WAPINZANI WA TRUMP WAUNGANISHA NGUVU KUMZUIA
Local News

WAPINZANI wawili wakuu wa Donald Trump katika kinyang’anyiro cha kumteua mgombea urais wa chama cha Republican nchini Marekani wametangaza mipango ya kuungana kukabiliana na mgombea huyo. Ted Cruz na John Kasich wanataka kushirikiana kupunguza uwezekano wa mfanyabiashara huyo tajiri kutoka New York kushinda mchujo katika majimbo zaidi. Cruz, ambaye ni seneta wa jimbo la Texas, amesema atapunguza kampeni zake katika majimbo ya Oregon na New Mexico, Kwa upande wake John Kasich, ambaye ni gavana wa Ohio, naye amesema atamwachia Cruz katika...

Like
247
0
Monday, 25 April 2016
WANANCHI KUNUFAIKA NA UVUVI KWENYE BWAWA LA MTERA
Local News

WANANCHI wanaoishi kando ya bwawa la mtera mkoani Iringa wataendelea kunufaika na shughuli za uvuvi kutokana na bwawa hilo kujaa maji. Wakizungumzia kujaa huko kwa maji baadhi ya Wavuvi wamesema hali ya uchumi wao imeanza kutengemaa tofauti na ilivyokuwa awali kwa kuwa Samaki wameanza kupatikana kwa wingi. Nao wafanyabiashara wa Samaki wamesema bei ya samaki inaendelea kushuka kutokana na Samaki kupatikana kwa...

Like
489
0
Monday, 25 April 2016
SUDAN KUSINI: MATAIFA YENYE NGUVU YATAKA MACHAR AREJEE JUBA
Global News

MATAIFA makuu duniani yamewapa muda viongozi wa pande zinazohasimiana nchini Sudan Kusini kuhakikisha wanakubaliana na kuhakikisha kiongozi wa zamani wa waasi Riek Machar anarejea Juba ifikapo kesho. Mataifa hayo yamesema kuwa wakishindwa kukubaliana, makubalianao ya amani yaliyolengwa kumaliza miaka miwili ya vita vya wenyewe kwa wenyewe yatavunjika. Siku ya Jumamosi April 23 imewekwa na wawakilishi wa  halmashauri ya JMEC iliyoundwa na Umoja wa Afrika, Umoja wa Ulaya, China, Uengereza, Norway na Marekani ambapo Sudan Kusini ni mwanachama wa...

Like
249
0
Friday, 22 April 2016
MAREKANI: IDADI YA WATU WANAOJIUA YAONGEZEKA
Global News

TAKWIMU rasmi za serikali zinaonesha idadi ya watu wanaojiua nchini Marekani imeongezeka kwa kiasi kikubwa. Takwimu hizo kutoka Kituo cha Taifa cha Takwimu za Afya zinaonyesha kuwa viwango vya watu kujiua vimeongezeka kwa karibu asilimia 25 katika kipindi cha miaka 15 iliyopita. Utafiti huo uliofanyika kwa jinsia zote umeonesha kwamba viwango vya wanawake kujiua ndivyo vilivyoongezeka zaidi, vikipanda kwa asilimia 36 vikiwahusisha zaidi wanawake wa umri wa makamo.                        ...

Like
287
0
Friday, 22 April 2016
23% YA WATOTO NCHINI WANASUMBULIWA NA UGONJWA WA MATUNDU YA MOYO
Local News

IMEELEZWA kuwa asilimia 23 ya watoto nchini wanasumbuliwa na ugonjwa wa matundu ya moyo ambao umekuwa ni moja kati ya magonjwa yanayoongoza kwa kusababisha vifo vingi vya watoto. Akizungumza na Waandishi wa Habari Jijini dar es salaam leo Daktari bingwa wa Magonjwa ya moyo kutoka kitengo cha moyo cha Jakaya Kikwete, Peter Richard amesema kuwa dalili zinazoashiria uwepo wa ugonjwa huo kwa mtoto ni pamoja na kushuka kwa kiwango cha ukuaji na homa kali za mapafu zinazojitokea mara kwa mara....

Like
314
0
Friday, 22 April 2016
TCRA: SIMU BANDIA CHANZO CHA KUUNGUZA NYUMBA
Local News

MAMLAKA ya Mawasiliano Nchini-TCRA-imesema kuwa asilimia 79 ya simu za mkononi zilizofanyiwa utafiti kwa kipindi cha mwezi disemba mwaka jana hadi Februari mwaka huu sio bandia wakati asilimia 18 ya simu hizo ni bandia. Aidha imeeleza kuwa asilimia kubwa ya nyumba zinazoungua kwa umeme kunatokana na simu bandia ambazo betri zake au vifaa vyake hushindwa kuhimili mionzi wakati zinapokuwa zinachajiwa hivyo kusababisha moto. Hayo yamesemwa na meneja uhusiano wa mamlaka hiyo Innocent Mungi wakati akizungumza katika semina ya mfumo wa...

Like
238
0
Friday, 22 April 2016
VOLKSWAGEN YATANGAZA KUNUNUA MAGARI YAKE
Global News

KAMPUNI ya magari ya Volkswagen imetangaza kuyanunua magari ya kampuni yake kutoka kwa wateja nchini Marekani yapatayo laki tano kama sehemu ya kutimiza makubaliano yaliyoafikiwa na idara ya sheria ya Marekani dhidi ya kampuni hiyo kuhusika na kashfa ya uchafuzi wa hali ya hewa. Jaji kutoka San Francisco hajabainisha wazi kiasi ambacho wamiliki wa magari hayo watalipwa na kampuni ya Volkswagen pale watakapo iuzia kampuni hiyo magari yake wanayoyamiliki. Makubaliano mengine yaliyofikiwa ni kwamba Volkswagen itatakiwa kutoa fungu la fedha...

Like
197
0
Friday, 22 April 2016
OBAMA AISIHI UINGEREZA ISIJITOE EU
Global News

RAIS wa Marekani Barack Obama amesema anaunga mkono Uingereza kubaki katika jumuiya ya Umoja wa Ulaya ili kuweza kuchangia katika vita dhidi ya ugaidi na masuala ya wahamiaji na utatuzi wa migogoro ya kiuchumi. Rais Obama amenukuliwa na gazeti la Uingereza la Telegraph, akisema kwamba uanachama wa Uingereza katika umoja wa Ulaya una umuhimu mkubwa na endapo nchi hiyo itajiondoa katika umoja huo itapunguza nguvu katika vita dhidi ya ugaidi duniani. Hata hivyo Obama amesema anatetea hoja ya umoja wa...

Like
227
0
Friday, 22 April 2016
KATIBU MKUU WIZARA YA HABARI, UTALII, UTAMADUNI NA MICHEZO WA SERIKALI YA MAPINDUZI AAHIDI KUTOA HUDUMA BORA
Local News

KATIBU Mkuu wa Wizara ya Habari, Utalii, Utamaduni na Michezo wa Serikali ya Mapinduzi Zanzibar Omar Hassan Omar amesema atahakikisha anasimamia na kutekeleza adhima ya Serikali hiyo ya kuwapatia wafanyakazi wake huduma bora ili waweze kutekeleza kazi zao kwa ufanisi. Mheshimiwa Omar Hassan Omar ameyasema hayo baada ya kukabidhiwa rasmi ofisi na Katibu mkuu aliyemaliza muda wake Ali Mwinyikai katika ukumbi wa Wizara iliyopo Mnazi mmoja visiwani. Amesema utendaji kazi wa Serikali ni wa pamoja  na sio mtu mmoja mmoja hivyo amewaomba viongozi...

Like
209
0
Friday, 22 April 2016
WATENDAJI WA MAMLAKA ZA SERIKALI ZA MITAA WATAKIWA KUTEMBELEA MAENEO YAO YA KAZI
Local News

NAIBU waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa Mheshimiwa Selemani Jafo amewataka watendaji wa mamlaka za serikali za mitaa kuwa na utaratibu wa kutembelea maeneo yao ya kazi ili kujua changamoto zilizopo na kuzitatua. Akizungumza na walimu wa shule ya msingi Nzuguni B mkoani Dodoma wakati wa ziara aliyoifanya Mheshimiwa Jafo amesema kuwa watumishi hawawezi kufanya kazi kwa ubora iwapo hawatakuwa wakitembelea na kukagua maeneo yao ya kazi. Katika ziara yake amewataka walimu wa...

Like
181
0
Friday, 22 April 2016
KENYA YAITAKA ICC KUIKABIDHI FAILI ZA WASHUKIWA 3
Global News

KENYA sasa inataka faili za kesi zinazowakabili wakenya watatu wanaotuhumiwa kuingilia ushahidi wa mashahidi wa ICC kushtakiwa nchini humo. Mwanasheria mkuu Profesa Githu Muigai amesema kuwa Kenya ina mahakama zilizo na uwezo za kushtaki kesi ndogo kufuatia kuanguka kwa kesi kuu iliowahusisha wakenya sita maarufu kama Ocampo 6. Mwanasheria huyo pia ameshtumu idara ya mashtaka katika mahakama ya ICC kwa kushindwa kushirikiana na Kenya kuhusu ombi la awali lililowasilishwa kwa aliyekuwa kiongozi wa mashtaka Moreno Ocampo kuikabidhi Kenya faili...

Like
177
0
Thursday, 21 April 2016
« Previous PageNext Page »