MUFTI Mkuu wa Tanzania Sheikh Abubakar Zuber bin Ally amewataka watanzania kudumisha umoja na mshikamano ili kujenga taifa na kuleta maendeleo. Sheikh Zuber ameyasema hayo wakati akizungumza na baraza kuu la waislamu Tanzania BAKWATA katika semina elekezi kwa viongozi wa baraza hilo Taifa. Naye Sheikh mkuu wa mkoa wa Mtwara Nurdin Abdala Athumani ameongeza kuwa watanzania ili wapate maendeleo ni lazima watumie viwanda ipasavyo kuzalisha na kudumisha suala la umoja pamoja na amani iliyopo kwa manufaa ya...
WIZARA ya Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imesema kuwa inakusudia kutoa taarifa ya wanawake wanaofariki Dunia kutokana na matatizo ya uzazi kila baada ya miezi mitatu ili kukabiliana na tatizo la vifo vya wanawake nchini. Hayo yamesemwa na Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Mheshimiwa Ummy Mwalimu Jijini Dar es Salaam wakati akifungua Mkutano wa Viongozi Wanawake kuhusu masuala ya Afya. Ameeleza kuwa, katika uteuzi atakaoufanya kwenye bodi zilizo chini ya Wizara...
SERIKALI ya Uganda imepiga marufuku urushwaji wa matangazo ya moja kwa moja yanayopinga uchaguzi wa rais Yoweri Museveni. Usalama katika mji mkuu wa Uganda- Kampala umeimarishwa kabla ya maandamano yalioitishwa na chama cha Forum for Democratic Change (FDC). Vyombo vya habari nchini Uganda vimetakiwa kutofanya matangazo ya moja kwa moja na wanachama wa upinzani ambao wanapinga kuchaguliwa kwa rais...
IMEBAINIKA kwamba Mwanamke amepatikana akiwa hai kwenye vifusi ikiwa ni siku sita baada ya jengo kuporomoka katika mtaa wa Huruma jijini Nairobi. Kwa mujibu wa Pius Masai, mkuu wa kitengo cha taifa cha kukabiliana na majanga, amesema kuwa maafisa wa uokoaji bado wanajaribu kutengeneza njia ya kumtoa kwenye vifusi hivyo. Hata hivyo, mwanamke huyo amekuwa akiwasiliana na matabibu ambao wanasubiri kumpatia matibabu punde...
JESHI la polisi Mkoa wa kipolisi Ilala limewahakikishia usalama wananchi wa Mkoa wa kipolisi Ilala na kuachana na taarifa za uvumi kuwa hali ya usalama katika mkoa huo wa kipolisi sio nzuri. Akizungumzia suala hilo, Kamanda wa Polisi Mkoa wa Ilala Kamishna Msaidizi Mwandamizi wa Polisi Lucas Mkondya amesema kuwa Jeshi la Polisi limejipanga ipasavyo kukabiliana na uhalifu wa aina yoyote. Kuhusiana na malalamiko ya wananchi wa Buguruni kuhusiana na kuwepo kwa kundi la vibaka na waporaji kamanda Mkondya amesema...
MKOA wa Dar es salaam unatarajiwa kuwa na watu milioni 10 ifikapo mwaka 2030 hivyo ni muhimu kuzingatia uboreshaji wa Jiji kulingana na idadi ya watu. Hayo yamebainishwa leo na Mkuu wa mkoa wa Dar es salaam Mheshimiwa Paul Makonda wakati akizungumza na wanahabari ofisini kwake ambapo amesema kuwa kutokana na kuwepo kwa ongezeko la watu serikali ilibuni mradi wa uendelezaji wa Jiji kwa ufadhili wa benki ya dunia. Amesema kuwa ukuaji wa Jiji la Dar es salaam unakabiliwa na makazi...
MWANASIASA mashuhuri wa Jamhuri ya Demokrasi ya Congo Moise Katumbi amethibitisha kuwa atagombea urais kwenye uchaguzi mkuu unaotarajiwa kufanyika mwezi Novemba. Mfanyabiashara huyo na gavana wa zamani wa jimbo la Katanga ametoa tangazo hilo kupitia mitandao ya kijamii. Muungano wa vyama kadhaa vya upinzani nchini humo umeamua kumuidhinisha Bwana Katumbi kuwa mgombea wao wa nafasi ya Urais katika Uchaguzi...
WABUNGE wa Bunge la Afrika Kusini wamepigana bungeni baada ya spika kuamuru maafisa wa usalama kuwaondoa kwa lazima wabunge wa upinzani ambao walimbeza rais Jacob Zuma alipoingia bungeni kwaajili ya kuwahutubia. Rais Zuma ambaye ameshindwa katika kesi mbili kuu zinazomhusisha na ubadhirifu wa mali ya umma na usimamizi mbaya alikuwa amefika bungeni kwa mara ya kwanza tangu kushindwa mahakamani. Hata hivyo ujio wake uliwakera wabunge wa chama cha upinzani cha Economic Freedom Fighters (EFF) ambao walipiga mayowe na kumtupia matusi Rais...
MKURUGENZI wa Idara ya Ajira Ameir Ali Ameir amesema tatizo la ajira nchini bado ni changamoto kubwa kwa vijana kutokana na vijana wengi kukosa sifa za kuajiriwa na baadhi yao kuchagua kazi za kuajiriwa. Ameir ameyasema hayo katika Ukumbi wa Kidongo chekundu wakati alipokuwa akifungua mafunzo ya Kuwajengea Uwezo wa Kamati za Ajira za Wilaya za Mjini na Magharibi. Amesema vijana ndio nguvu kazi katika jamii hivyo wana nafasi kubwa katika kulitumika Taifa kwa kufanya kazi lakini mtazamo wa vijana bado...
SERIKALI imesema kuwa inatarajia kutoa mafunzo kwa wasimamizi 61 wa shughuli za Kemikali na madereva 123wanaosafirisha Kemikali mbalimbali ili kuzuia athari zinazotokana na matumizi yasiyozingatia sheria na kanuni za kemikali. Akizungumza jana Jijini Dar es salaam wakati wa mkutano na waandishi wa Habari, Mkuu wa Kitengo Cha Utafiti na ubora wa Mifumo Benny Mallya kutoka Ofisi ya Wakala wa Maabara ya Mkemia Mkuu wa Serikali amesema mafunzo hayo ni sehemu ya utekelezaji wa sheria ya usimamizi na udhibiti wa kemikali za viwandani...
Chelsea na Tottenham wamepigwa faini kwa pamoja na shirikisho la soka nchini Uingereza FA kwa kukabiliwa na makosa matatu ya kushindwa kuwazuia wachezaji pamoja na maofisa wake wakati na baada ya mchezo wa jumatatu. Kiungo wa Spurs Mousa Dembele amekumbana na adhabu pia ya kusababisha vurugu katika mchezo huo ulioisha kwa suluhu ya 2-2.FA inasema kuwa kitendo cha Dembele kumuingizia vidole machoni mchezaji wa Chelsea Diego Costa ni utovu mkubwa wa nidhamu. Hiyo ina maana ”akikutwa na hatia” kufungiwa michezo...