Watangazaji mahiri Gerald Hando na Paul James (PJ) wameanza rasmi kutangaza 93.7 Efm redio siku ya leo ya tarehe 02/05/2016 katika kipindi cha Joto la asubuhi kilichoboreshwa wakiwa pamoja na Adela Tilya live nje ya jengo la K- net house zilipo ofisi za E fm. Kipindi hiki kinarushwa kuanzia Jumatatu hadi Ijumaa saa 12:00 hadi saa 3:00 Asubuhi. Usipitwe. Kutoka kushoto ni Gerald Hando, Adella Tillya, pamoja na Paul James wakitangaza live chini ya jendo la K-net house. Rdj Spar akisababisha muziki live katika kipindi cha...
Kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa kwenye tovuti ya Standard Digital nchini Kenya zinasema kuwa mashirika mawili ya serikali nchini humo yamewatangazia watumiaji wa njia za Lang’ata, Muhoho, Popo, Lusaka, Gichuru, Ushirika, Jakaya Kikwete, Lenana, Jogoo kuwa makini na barabara hizo kutokana na mafuriko, hivyo watumiaji wametakiwa kuepuka njia hizo katika kipindi cha mvua kubwa zinazopelekea kuharibika kwa miundombinu ya...
Leicester City wamebakiwa na alama mbili pekee kuupata ushindi wa ligi kuu ya England baada ya kupata sare ya 1-1 dhidi ya klabu ya Manchester United katika dimba la Old Trafford huku wakitegemea matokeo ya mchezo kati ya Chelsea dhidi ya Tottenham utakaopigwa leo hii majira ya saa nne usiku kwa saa za afrika mashariki katika dimba la Stamford Bridge. Mbweha walipata afueni baada ya kuwa nyuma kwa goli moja lililofungwa na Antony Martial dakika ya nane ya mchezo kabla...
Mcheza tenisi wa Bulgaria Grigor Dimitrov ameomba radhi baada ya kuonyesha utovu wa nidhamu pale alipoibamiza chini mara tatu fimbo yake ya kuchezea baada ya kukubali kichapo dhidi ya Diego Schwartzman katika michuano ya wazi ya Istanbul. Mbulgaria huyo aliyekuwa akilisaka taji lake la kwanza katika kipindi cha miaka miwili alipoteza kwa seti 6-7,5-7,7-6, 7-4,na 6-0. Dimitrov alipewa onyo kali aliporusha kwa mara ya kwanza na kwa hasira fimbo yake ya kuchezea mapema mnamo seti ya tatu na kisha akapewa...
WANASAYANSI nchini Brazil wamesema kuwa virusi vya ZIKA ambavyo vimehusishwa na kuzaliwa kwa watoto wakiwa na vichwa vidogo huenda ni hatari zaidi kuliko ilivyofikiriwa awali. Madaktari bingwa wamesema kuwa virusi vya Zika vinaweza kuwa sababu ya kutokea kwa matatizo ya neva za fahamu kwa mwanamke mmoja mjamzito kati ya watano wanaoathiriwa na Virusi hivyo. Madaktari wengi na watafiti kwa sasa wanakubali kuwa kuna uhusiano kati ya mbu anayeeneza virusi na tatizo la watoto kuzaliwa na dosari kwenye...
MKURUGENZI wa CIA John Brennan amesema kwa miaka mitano iliyopita Marekani imeharibu kwa kiasi kikubwa kundi la Al Qaed baada ya kuuawa kwa kiongozi wake mkuu Osama bin Laden kutokana na uvamizi wa vikosi maalum nchini Pakistan. Brennan amesema kuwa Bin Laden alikuwa nembo na mwenye mikakati imara na muhimu na ilikuwa lazima kumuondoa mtu huyo ambaye amehusika katika mashambulizi ya kigaidi mjini Washington na New York Septemba 11. Mkuu huyo wa CIA ameongeza kuwa kumuondoa kiongozi wa IS Abu Bakr Al-Baghdadi...
WAZIRI wa Afya Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Bi. Ummy Mwalimu ameziagiza hospitali mbalimbali nchini kuhakikisha zinachukua tahadhari za kuwalinda wafanyakazi wake kitengo cha kumbukumbu katika mazingira ya kupata maambukizi hasa wanapokuwa kazini wakitimiza majukumu yao. Waziri, Mwalimu ametoa maagizo hayo kupitia hotuba yake iliyosomwa na Mkurugenzi wa Uhakiki Ubora wa Huduma za Afya kutoka wizara hiyo Dkt Mohamed Mohamed alipomwakilisha katika hafla ya kufungwa kwa mkutano wa Chama cha Maofisa Kumbukumbu na Taarifa za...
TANZANIA leo inaungana na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari Duniani ambapo kitaifa maadhimisho hayo yanafanyika Jijini Mwanza Mei tatu. Katika maadhimisho ya Mwaka huu kubwa linalohimizwa na wadau wa Habari nchini ni kuitaka Serikali kuharakisha kupitisha Sheria ya Vymbo vya Habari kwa kuzingatia maoni yanayotokana na mapendekezo ya wadau mbalimbali. Maadhimisho hayo kwa mwaka huu yanaenda sambamba na matukio muhimu matatu ya kihistoria ya kuadhimisha miaka 250 ya Sheria ya kwanza ya uhuru wa Habari...
Shabiki mmoja wa timu ya Leicester amesema kuwa ana uhakika klabu hiyo itashinda ubingwa wa ligi na kumfanya kupata zaidi ya pauni 20,000 ambayo ni sawa na milioni 64 za Tanzania. Leigh Herbert aliwekeza 5000 baada ya kupata vinywaji kadhaa wakati wa likizo huko Newquay ,Cornwall mwaka uliopita. Nina furaha tele kwa sababu nina uhakika wa asilimia 100 kwamba hilo litafanyika. Leigh aliweka fedha alicheza kamari hiyo kufuatia uteuzi wa mkufunzi Claudio Ranieri.Nilifikiria kwamba atailetea kilabu hiyo kitu maalum. Nilijua...
Beki wa Liverpool Mamadou Sakho amepewa marufuku ya siku 30 na shirikisho la soka barani Ulaya Uefa baada ya kuanzisha harakati za kumuadhibu baada ya kuaptikana ametumia dawa za kusisimua misuli. Marufuku hiyo ni ya mda hadi pale uamuzi wa mwisho utakapoafikiwa na kitengo cha maadili cha shirikisho hilo. Sakho mwenye umri wa miaka 26 alipatikana ametumia dawa za kusisimua misuli kufuatia ushindi wa mechi ya taji la Europa dhidi ya Manchester United mnamo tarehe 27 mwezi Machi. Aliamua kutopinga...
RAIA wa Marekani amefungwa jela miaka 10 na kazi ngumu nchini Korea Kaskazini baada ya kupatikana na makosa ya kufanya ujasusi, shirika la habari la Uchina la Xinhua limeripoti. Kim Dong-chul, raia wa Marekani aliyezaliwa Korea Kusini, alikamatwa mwezi Oktoba mwaka jana. Kim alifikishwa kwa wanahabari mjini Pyongyang mwezi jana na akaoneshwa akikiri makosa, na kusema kwamba alilipwa na Korea Kusini kufanya ujasusi...