SERIKALI imewataka wananchi kutunza barabara zinazojengwa na Serikali kwa kushirikiana na wafadhili katika Halmashauri zote hapa nchini. Akizungumza Jijini Dar es salaam katika hafla fupi ya kupokea ripoti ya utekelezaji wa mradi wa Ujenzi na ukarabati wa barabara za halmashauri nchini Katibu Mkuu Ofisi ya Rais TAMISEMI bwana Mussa Iyombe amebainisha kuwa mradi huo umefadhiliwa na Shirika la Maendeleo la Japan (JICA) . Kwa mujibu wa Iyombe, Mradi huo unatekelezwa katika Halmashauri za Iringa,Mufindi,Chamwino na...
IMEELEZWA kuwa sekta ya mifugo nchini haichangii uchumi wa nchi kama ilivyotarajiwa na serikali. Akizungumza katika mkutano wa kwanza wa maaandalizi ya mpango mkakati wa sekta ya mifugo, Naibu Waziri wa kilimo mifugo na uvuvi Mheshimiwa WILLIAM OLE NASHA, amesema kutokana na hali hiyo Serikali inakusudia kuandaa mkakati ambao utainua sekta hiyo nakuweza kuchangia uchumi wa nchi na wananchi na wananchi kwa ujumla. Amesema kuwa pamoja na Tanzania kuwa nchi ya tatu Afrika kwakuwa na mifugo mingi ,lakini...
Klabu ya soka ya Barcelona imefanikiwa kuchomoza na ushindi wa bao 2-0 dhidi ya Arsenal katika mchezo wa kwanza wa Raundi ya Mtoano ya Timu 16 ya klabu bingwa barani ulaya (UEFA) mchezo uliopigwa uwanja wa Emirates. Mabao ya Barcelona katika mchezo huo yamefungwa na mchezaji Lionel Messi dakika ya 71 na Dakika ya 83 likiwa ni bao la pili lililofungwa kwa njia ya penati...
Mwakilishi wa ubalozi wa Nigeria, bibi Abiola Delupe aitembelea Efm Radio leo katika vitengo tofauti na kuona utendaji kazi wa radio. Huku akikutana na baadhi ya watangaziji kujadili mambo tofauti tofauti na jinsi watakavyo weza kuendeleza kazi zoa nje ya mipaka ya Tanzania. Bibi Abiola Delupe akizungumza jambo na Mkurugenzi wa Efm radio Francis Ciza. Baadhi ya viogozi wa Efm Radio katika mazungumzo na Bibi Abiola Delupe. Meneja mkuu Dennis Ssebbo akijadili mambo tofauti kuhusiana na ufanisi wa kazi katika...
KUNDI la kislamu la Islamic State limesema kuwa limetekeleza mashambulizi katika mji mkuu wa Syria Damascus na mji wa Homs, na kusababisha vifo vya watu 140. Kwa mujibu wa taarifa zilizotolewa kwa vyombo vya Habari zimeeleza kwamba Mapema huko Homs watu 57, wengi wao raia wa kawaida wameuawa katika mashambulizi mawili ya magari. Mashambulizi hayo mawili yamelenga maeneo yaliyozingirwa na waislamu wachache, kama ilivyoelezwa na kundi la waislamu la Sunni la...
KIONGOZI wa chama cha upinzani cha Forum for Democratic Change (FDC) nchini Uganda Kizza Besigye amekamatwa tena na maafisa wa polisi nchini humo. Watu walioshuhudia kukamatwa kwake wamesema kwamba Kizza amekamatwa alipokuwa akijaribu kuondoka nyumbani kwake alipokuwa amewekwa kizuizini. Awali kulikuwa na habari kwamba kiongozi huyo angefika makao makuu ya Tume ya Uchaguzi kuonesha matokeo rasmi ya uchaguzi wa urais ingawa tayari Tume ya Uchaguzi ilishamtangaza Rais Yoweri Museveni kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais uliofanyika Alhamisi wiki...
WAKATI Serikali kupitia Mawaziri,Wakuu wa Mikoa na Wakuu wa Wilaya ikiendelea na mpango wa kufukuza wafanyakazi wasiokidhi viwango vya utendaji kazi kwa kutumia Kauli ya Kutumbua Majipu iliyoanzishwa na Rais wa Awamu ya Tano Dokta John Pombe Magofuli, Wananchi wengi wameonesha kuunga mkono hatua hiyo. Wakizungumza na EFM kwa nyakati tofauti Wananchi hao wamesema Sehemu kubwa ya Wafanyakazi wamekuwa wakifanya kazi zao kwa mazoea na kufanya Ofisi na Taasisi za Serikali kama mali zao hivyo kitendo cha kuwaondosha kitasaidia kuongeza...
WAZIRI wa nchi ofisi ya Rais menejimenti ya utumishi wa umma na utawala bora mheshimiwa Angela Kairuki amemsimamisha kazi aliyekuwa mkuu wa chuo cha utumishi wa umma Said Nassoro kutokana na kushindwa kusimamia watumishi waliopo chini yake. Kairuki ametoa maagizo hayo leo Jijini Dar es salaam kwenye mkutano na waandishi wa Habari katika mkutano ulifanyika chuoni hapo. Aidha amebainisha kuwa usimamizi mbovu wa bwana Nassoro umetoa mwanya kwa viongozi mbalimbali wa matawi kufanya ubadhilifu wa mali za...
TAKRIBAN watu 140 wameuawa kwa milipuko ya mabomu katika miji ya Homs na Damascus nchini Syria, waangalizi na vyombo vya habari vya serikali wameeleza. Inaelezwa kuwa milipuko minne ilitokea katika eneo la Sayyida Zeinab mjini Damascus na kuua takriban watu 83, ambapo awali mjini Homs Watu 57 wengi wao raia waliuawa kwa mashambulizi ya mabomu yaliyokuwa yametegwa kwenye magari mawili. Wanamgambo wa Islamic State wamekiri kutekeleza mashambulizi hayo katika miji hiyo yote...
RAIS wa Uganda Yoweri Museveni amesema uchaguzi uliofanyika nchini humo Alhamisi wiki iliyopita ulikuwa wa haki na akasema wanaoutilia shaka hawaielewi Uganda. Aidha, ametetea hatua ya maafisa wa usalama kumzuilia mgombea mkuu wa upinzani Dkt Kizza Besigye wa chama cha FDC. Tume ya Uchaguzi ilisema Jumapili kwamba Bwana Museveni alipata ushindi wa asilimia 60.75 dhidi ya mpinzani wake wa karibu Dkt Besigye aliyepata asilimia 37.35, lakini upinzani umedai kuwepo wizi wa kura na waangalizi wa kimataifa wamesema pia kwamba...
CHAMA cha Waandishi wa Habari Wanawake Tanzania (TAMWA) kimesema wanawake waliogombea nafasi mbalimbali kwenye Uchaguzi Mkuu 2015 walikosa nafasi ya kutosha kuzungumza kwenye vyombo vya habari. Kwa mujibu wa TAMWA, utafiti mdogo walioufanya katika vyombo vya habari kadhaa ulibaini kuwa ni asilimia 11 tu ya wanawake wagombea ndio walipata nafasi ya kuandikwa katika magazeti wakati wa uchaguzi huo. Takwimu hizo zilitolewa mwishoni mwa wiki katika semina ya wadau wa vyombo vya habari pamoja na baadhi ya wagombea na...