Sports

AMAVUBI KUINGIA MWANZA JAN 21TAYARI KUKIPIGA NA STARS
Slider

Timu ya Taifa ya Rwanda (Amavubi) inatarajiwa kuwasili katika jiji la Mwanza, Januari 21 mwaka huu kwa ajili ya mechi ya kirafiki ya kimataifa dhidi ya Taifa Stars ambapo nyasi zitawaka moto kwenye Uwanja wa CCM Kirumba. Kwa mujibu wa Mkurugenzi wa Mashindano wa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) Boniface Wambura, Amavubi yenye msafara wa watu 26, wakiwemo wachezaji, benchi la ufundi na viongozi itawasili kwa ndege ya RwandAir na siku hiyo hiyo jioni itafanya mazoezi kwenye Uwanja wa CCM...

Like
251
0
Saturday, 17 January 2015
DAVID GINOLA ATANGAZA NIA YA KUWANIA URAIS FIFA
Slider

Mchezaji wa zamani wa Ufaransa David Ginola amesema kuwa atasimama dhidi ya Sepp Blatter kuwania Urais wa shirikisho la kandanda duniani,Fifa. Lakini richa ya kuwa imetangazwa hivyo hakuna uhakika kama Ginola ataendelea na nia yake. Hali hii inakuja kwakuzingatia vigezo ambapo mgombea anahitajika kuungwa mkono na vyama vitano vya soka na kigezo kingine anapaswa kuwa amejihusisha na soka kwa miaka miwili kati ya mitano iliyopita Mchezaji huyo mwenye miaka 47 , aliichezea Ufaransa, pia club ya nchi hiyo Paris St...

Like
322
0
Friday, 16 January 2015
MAKALA YA UCHAMBUZI KUELEKEKEA AFCON 2015 TAIFA LA EQUTORIAL GUINEA
Slider

Miezi michache iliyopita Shirikisho la soka barani afrika CAF linalo ongozwa na raisi wake Issa Hayatou lilikuwa katika wakati mgumu kutokana na taarifa iliyotolewa na walio kuwa waandaaji wa michuano hiyo mwaka huu MOROCO kujivua uwenyeji muda mchache kuelekea kuanza kwa michuano hiyo kwa kuogopa ugonjwa wa Ebola. Shirikisho hilo kwa wakati tofauti likachagua mataifa ya GHANA,SOUTHAFRIKA na NIGERIA kuandaa michuano hiyo nayo yakatolea njee ombi hilo na kuibuka hali ya sintofahamu. Mashabiki wengi walitahamaki kuona Raisi wa EQUTORIAL GUINEA...

Like
393
0
Thursday, 15 January 2015
PAMBANO LA FLOYD MAYWEATHER V MANNY PACQUIAO LINAKARIBIA
Slider

Lile pambano la uzito wa juu lililokuwa likisubiliwa kwa hamu kati ya bondia anaesifika kwa kutopigika raia wa Marekani Floyd Mayweather na bondia mfilipino Pacquiao lipo kwenye hatua za mwisho za maandalizi. Pacquiao ambae anashikilia mkanda wa dunia wa WBO wakati Mayweather anashikilia mkanda wa WBC na WBA Pambano hili linasubiriwa kwa hamu saana maana hawa mabondia wawili wanatajwa kuwa mabondia bora katika kipindi hiki ila hawajawahi kukutana kwenye ulingo...

Like
246
0
Thursday, 15 January 2015
GENOVEVA ANONMA: NILILAZIMIKA KUVUA NGUO KUTHIBITISHA KUWA MIMI NI MWANAMKE
Slider

  Richa ya kutukanwa na kudharaulika zaidi kupitia nyakati ngumu mpaka kwenye maisha ya Familia yake mchezaji huyu hakukatishwa tamaaa katika kuifikia ndoto yake. Nyota yake ilianza kung’aa pale alipoitumikia Equatorial Guinea mnamo mwaka 2008 katika michuano ya kombe la mabingwa Afrika wanawake Alipokuwa Mfungaji wa bao la ushindi katika ardhi ya nyumbani na kuifanya timu yake kua ya kwanza kwa kuipiku Nigeria Hapa ndipo changamoto zilizidi kwa Anonma kutokana na uwezo wake mkubwa kiuchezaji pamoja nguvu hii ilipelekea timu...

Like
291
0
Thursday, 15 January 2015
MENEJA WA ENGLAND AMEAHIRISHA KIKAO BAADA YA WACHEZAJI KUBANWA NA RATIBA
Slider

Meneja wa timu ya taifa ya England Roy Hodgson amejikuta akilazimika kufuta ratiba ya kukutana na wachezaji wake na kupata chakula cha usiku pamoja kufuatia ratiba kuwabana wachezaji hao. Roy Hodgson alikuwa na lengo la kukutana na wachezaji hao mwishoni mwa mwezi wa kwanza ili kuweza kujadili pamoja ikiwemo ushindi dhidi ya Scotland. Shirikisho la mpira wa miguu nchini humo limeeleza kuwa timu hiyo pia ilikuwa ipo kwenye utayari wa kikao hicho ila kufuatia kile kilichotokea wamejikuta wakiahirisha kukutana na...

Like
275
0
Wednesday, 14 January 2015
SIMBA KINARA KOMBE LA MAPINDUZI
Slider

Fainali za kombe la mapinduzi zimemalizika jana katika uwanaja wa Amani mjini Unguja huko zanzabar kwa kuwakutanisha vinara wa ligi kuu ya bara mtibwa sugar na wekundu wa msimbazi Simba Ambapo imeshuhudiwa katika fainali hiyo Simba wakilibeba kombe kwa kuifunga mtibwa kwa mikwaju 4 – 3 baada ya kwenda suluhu kwa sare tasa katika dakika 90 za mchezo Ushndi huo wa simba ni mwanzo mzuri kwa kocha wao mpya kabisa Mserbia Goran kopunorvic ambae amejiunga na club hiyo hivi karibuni...

Like
427
0
Wednesday, 14 January 2015
RADAMEL FALCAO HUENDA HATOICHEZEA MANCHESTER UNITED MSIMU UJAO
Slider

  Kiungo mshambuliaji kutoka Colombia Radamel Falcao anaepokea kiasi cha paundi 265,000 kwa wiki kuna uwezekano wa kutochezea tena katika klabu ya Man Utd Hii imekuja mara baada ya wakala wa mchezaji huyo kusema Falcao ataichezea moja kati ya klabu kubwa duniani katika msimu ujao Hayo yamesemwa na Jorge Mendes. Ambae ndie wakala...

Like
243
0
Wednesday, 14 January 2015
NOVAK DJOKOVIC ATUPWA NJE KWENYE MICHUANO YA WAZI YA QATAR
Slider

Bingwa namba moja katika mchezo wa Tennis, Novak Djokovic ametupwa nje katika michuano ya wazi ya Qatar baada ya kupokea kichapo ca seti 6-7 (2-7) 7-6 (8-6) kutoka kwa Ivo Karlovic. Djokovic ambaye alijitoa katika michuano iliyopita alionekana anashindwa kuendana sawa na kasi ya mkongwe huyo kutoka katika taifa la Croatia mwenye umri wa miaka 35. Kwa matokeo hayo sasa Ivo atacheza na raia wa Hispania, David Ferrer aliyefanikiwa kutinga hatua ya nusu fainali kwa kumtoa Dustin Brown kwa seti...

Like
200
0
Friday, 09 January 2015
YAYA TOURE ANYAKUA TUZO YA MWANASOKA BORA AFRIKA KWA MARA YA NNE MFULULIZO
Slider

Mchezaji wa timu ya taifa ya Ivory Coast na klabu ya Manchester City, Yaya Toure afanikiwa kutwaa tuzo ya mwanasoka bora wa bara la Afrika kwa mara ya nne mfululizo. Tuzo hiyo inayotolewa na shirikisho la soka barani Afrika (CAF), imeshuhudia Yaya Toure akiwapiku wachezaji wawili, Pierre Emerick Aubameyang (Gabon) na golikipa wa timu ya taifa ya Nigeria, Vicent Enyeama. Yaya alipata kura 175 dhidi ya mshambuliaji wa klabu ya Borrusia Dortmund, Aubemayang aliyejinyakulia kura 12o huku Enyeama akiangukia nafasi...

Like
216
0
Friday, 09 January 2015
AFRIKA MAGHARIBI WAAZIMIA KUMALIZA EBOLA
Global News

WAKATI UGONJWA wa maradhi ya Ebola ukiendelea kuwa tishio katika baadhi ya nchi Afrika Magharibi, Wataalam wa Afya nao wameendelea kuweka jitihada zaidi kuhakikisha kuwa wanaumaliza ugonjwa huo. Katika jitihada zao hivi sasa wamebuni mpango wa mawasiliano ya simu ya mkononi wenye mpango maalum inayotoa taarifa kutoka maeneo yaliyokumbwa na...

Like
262
0
Tuesday, 06 January 2015