MUUNGANO wa vyama vya upinzani nchini Kenya-CORD, umetangaza kuendelea na maandamano ya upinzani leo Jumatatu, kama ilivyopangwa ikiwa ni sehemu ya kampeni ya kutaka kutupiliwa mbali kwa tume ya uchaguzi nchini humo, IEBC, kabla ya uchaguzi mkuu wa mwaka ujao. Maandamano kama hayo yaliyofanyika Juma liliopita, yaliambatana na ghasia ambapo polisi walishutumiwa kwa vitendo vya...
WAJASIRIAMALI Wadogo Jijini Tanga wameiomba wakala wa afya na usalama pahala pa kazi (OSHA) kutoa semina ya mafuzo kila mara hapa Nchini. Wakizungumza na EFM RADIO baada ya kumalizika semina hiyo jana atika ukumbi wa mkuu wa mkoa, baadhi ya wajasiriamali hao wameishukuru OSHA kwa kutoa mafunzo hayo ambayo yatasaidia kwa kiasi kikubwa kuweza kujikinga na madhara yanayoweza kuzuilika atika jamii. Kwa upande wake AKWILINA KATUMBA ambaye ni mtendaji mkuu wa wakala wa afya na usalama pahala pa kazi, amesema kuwa madhumuni makubwa...
ALIYEKUWA Naibu Waziri wa Kazi, Ajira na Maendeleo ya Vijana,katika serikali ya awamu ya nne, Dokta Makongoro Mahanga, amesema amesikitishwa na uvumi wa taarifa kuwa amefariki dunia. Akizungumza kwa njia ya simu na Efm Habari, Dokta Mahanga amesema hata yeye hajui ni nani ametoa taarifa hizo ambazo siyo za kweli na amewaomba watanzania kuitumia vyema mitandao badala ya kuibuka na taarifa ambazo hazina...
ZAIDI ya wajumbe 5,000 kutoka nchi 150 wamewasili mjini Copenhagen, Denmark kuhudhuria mkutano wa wiki nzima kuhusu masuala ya wanawake. Mkutano huo unoatajwa kuwa mkubwa zaidi kuwahi kuandaliwa katika kipindi cha muongo mmoja kujadili masuala ya wanawake kama afya, haki na maslahi ya wanawake na wasichana umeandaliwa na shirika la kimataifa la kutetea maslahi ya wanawake la Wellbeing. Mkutano huo unaanza leo hadi Alhamisi wiki hii na Miongoni mwa ajenda za mkutano huo ni kuhusu jinsi ya kupunguza vifo vya...
NCHI zenye nguvu duniani zinakutana mjini Vienna, Austria leo kujadili kupanuka kwa shughhuli za kundi la wanamgambo wenye itikadi kali la Dola la Kiislamu IS nchini Libya. Mkutano huo unaongozwa na waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry na mwenzake wa Italia Paoli Gentiloni. Msemaji wa wizara ya mambo ya nje ya Marekani John Kiry amesema mkutano huo wa Vienna utajadili uungwaji mkono wa serikali ya Umoja wa kitaifa ya Libya na jumuiya ya kimataifa kwa...
MAMLAKA ya chakula na dawa-TFDA imekutana na adau mbalimbali wa usalama wa chakula na dawa kutoka nchi 12 za bara la Africa ikiwemo Tanzania kwa lengo la kubadilishana uzoefu wa kiutendaji kazi utakaochangia kutatua changamoto zinazoikabili mamlaka hiyo. Akizungumza jijin dar es salaam, Mkurugenzi mkuu wa TFDA HIIT SILLO amesema kuwa kupitia mkutano huo wadau wataweza kuchambua ubora wa maabara zinazozingatia viwango vya upimaji vya vakula, dawa pamoja na viwango vya uchunguzi wa vyakula. Hata hivyo sillo ametoa...
KIJANA mmoja aliyefahamika kwa jina la Ramadhani Saidi mwenye umri wa miaka 20 mkazi wa kijiji cha Manyinga Turiani Wilaya ya Mvomero mkoani Morogoro amenusurika kifo baada ya kupigwa risasi na askari wa jeshi la polisi wakati wakiwa doria usiku wa kuamkia leo. Mkuu wa upelelezi wilaya ya mvomero ASP Peter Majengo akizungumza na wananchi waliokusanyika katika hospitali hiyo amesema tukio hilo lilitokea usiku wakati askari wakiwa doria na walipomuona walimsimamisha kijana huyo na kumtilia shaka kuwa ni jambazi ndipo...
WAZIRI wa Mambo ya nje wa Marekani John Kerry amefanya mazungumzo na Mfalme Salman wa Saudi Arabia kuhusu mizozo ya Syria, Libya na Yemen, kabla ya mikutano ya kimataifa inayopangwa kuandaliwa wiki ijayo barani Ulaya kuhusu mizozo hiyo. Ziara ya Kerry, ambaye pia amefanya mazungumzo na mwanamrithi wa ufalme na naibu mwanamrithi wa ufalme na waziri wa mambo ya nje, inakuja katika wakati muhimu wa kuimarisha juhudi za kudhibiti mapigano na kuhimiza mazungumzo ya kisiasa katika nchi zote tatu ambazo...
MKUU wa Mkoa wa Dar es Salaam, Paul Makonda amesema wanawake wamekuwa ni chanzo cha ufisadi nchini kutokana na kupokea zawadi zitokanazo na fedha za kifisadi. Makonda aliyasema hayo wakati akizungumza na wananchi wa Kata ya Mnyamani Vingunguti Jijini Dar es Salaam jana katika mkutano wa kujadili namna ya kupata mikopo mbalimbali kutoka Benki ya Wananchi Dar es Salaam (DCB). Makonda amewaambia wanawake hao kuwa hata katika suala la usafi linaanzia na malezi ya usafi ya akina mama kwa watoto...
Watu 31 wameuawa kwa bomu la kujitoa muhanga nchini Yemen,shambulizi linalodaiwa kutekelezwa na wanamgambo wa Islamic state. Polisi wamethibitisha kutoka kwa shambulizi hilo katika ngome iliyoko kusini mwa nchi hiyo ya Mukalla. Vyanzo kutoka idara ya afya vinasema kuwa zaidi ya watu sita wamejeruhiwa katika shambulizi hilo. Maafisa wanasema kiongozi mmoja wa ulinzi na usalama alilengwa katika shambulizi la pili,ambapo aliponea chupuchupu, lakini walinzi wake wapatao sita waliuawa. Mashambulizi haya yanakuja pakiwa panafanyika mzungumzo ya...
Mahakama nchini Misri imewahukumu kwenda jela watu sita kwa tuhuma za kumpiga hadi kumuua raia wa Ufaransa katika kituo cha Polisi walikokuwa wamewekwa kizuizini. Eric Lang mwenye umri wa miaka 49 aliyekuwa mwalimu wa lugha aliwekwa kizuizini nchini Misri miaka mitatu iliyopita. Kwa mjibu wa upande wa mashitaka ni kwamba Lang aligombana na wenzake wakiwa rumande ambapo walianza kumshambulia hadi kumsababishia kifo chake. Hata hivyo Polisi wa Misri wamekuwa wakituhumiwa kuhusiaka na mauaji ya mwanafunzi raia wa Italia Giulio Regeni...