Mkali wa Nigeria, Ludemilade Martin Alejo maarufu kama YCEE, anatarajiwa kutua bongo, Jumapili hii. Mkali huyu anatarajiwa kuja Tanzania kwa dhumuni la kuutangaza zaidi muziki wake akiwa na ngoma kama Omo Alhaji, Jagabana’ na nyinginezo. Ziara hiyo itaambatana na mkutano wa waandishi wa habari siku ya Jumatatu, ikifuatiwa na ziara ya kutembelea vituo mbalimbali vya habari kuanzia Agosti 29 mpaka tarehe Septemba 1. Pamoja na hayo amesema kuwa, anayo shauku kubwa juu ya ziara yake kwani hii ni mara yake...
Wanariadha wa Kenya wamekuwa wakiishi kwenye makazi ambayo hayawafurahishi timu hiyo baada ya kumalizika kwa Michezo ya Olimpiki mjini Rio, mmoja wa wanariadha hao amelalamika. Mkimbiaji wa mbio za Marathon, Wesley Korir, ambaye pia ni mbunge, amepakia picha za hoteli anayosema ni duni kwenye mitandao ya Twitter na Facebook akilalamika. “Timu iliyoongoza Afrika na timu ya pili dunia nzima katika riadha, na hivi ndivyo tunavyotunzwa ,” ameandika. Amelinganisha mazingira ya eneo wanamoishi na mtaa wa mabanda. Wanariadha hao...
PICHA: Amiri Jeshi Mkuu Rais Dkt.John Pombe magufuli akimsikiliza Mkurugenzi Mkuu wa Idara ya Usalama wa Taifa Dkt Modestus Francis Kapilimba akila kiapo cha maadili ya viongozi wa Umma Ikulu jijini Dar es salaam leo Agosti 24,...
Polisi nchini Burundi wamewatia nguvuni wajumbe wanane wa mtandao wa kijamii wa WhatApp . Kulingana na msemaji wa wizara ya usalama wa umma nchini humo Pierre Nkurikiye watu hao ambao ni wakazi wa mji mkuu Bujumbura walikamatwa mnamo tarehe 20 Agosti kutokana na “vitendo vya uhalifu wa kimtandao “. Wanane hao kwa pamoja walikuwa ni wajumbe wa kundi moja la WhatsApp. Kwa mujibu wa Nkurikiye WhatsApp mijadala inayoendelea katika makundi ya WhatsApp inaeneza taarifa za “matusi ni chanzo cha ghasia...
Muogeleaji wa Marekani Ryan Lochte amepoteza mikataba yake yote minne ya udhamini baada ya wenzake watatu kudanganya kuwa waliibiwa na wezi waliokuwa na silaha katika michuano ya Olimpiki iliyofanyika mjini Rio. Kampuni ya uogeleaji ya Speedo ilikuwa ya kwanza kusitisha mkataba wake ikifuatiwa na Luxury retailer, Ralph Lauren, The Skin Care company,na Kampuni ya matress na Airweave. Lochte bado anakabiliwa na mashitaka ya kujibu kwa mamlaka ya michezo nchini Brazil ikiwa ni uhalifu pamoja na utovu wa...
Baada ya sekeseke la aliyekuwa Katibu wa Baraza la Wazee la Yanga Mzee Yahya Akilimali na wapenzi na mashabiki wa klabu hiyo. Limechukua sura mpya baada ya kuibiwa kofia yake alipokuwa ameketi maeneo yanayosemekana kulikuwa na vijana waliokuwa wakimfuatilia. Mzee Akilimali ameeleza kuwa, walishamaliza tofauti zao na mashabiki wa kbabu hiyo waliokuwa wakimfuatilia na kinachofanyika sasa ni uhuni tu wa vijana wa mtaani aliodai ni watumiaji wa dawa za kulevya....
Serikali ya Sudan Kusini imewaajiri watoto wavulana kama wanajeshi wakati huu inapojiandaa kwa mzozo mpya, kwa mujibu wa shirika la Associated Press. Mwanasiasa mmoja mwenye ushawishi anaripotiwa kuongoza shughuli ya kuwaajiri watoto hao, wengine wakitajwa kuwa na umri wa hadi miaka 12 kutoka kijiji kimoja nchini humo. Nyaraka zinaonyesha kuwa shughuli ya kuwaajiri watoto hao, ilifanyika muda mfupi baada ya baraza la usalama la umoja wa mataifa kuidhinisha azimio wiki moja iliyopita la kutuma wanajeshi 4000 kwenda Sudan Kusini, kuwalinda...
WALIMU wakuu wa shule 68 wa shule za Msingi wanatakiwa kuvuliwa na kunyang’anywa vyeo vyao kwa kosa la udananyifu wa takwimu za wanafunzi hewa tangu elimu itangazwe kuwa bure. Hayo yamesemwa na Mkuu wa Wilaya ya Kinondoni, Ally Salum Hapi wakati akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo. Amesema kuwa walimu wakuu hao wametakiwa kuvuliwa vyeo vyao na kuwapa walimu wengine kwa kosa la kutoa takwimu za wanafunzi hewa 3462 wa shule za msingi 68 za Wilaya...
Mwana wa mlanguzi mkuu wa mihadarati nchini Mexico Joaquin El Chapo Guzman ni miongoni mwa washukiwa wa uhalifu waliotekwa nyara katika mji uliopo pwani ya Pacific siku ya Jumatatu kulingana na maafisa. Wanasema kuwa Jesus Alfredo Guzman mwenye umri wa miaka 29 ni miongoni mwa wanachama sita wa genge la Sinaloa waliotekwa nyara na genge pinzani ,kwa jina Jalisco New Generation. Kisa hicho kilitokea katika mkahawa uliopo mji wa kitalii wa Puerto Vallarta. Chapo Guzman ambaye anahudumia kifungo ,aliliongoza genge...
Makao makuu ya kijeshi ya Marekani, The Pentagon, yametangaza kuwa watu 15 waliokuwa wakizuiliwa katika gereza maalumu la Guantanamo Bay, nchini Cuba wamehamishiwa hadi Emarati. Ni kundi kubwa zaidi kuwahi kuhamishwa kutoka gereza hilo chini ya utawala wa Rais Barack Obama. Kumi na mbili kati yao wanatoka Yemen na watatu Afghanistan. Wanachama wakuu wa chama cha Republican wamekosoa hatua hiyo. Hatua hiyo inapunguza wafungwa hadi 61 wanaozuiliwa katika kituo hicho cha Marekani. Mara kwa mara Bwana Obama ameeleza masikitiko yake...
Mwanariadha raia wa Kenya amedhihirisha umwamba wake baada ya kushinda mbio za mita 800 huko Rio De Jeneiro nchini Brazil usiku wa kuamkia leo. Mwanariadha huyo mwenye miaka 27 ameonyesha uzoefu wake katika mbio ambapo baada ya kuwa nyuma alianza kuwapita wenzake katika mzunguko wa mwisho na hata Mkenya mwenzake Alfred Kipketer na kukamilisha mbio hizo kwa dakika moja na sekunde 42.15 Naye Malgeria Taoufik Makhloufi alishika nafasi ya pili na kujinyakulia medali ya dhahabu kwa kikimbia kwa dakika moja...