotumika na mwaka mivinyo hiyo iliotengezwa. Waandalizi wa shindano hilo waliwataja wataalam hao wa China kuwa mabingwa katika ulimwengu wa mvinyo. Waliyashinda mataifa mengine 20,ikiwemo washindi wa awali Ubelgiji na Uhispania. Huku mapato yakiongezeka nchini China,taifa hilo linaongoza katika utengezaji na utumiaji wa mvinyo...

Like
308
0
Monday, 10 October 2016
SAMSUNG NOTE 7 YASHIKA MOTO KWENYE NDEGE
Slider

Simu ya kampuni ya Samsung aina ya Galaxy Note 7, ambayo ilikuwa imethibitishwa na kampuni hiyo kuwa ilikuwa salama, imeshika moto kwenye ndege nchini Marekani. Simu hiyo inadaiwa kushika moto ikiwa na abiria aliyekuwa kwenye shirika la ndege la Southwest Airlines. Shirika hilo limesema abiria waliokuwa kwenye ndege moja yake, iliyokuwa imepangiwa kusafiri kutoka Louisville, Kentucky, hadi Baltimore, Maryland, waliondolewa kwenye ndege kwa dharura kabla ya ndege hiyo kupaa Jumatano. Kampuni ya Samsung iliwashauri watu waliokuwa wamenunua simu...

Like
197
0
Thursday, 06 October 2016
ASWEKWA LUPANGO KWA KUMNYONGA MKEWE
Slider

Mkazi wa Kijiji cha Igate, Kata ya Nzera wilayani Geita anashikiliwa na polisi kwa tuhuma za kumnyonga mkewe Dotto Frederick (25) baada ya kuibuka ugomvi kati yao. Kamanda wa Polisi Mkoa wa Geita, Mponjoli Mwabulambo amesema kuwa mauaji hayo yalitokea nyumbani kwa mtuhumiwa.   Amesema mtuhumiwa huyo alikamatwa Oktoba Mosi eneo la Machimboni Kijiji cha Muranda Kata ya Buseresere wilayani hapa baada ya kuishi mafichoni kwa siku 15. Kamanda Mwabulambo amesema mtuhumiwa huyo alimnyonga mkewe kwa kutumia kipande cha nguo...

Like
172
0
Thursday, 06 October 2016
YANGA YATOA MUHTASARI WA MKATABA
Slider

1.    Bodi ya Wadhamini wa Young Africans Sports Club, (ambayo hapa inajulikana kama Mmiliki”) imeingia tarehe 3 September, 2016 Mkataba wa kukodishwa na kampuni ijulikanayo Yanga Yetu Limited (inayojulikana hapa kama “Mkodishwaji” kwa muhtasari wa maazimio yaliyoafikiwa katika Mkutano Mkuu wa Young Africans Sports Club uliofanyika tarehe 6 Agosti, 2016 ulitambua kuwa Young Africans Sports Club (anayejulikana hapa kama “YANGA”): 1.1    KWA KUWA, Timu ya Soka ya Mmiliki ni kongwe na yenye mafanikio kuliko timu ya soka nyingine...

Like
238
0
Thursday, 06 October 2016
BODI YA WADHAMINI CUF KUMFUNGULIA KESI LIPUMBA NA MSAJILI
Slider

Bodi ya wadhamini CUF imefungua maombi ya kufungua kesi katika Mahakama Kuu dhidi ya Msajili wa Vyama vya Siasa,Jaji Francis Mutungi, Prof Ibrahim Lipumba na wanachama 12 waliosimamishwa uanachama wa chama hicho. Katika maombi hayo bodi hiyo inaomba kibali cha kufungua kesi dhidi ya Msajili, Lipumba na wenzake, ili mahakama itoe amri ya kumzuia Msajili asifanye kazi nje ya mipaka ya mamlaka yake kisheria. Jana wajumbe wanne wa bodi hiyo waliibuka na kuunga mkono msimamo wa msajili wa vyama vya...

Like
177
0
Wednesday, 05 October 2016
TYSON FURY AKIRI KUTUMIA COCAINE
Slider

Bingwa wa ndondi katika uzani mzito duniani Tyson Fury amesema amekuwa akitumia Cocaine ili kumsaidia kukubiliana na matatizo ya kiakili. Bondia huyo wa Uingereza amesema kuwa amekuwa akiugua ugonjwa wa kiakili kwa miaka kadhaa na hajafanya mazoezi tangu mwezi Mei. Nimekuwa nje nikilewa ,Jumatatu hadi Ijumaa hadi Jumapili na kutumia Cocaine,Fury aliambia jarida la Rolling Stones. Hatua hiyo inajiri siku mbili baada ya Fury kudai katika mitandao ya kijamii kwamba amejiuzulu,kabla kukana madai hayo saa tatu baadaye akisema alikuwa akifanya...

Like
145
0
Wednesday, 05 October 2016
« Previous PageNext Page »