ISRAEL imetoa wito kwa mataifa yenye nguvu duniani kuiadhibu Iran kwa jaribio lake la hivi karibuni la kurusha makombora ya masafa marefu. Waziri Mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Israel inapeleka dai hilo kwa Marekani, Urusi, China, Uingereza, Ufaransa na Ujerumani-mataifa ambayo yamesaini mpango wa kuiondoshea Iran vikwazo kwa makubalino ya taifa hilo kuachana na mpango wake wa nyuklia. Netanyahu amesema Iran imekwenda kinyume na maazimio ya Umoja wa Mataifa kuhusu majaribio ya makombora, na mataifa hayo yenye...
HUDUMA ya usafiri wa reli ya Kati iliyokuwa imesimama kwa takribani miezi miwili sasa imerejea kufuatia kukamilika kwa ukarabati wa reli hiyo katika eneo la kidete wilayani kilosa, mkoani Morogoro. Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amesema hayo baada ya kukagua na kuridhika na ukarabati uliofanywa katika maeneo ya Magulu, Munisagara, Mzaganza na kidete Wilayani Kilosa. ...
SERIKALI kupitia Wizara ya Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto imeipa hadhi ya kuwa Hospitali Wilaya iliyokuwa Zahanati ya Msoga ambayo tayari imekamilisha jengo lake jipya la Hospitali hiyo inayotarajia kuanza kazi Mwezi Aprili mwaka huu. Akitoa maagizo hayo baada ya ukaguzi wa timu ya wataalam kutoka Wizara hiyo ya Afya , Naibu Waziri wa Afya, Ustawi wa Jamii, Jinsia, Wazee na Watoto, Dk. Hamisi Kigwangalla waliofanya hivi karibuni katika Hospitali hiyo, ameeleza kuwa kuanzia Mwezi Aprili...
Kwa mujibu wa taarifa zilizotoka hivi karibuni inadaiwa kuwa producer Pharell Williams na mwenzie walitengeneza beat ya ngoma ya Kendrick Lamar ilioshinda Award kibao na kisha kutiwa vokali na rappa mwengine mkubwa mwaka moja kabla ya rappa lamar kupewa na kufanya alichofanya. Mwaka 2014 katika party moja baada ya grammy ilidaiwa kuchezwa clip moja ambayo ilisikika kama wimbo huo alisema shahidi mmoja, akasema aidha ilikua ni sauti ya pusha T au fabolous ndie alirap katika biti hiyo. je kwako unadhani...
Thomson Joseph Mloyi ambae ni afisa wa polisi nchini Zimbabwe amefikishwa mahakamani kujibu tuhuma dhidi yake kwa kusema Rais Mugabe ni mzee sana kuwa kiongozi, Afisa huyo pia anadaiwa kumtusi mke wa Rais Mugabe, Grace kuwa kahaba kwa mujibu wa taarifa iliyochapishwa na gazeti binafsi nchini humo Tuhuma dhidi yake zilianza asubuhi ya Machi 5 alipoingia katika moja ya kambi katika kambi ya Craneborne na kukuta maafisa wengine wakifanya maandalizi kwa ajili ya kazi . ndipo afisa huyo...
KOREA KASKAZINI imerusha makombora mawili ya masafa mafupi kuelekea Bahari ya Japan, kwa mujibu wa maafisa wa Korea Kusini. Mkuu wa majeshi wa Korea Kusini amesema makombora hayo yaliruka umbali wa kilomita 500 kutoka kusini mwa Korea Kaskazini, kabla ya kuangukia pwani ya mji wa kusini mashariki mwa Japan, mapema leo. Tayari Japan imetuma rasmi malalamiko yake dhidi ya Korea Kaskazini kupitia ubalozi wake uliopo mjini Beijing, China, kwa mujibu wa shirika la habari la Japan, Kyodo. Korea...
WAGOMBEA wa urais kupitia chama cha Demokrat nchini Marekani Hillary Clinton na mwenzake Bernie Sanders wamekabiliana vikali kuhusu swala la uhamiaji pamoja na maswala mengine katika mjadala mjini Florida. Mjadala huo uliokuwa moja kwa moja kupitia runinga mjini Miami ulifanyika siku chache tu kabla ya uteuzi wa jimbo la Florida. Huku wajumbe 246 wakiwa watapiganiwa na vigogo hao wawili wa chama cha Demokrat jimbo hilo la Kusini linaelezwa kuwa ni muhimu...
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amesema mabadiliko ya kiuchumi yaliyofanyika nchini yameifanya Tanzania ipige hatua kubwa katika kipindi cha miaka 10 iliyopita. Ametoa kauli hiyo jana jioni wakati akihutubia kongamano la biashara baina ya Tanzania na Vietnam lililofanyika kwenye ukumbi wa Mikutano wa Mwalimu Nyerere jijini Dar es Salaam na kuhudhuriwa na Rais wa Jamhuri ya Kisoshalisti ya Vietnam, Bw. Troung Tan Sang. Akizungumza kwa niaba ya Rais, Dk. John Pombe Magufuli, Waziri Mkuu alisema mbali ya mabadiliko ya...
WATANZANIA leo wanaungana na watu wote duniani kuadhimisha siku ya Figo na tafiti za ugonjwa huo zinaonyesha kuwa kati ya mwezi Agosti 2014 na Februari 2015 kati ya watoto 513 waliopimwa magonjwa ya figo katika Hospitali za Bugando na Sekou Toure asilimia 16.2% walikuwa na matatizo ya figo. Siku ya Figo Duniani huadhimishwa duniani kote kila Alhamis ya pili ya mwezi Machi tangu mwaka 2006. Mwaka huu inaadhimishwa leo ikiwa na Kaulimbiu isemayo “Chukua Hatua Mapema Kuepuka Magonjwa ya...
Taasisi ya The Neghesti Sumari iliwakutanisha wanawake kwenye mjadala kuhusu usawa wa kijinsia uliofanyika kwendana na maadhimisho ya siku ya wanawake duniani. Kwenye mjadala huo uliofanyika Buni Hub kwenye jengo la COSTECH jijini Dar es Salaam, watoa mada walikuwa ni pamoja na mwenyekiti wa chama cha ACT Wazalendo, Anna Mghwira, Profesa Esther Mwaikambo, muanzilishi wa taasisi ya Doris Mollel na mjasiriamali na mtaalam wa masuala ya uchumi na Monica Joseph. Akizungumza kwenye mjadala huo, Mama Mghwira alisema alijifunza kujitegemea...
Tarehe kama ya leo 9th March mwaka 1997 ikiwa ni siku mbili baada ya kutwaa tuzo katika tukio la Soul Train music Awards Rappa anaeaminika kua ni bora wa muda wote Notorius.B.I.g akiwa anatoka katika Party moja majira ya saa 6 na nusu usiku gari aliyopanda ilisimama katika mataa ndipo ilitokea gari nyingine nyeusi aina ya chevrolet impala ss na dereva wake kushusha kioo na kumimina risasi kuelekea kwenye gari ya biggie ambazo zilimpata na kumjeruhi vibaya na kukimbizwa hospitali...