Polisi nchini Uingereza imethibitisha kuwa kitu kilichokuwa kinadhaniwa kuwa ni bomu kilichoonekana kwenye uwanja wa timu ya Manchester United wa Old Trafford hakikuwa bomu kama ilivyodhaniwa bali kilikuwa ni kifaa cha wanausalama cha mazoezi kwa ajili milipuko. Kifaa hicho kiliachwa na walinzi wa kampuni moja ya binafsi baada ya kufanya mazoezi yaliyowahusisha mbwa wenye kunusa vifaa na vitu vya kihalifu. Kutokana na kuonekana kwa kifaa hicho mechi kati ya Manchester United na Bournemouth iliahirishwa. Tayari kifaa hicho kimeshaharibiwa chini...
SHIRIKA la Umoja wa Mataifa linalosimamia wakimbizi UNHCR limeitaka serikali ya Kenya kubatilisha msimamo wake wa kutaka kuzifunga kambi mbili za wakimbizi ikiwemo ya Dadaab nchini humo. Awali siku ya Ijumaa iliyopita Serikali ya Kenya ilisema kwamba kambi hizo mbili zitafungwa kufuatia wasiwasi wa usalama na ukosefu wa fedha. Aidha imetoa tangazo kama hilo mapema, lakini wakati huu serikali imesema kuwa inazifunga kambi zake za wakimbizi katika kile kinachoonekana kama hatua ya kwanza ya kusitisha uhifadhi wa wakimbizi Laki...
MEYA wa jimbo aliyeongoza kampeni kali ya urais nchini Ufilipino, Rodrigo “Digong” Duterte ameshinda uchaguzi huo kufuatia kujitoa kwa wapinzani wake. Licha ya kwamba matokeo rasmi hayajatangazwa, mpinani wake mkuu Mar Roxas amekiri kushindwa baada ya kura zinazohesabiwa kudhihirisha Duterte anaongoza kwa kura nyingi. Mgombea huyo aliye na umri wa miaka 71 alizusha mzozo wakati wa kampeni kwa matamshi yake makali....
KATIKA kutekeleza agizo la serikali la kuwafikia wateja laki 4 ifikapo June mwaka 2016 Shirika la Majisafi na Majitaka jijini Dar es salaam (Dawasco) limesema linaendelea na zoezi la uunganishaji wa huduma ya Maji kwa wananchi wote wa jiji la Dar es salaam. Akizungumza na waandishi wa habari Afisa mtendaji mkuu wa Dawasco, Mhandisi Cyprian Luhemeja ameeleza kuwa kwenye awamu hii ya zoezi la uunganishaji wateja wapya shirika litagharamia gharama zote za maunganisho ambazo ni gharama za uunganishaji mabomba na vifaa...
WAZIRI mkuu wa jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Kassim Majaliwa anatarajiwa kuondoka nchini leo kwenda London nchini Uingereza kuhudhuria mkutano wa wakuu wa nchi kuhusu mapambano dhidi ya rushwa. Akizungumza na waandishi wa Habari Jijini Dar es salaam, Mheshimiwa Majaliwa amesema kuwa anaenda kumuwakilisha Mheshimiwa Rais kwa sababu siku hiyo ya mkutano atalazimika kuhudhuria sherehe za kuapishwa kwa Rais Yower Museven Akizungumzia kuhusu suala la kupambana na rushwa waziri Mkuu amesema kuwa Tanzania inafanya jitihada...
Kesi dhidi ya mwanamke mfanyabiashara raia wa China anayetuhumiwa na mashtaka ya kuendeleza mtandaoa wa kihalifu wa ulanguzi wa pembe barani Asia imeahirishwa kwa wiki mbili nchini Tanzania. Alifikishwa mahakamani Jumatatu asubuhi mjini Dar es Salaam. Waendesha mashtaka wanasema Yang Feng Glan, anayejulikana kwa umaarufu pia kama Malkia wa pembe, aliendesha biashara haramu ya kuwaua ndovu katika mbuga za wanyama ili kupata pembe zao ambazo wanazisafirisha na kuziuza katika mataifa ya bara Asia. Anashutumiwa kwa kuendeleza shughuli hiyo kwa...
Sehemu ya jumba kubwa la kibiashara mjini Mombasa imeporomoka siku chache baada ya jumba la makazi kuporomoka jijini Nairobi na kusababisha vifo vya watu zaidi ya 40. Sehemu ya jumba hilo la Nyali Centre iliporomoka usiku wa kuamkia Jumatatu. Hakuna aliyeripotiwa kujeruhiwa wakati wa mkasa huo. Polisi, maafisa wa Shirika la Msalaba Mwekundu na maafisa wa Mamlaka ya Taifa ya Ujenzi (NCA) wamefika eneo hilo kufanya uchunguzi...
Odinga zikiwa jukwaan zikisubiri kushindaniwa Majaji wakiandaa eneo la kufanya mashindano Swebe Santana akisherehea Choggo Chema Mmoja ya washiriki akipokea maelekezo Mashabiki wakifuatilia mtanange Mashindano yakiendelea David Urasa akikabidhi zawadi kwa baadhi ya washiriki walioingia kwenye fainali kuiwakilisha Kibaha Washindi wa pikipiki wakiwa kwenye pikipiki zao Matery Mushi akikabidhi zawdi kutoka Vodacom Meneja Mkuu E-fm, Denis Ssebo akizungumza na wakazi wa Kibaha Mzee Kungu baya akitoa burudani ya...
Jurgen Klopp amefanikiwa kuifikisha Liverpool katika hatua ya fainali ya ligi ya Uropa baada ya kuibuka na ushindi wa mabao 3-0 dhidi ya Villarreal. Wakiwa nyuma kwa bao moja katika mchezo wa awali, Liverpool walisawazisha matokeo baada ya Bruno Soriano kujifunga. Daniel Sturridge aliongeza bao la pili baadaye na kuanza kuidididmiza timu hiyo kutoka Uhispania baada ya kupokea pasi safi kutoka kwa Roberto Firmino. Baada ya mchezaji wa Villareal Victor Ruiz kutolewa kwa kadi nyekundu, Adam Lallana alipigilia msumari wa...
SPIKA wa Republican katika Baraza la Wawakilishi la Marekani Paul Ryan amesema hayupo tayari kumuunga mkono Donald Trump kuwa mgombea wa Urais kupitia chama hicho. Mfanyabiashara huyo bilionea anaonekana dhahiri kushinda katika mbio za uteuzi kukiwakilisha chama hicho lakini Ryan amesema kuwa kabla hakuweza kuidhinisha suala hilo Trump alipaswa kuwaonyesha watu kuwa anaheshimu taratibu za Republican na angepata kura za Wamarekani wengi zaidi. Mapema Marais wa zamani wa Marekani George W Bush na baba yake George Bush waliweka wazi kuwa...
AFISA mwandamizi wa Umoja wa Mataifa amesema mashambulizi ya ndege za angani katika kambi ya wakimbizi,yanahofiwa kuwaua zaidi ya watu 30. Mkuu wa kitengo cha haki za binaadamu katika umoja wa mataifa, Stephen O’Brien ametaka pawepo uchunguzi juu ya shambulizi hilo lililotokea katika jimbo la Idlib, karibu na mpaka wa Uturuki. Waziri wa mambo ya nje wa Uingereza Philip Hammond amemtuhumu Rais wa Syria Bashar Al-Assad kwa kuonyesha dharau juu ya juhudi za kimataifa kumaliza mapigano nchini...