UMOJA wa Ulaya na Uturuki wamekubaliana, kwa mujibu wa ripoti za vyombo vya Habari juu ya namna ya kuwachagua wakimbizi wa Syria watakaohamishiwa katika nchi za Umoja huo. Gazeti la “Bild” limenukuu waraka wa siri unaoonyesha kwamba wasyria tu ndio watakaoruhusiwa kwanza kuingia katika nchi za Umoja wa ulaya ikiwa wameomba kinga kabla ya novemba 29 nchini Uturuki. Aidha taarifa zimeeleza kwamba Makubaliano ya awali yanawataka wakimbizi kutojichagulia wenyewe nchi wanayotaka wapelekwe na badala yake kukubali kupangiwa nchi za...
RAIS wa zamani wa Burundi Kanali Jean-Baptiste Bagaza amefariki dunia wakati akipatiwa matibabu katika hospitali ya Sainte Elisabeth mjini Brussels nchini Ubelgiji. Kwa mujibu wa taarifa iliyotolewa na mshauri wa rais wa Burundi Willy Nyamitwe kupitia mtandao wa kijamii wa Twitter imeeleza kuwa Kanali Bagaza aliingia madarakani Novemba 1976 kupitia mapinduzi ya kijeshi. Hata hivyo baadaye aliondolewa madarakani kupitia mapinduzi mengine yaliyoongozwa na binamu yake Meja Pierre Buyoya mwezi Septemba...
JAMII imetakiwa kushirikiana na Serikali pamoja na Sekta binafsi zinazojishughulisha na mapambano dhidi ya matumizi ya dawa za kulevya kwani vita hiyo ni ya kila Mtanzania mwenye nia njema na vijana. Wito huo umetolewa na Mkurugenzi wa Kituo cha kusaidia waathirika wa Dawa za kulevya cha Pili Misana Foundation kilichopo Kigamboni jijini Dar es salaam Bi Pili Misana alipozungumza na Waandishi wa habari katika hafla ya kituo hicho kufikisha miaka minne tangu kuanzishwa kwake. Bi. Misana amesema tangu kuanzishwa kwa vituo...
SERIKALI imesema kuwa maendeleo katika sekta ya fedha kwa kutumia teknolojia yamepiga hatua kubwa kwa kupitia mkonge wa Taifa imekuwa rahisi kwa Watanzania kutumia na kuchochea kasi ya biashara na kujenga uchumi wa Taifa kwa ujumla. Akizungumza na E fm Jijini Dar es salaam Naibu Waziri fedha na Mipango Dokta Ashatu Kijaji amesema kuwa Watanzania wana nafasi kubwa ya kutumia teknolojia hiyo vizuri na itasaidia kuinua uchumi na kuchochoea maendeleo ya Taifa. Amebainisha kuwa Serikali imejipanga vizuri katika kudhibiti udanganyifu na...
Mwingereza Andy Murray ameanza vyema kutetea taji lake katika michuano ya Madrid Open kwa ushindi wa seti 7-6 7-3 3-6 na 6-1 dhidi ya Radek Stepanek. Ilichukua muda wa saa mbili na dakika 16 kwa Murry kumshinda Stepanek raia wa Czech mwenye miaka 37. ”Sikucheza michezo mingi kipindi cha nyuma.Ilikua ngumu sana,”alisema Murray mwenye miaka 28 ambaye atakutana na Gilles Simon ama Pablo Busta katika mzunguko wa tatu siku ya Alhamisi. Mapema kwenye mchezo wa awali Muhispaniola Rafael Nadal alimshinda...
IDADI ya watu waliofariki baada ya jumba la ghorofa sita kuporomoka siku ya Ijumaa imeongezeka baada ya miili zaidi kupatikana kwenye vifusi. Maafisa wa uokoaji wamepata miili mitatu zaidi na kufikisha miili 26, ambayo ni idadi ya watu waliofariki kutokana na mkasa huo uliotokea baada ya mvua kubwa kunyesha. Hata hivyo Shirika la msalaba mwekundu nchini humo limeeleza kuwa Watu 93 bado hawajulikani...
SENETA wa jimbo la Texas Ted Cruz amejiondoa katika kinyang’anyiro cha uteuzi wa kugombea nafasi ya urais wa Marekani kupitia chama cha Republican. Cruz ametoa tangazo lake muda mfupi baada ya kupoteza kura katika kampeni za mwisho Indiana. Katika hatua nyingine Seneta wa Vermont- Bernie Sanders amemshinda Hillary Clinton kwenye uchaguzi wa mchujo wa kuteua mgombea urais wa chama cha Democratic katika jimbo la...
INAKADIRIWA kuwa Watu laki nne hupoteza maisha kila mwaka Nchini kutokana na athari zitokanazo na mabadiliko ya hali ya hewa ikiwemo mafuriko, ukame na migogoro ya rasilimali kwa Wakulima na Wafugaji. Hayo yamesemwa Jijini Dar es salaam na Dokta Azma Simba katika Semina maalum ya Wanahabari iliyoandaliwa na Wizara ya Afya kwa kushirikiana na Mamlaka ya hali ya hewa lengo ikiwa ni kuwajengea uwezo Wanahabari kutoa elimu juu ya athari za mabadiliko ya tabia nnchi. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi wa Idara ya...
MAAFISA wanne wa polisi nchini China wamesema kuwa watashirikiana na wenzao wa Itali kupiga doria mjini Rome na Milan katika jaribio la wiki mbili zijazo. Waziri wa mambo ya nje wa Italia Angelino Alfano amesema Maafisa hao wanaozungumza Kiitaliano wanatumwa nchini Italia kwa lengo la kuwafanya watalii wa China kujisikia huru na salama wakati huu wa msimu wa juu wa utalii. Takribani watalii milioni 3 kutoka nchini China hutembelea nchi ya Italia kila mwaka....
MJUMBE wa Umoja wa Mataifa Staffan De Mistura anatarajiwa kukutana na waziri wa masuala ya kigeni nchini Urusi kujadiliana kuhusu juhudi za kunusuru kuvunjika kwa mkataba wa amani nchin Syria. De Mistura anataka Urusi na Marekani ambazo zinaunga mkono makundi pinzani nchini humo kushirikiana ili kurejesha makubaliano waliopatana mwezi Februari. Hata hivyo Washington imeilaumu Moscow kwa kushindwa kuwazuia wanajeshi wa Syria waliopo mjini...
NAIBU balozi wa Uingereza hapa nchini, Matt Sutherland, ameisifu taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete kwa kuratibu kambi ya upasuaji wa moyo kwa kushirikiana na madaktari kutoka nje kwa mafanikio makubwa. Pongezi hizo amezitoa leo baada ya kutembelea kambi hiyo maalum iliyoko kwenye taasisi hiyo na kujionea madaktari wakiendelea na kazi ya kuwafanyia upasuaji watoto wa Kitanzania kutoka sehemu mbalimbali nchini. Taasisi ya Muntada Aid, ni taasisi ya Kiislamu yenye makazi yake nchini Uingereza, ambayo ndiyo iliyowezwesha kuwaleta madaktari na...