MAMLAKA ya hali ya hewa Nchini-TMA-imewataka Wakulima na Wafugaji kufuatilia na kutumia taarifa za hali ya hewa zinazotolewa ili kuongeza ufanisi wa uzalishaji katika kilimo na Ufugaji. Akizungumza kwa niaba ya Mkurugenzi mkuu wa mamlaka hiyo, Mkurugenzi wa Utafiti na Matumizi ya hali ya hewa Nchini Dokta Ladislaus Chang’a amesema mifugo mingi pamoja na mazao ya kilimo yamekuwa yakiharibika kutokana na mabadiliko ya hali ya hewa jambo ambalo husababisha upungufu katika uzalishaji hivyo ni muhimu kwa wakulima hao kufuatilia taarifa...
TIMU ya kimataifa ya wanasayansi imekamilisha utafiti mkubwa zaidi kuwahi kutokea wa maumbile ya saratani ya matiti, ambayo wamesema inawapa karibu picha kamili ya nini husababisha ugonjwa huo. Wanasayansi hao wanajaribu kutizama mfuatano wa jinomu kamili wa kesi zaidi ya mia tano za saratani ya matiti. Utafiti huo unaoongozwa na taasisi ya Cambridge umeweza kugundua aina tano mpya za visababishi vya ugonjwa huo ambavyo vikibadilika husababisha uvimbe katika sehemu husika ya mwili wa...
MTOTO mwenye umri wa mwaka mmoja na nusu amepatikana akiwa hai kwenye vifusi vya jengo lililoporomoka siku ya Ijumaa jijini Nairobi nchini Kenya. Jengo hilo la ghorofa sita liliporomoka katika mtaa wa Huruma baada ya mvua kubwa kunyesha. Akizungumzia hali ya afya ya mtoto huyo, Kamanda wa kitengo cha taifa cha kudhibiti majanga Pius Maasai amesema kuwa hali ya mtoto huyo inaendelea kuimalika tangu alipofikishwa hospitalini...
KAMATI Maalumu iliyoundwa kutoka Tume ya Taifa ya Uchaguzi kwa ajili ya kuandaa Taarifa ya Uchaguzi Mkuu wa Rais, Wabunge na Madiwani uliofanyika nchini Oktoba 25 mwaka 2015 imekamilisha Rasimu ya kwanza ya Taarifa hiyo na kuiwasilisha kwa Tume. Akizungumza Katika kikao cha Tume baada ya kupokea Rasimu hiyo ya kwanza, Mwenyekiti wa Tume ya Taifa ya Uchaguzi Jaji Mstaafu Damian Lubuva amepongeza kazi iliyofanywa na Kamati hiyo licha ya majukumu mbalimbali yanayotekelezwa na Tume hiyo kwa sasa. Jaji Lubuva ameeleza kuwa Tume...
Maelfu ya waombolezaji walijitokeza kuadhimisha misa ya wafu kwa heshima ya mwanamuziki nyota wa muziki wa Soukus na Rhumba raia wa Jamhuri ya Congo Papa Wemba. Waomboloezaji walipiga foleni ilikupata fursa ya kutoa heshima zao za mwisho kwa msanii huyo nguli aliyeaga dunia juma lililopita alipokuwa akiwatumbuiza mashabiki wake huko Abidjan Ivory Coast. Mwili wake umewekwa katika majengo ya bunge mjini Kinshasa. Serikali imetangaza siku tatu za maombolezi kuanzia leo hadi jumatano atakapozikwa. Tayari amepewa tuzo kwa mchango wake. Msanii...
WAKATI Leo ni kilele cha siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, katibu wa baraza la habari Tanzania MCT-KAJUBI MUKAJANGA amesema kuwa uwepo wa vikwazo mbalimbali katika uhuru wa vyombo vya habari ikiwemo uingiliwaj wa urushwaji wa matangazo ya bunge moja kwa moja unaweza kuchangia kwa kiasi kikubwa urudishwaji nyuma wa mafanikio yaliopatikana katika tasnia ya habari nchini. Akizungumza na Efm Mukajanga amesema kuwa wadau wa habari wakiwemo waandishi wa Habari na serikali wana kazi kubwa ya kulinda mafanikio yaliopatikana katika...
Leicester City watajizolea $200m (£150m) baada yao kufanikiwa kushinda Ligi Kuu ya Uingereza Jumatatu, watathmini wa michezo na utangazaji wa Repucom wanasema. Pesa hizo zinatokana na tuzo ya kushinda Ligi ya Premia, pesa za kushiriki Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya, na ongezeko la mapato ya kila siku kutokana na mauzo ya tiketi. Klabu hiyo pia itajivunia kupanda kwa thamani ya udhamini na pia ongezeko la mashabiki duniani. Klabu hiyo inayotoka East Midlands itashiriki katika Ligi ya Klabu Bingwa Ulaya msimu...
IMEELEZWA kuwa Wanajeshi wa Uingereza wamewasili nchini Somalia kusaidia katika juhudi za kukabiliana na wapiganaji wa Kiislamu wa Al-Shabaab. Wanajeshi 10 waliowasili nchini Somalia ni sehemu ya kikosi cha umoja wa mataifa na watasaidia kikosi cha wanajeshi wa Umoja wa Afrika (Amisom) kukabiliana na Al-Shabaab. Idadi ya wanajeshi wa Uingereza nchini Somalia inatarajiwa kupanda hadi 70 ambao watahusika na shughuli za matibabu, mipango na...
WAZIRI wa mambo ya nchi za nje wa Marekani John Kerry amefungua siku ya pili ya mazungumzo mjini Geneva yenye lengo la kutafuta njia ya kupata suluhu ya mapigano nchini Syria. Kerry amekutana na Waziri wa mambo ya nchi za nje wa Saudi Arabia Adel Al-Jubeir na anapanga pia kuwa na mazungumzo baadae na mjumbe maalumu wa Umoja wa Mataifa anayehusika na Syria Staffan De Mistura. Waziri Kerry amesema hatua za maelewano kuhusu njia ya kupunguza mashambulizi mjini Aleppo zinaendelea kuimarika,...
WAKATI Tanzania Leo ikiungana na Mataifa mengine Duniani kuadhimisha siku ya Uhuru wa Vyombo vya Habari, imeelezwa kuwa watu takribani milioni 700 duniani wanaishi katika hali ya umasikini uliokithiri. Hayo yameelezwa na ofisa Habari wa ofisi ya ya umoja wa mataifa Tanzania USIA NKOMA wakati akizungumza katika siku ya kwanza ya maadhimisho ya Uhuru mkoani Mwanza. USIA amesema kuwa watu wengi wameendelea kushuhudia kuongezeka kwa ukosefu wa usawa hata baada ya nchi kufaulu kupata wastani wa maendeleo ya kiuchumi....
WAKUU wa Idara zote za Mkoa wa Dar es Salaam wametakiwa kuhakikisha wanatoa majina yote ya watumishi hewa ndani ya muda wa siku saba kuanzia leo. Agizo hilo limetolewa na Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mheshimiwa Paul Makonda wakati akizungumza na wakuu wa idara mbalimbali nchini, maafisa utumishi, wakurugenzi wa wilaya na viongozi wengine. Baada ya kutoa agizo hilo Mheshimiwa makonda amewataka Wakuu wa idara zote za mkoa huo, kusaini Mkataba wa kiapo cha kutojihusisha na suala la...