KIWANDA CHA KUZALISHA MBOLEA KUNZISHWA LINDI
Local News

SHIRILA la maendeleo ya mafuta na petrol Tanzania (TPDC) kwa kushrikiana na kampuni tatu wanatarajia kuanzisha kiwanda cha kuzalisha mbolea katika wilaya ya kilwa mkoani lindi. Akizungunza wakati wa semina ya siku mbili ya kuwajengea uwezo waandishi wa habari kuhusu uelewa wa sekta ndogo ya mafuta na gesi mkurugenzi wa mkondo wa chini kutoka TPDC dokta Wellington Hudson amezitaja baadhi ya kampuni watakazoshirikiana nazo katika ujenzi wa kiwanda hicho kuwa ni pamoja na kampuni ya ferostar ya Ujerumani na haldo...

Like
343
0
Friday, 29 January 2016
SERIKALI YAAHIDI KUWAWEZESHA WAVUVI WADOGO
Local News

SERIKALI imewahakikishia wananchi hususani wavuvi wadogo kuwa itahakikisha inawawezesha wavuvi hao kufanya shughuli zao za uvuvi kwa manufaa ili kujiletea maendeleo yao pamoja na Taifa kwa ujumla. Hayo yamebainishwa leo Bungeni Mjini Dodoma na Waziri wa Kilimo, Mifugo na Uvuvi mheshimiwa Mwigulu Nchemba wakati akijibu swali la mbunge wa Jimbo la Mwibara mheshimiwa Kangi Lugola aliyetaka kufahamu jitihada za serikali katika kuwanufaisha wavuvi. Katika majibu ya swali hilo pia mheshimiwa Nchemba amewataka watu wenye dhamana ya kusimamia shughuli...

Like
158
0
Friday, 29 January 2016
KENYA: WAWILI WAPANDISHWA KIZIMBANI KUJIBU MASHTAKA YA MAUAJI
Global News

MAHAKAMA Kuu mjini Mombasa imeamua kwamba washukiwa wawili walioshitakiwa kwa mauaji ya watu 60 eneo la Mpeketoni miaka miwili iliyopita wana kesi ya kujibu. Jaji Martin Muya amesema upande wa mashitaka uliwasilisha ushahidi wa kutosha kuwafungulia mashitaka wawili hao. Diana Salim Suleiman na Mahadi Suleiman Mahadi ajulikanaye kama Jesus wanadaiwa kuhusika katika uvamizi uliopelekea kuuawa kwa watu 60 mwezi Juni mwaka 2014 katika vijiji vya Mpeketoni na Kaisairi, Kaunti ya Lamu.nchini Kenya....

Like
166
0
Thursday, 28 January 2016
UFISADI: WAZIRI WA UCHUMI JAPAN AJIUZULU
Global News

WAZIRI wa uchumi nchini Japan Akira Amari amejiuzulu kutokana na madai ya ufisadi yaliyokuwa yakimkabili. Bwana Amari ametoa tangazo hilo ghafla katika mkutano na waandishi wa habari jana ambapo mbali na hayo amekanusha kupokea hongo kutoka kwa kampuni moja ya ujenzi kama ilivyodaiwa na jarida moja la Japan. Hatua hiyo imechukuliwa kama pigo kubwa kwa waziri mkuu Shinzo Abe kwani Amari alitarajiwa kusafiri hadi New Zealand wiki ijayo kusaini mkataba wa ushirikiano kati ya mataifa ya ng’ambo ya pili ya...

Like
194
0
Thursday, 28 January 2016
SERIKALI YAAHIDI KUENDELEZA UJENZI WA BARABARA KWA KINGO CHA RAMI
Local News

SERIKALI imeahidi kuendelea na ujenzi wa barabara katika maeneo tofauti nchini kwa kiwango cha lami ili kutatua adha kubwa ya ubovu wa barabara ulipo katika maeneo mengi nchini.   Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Naibu Waziri wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano  Mhandisi Godwin Ngonyani wakati akijibu maswali ya wabunge waliouliza kuhusu mpango wa serikali kuboresha barabara zilizopo.   Akijibu swali la Mhe Richard Mganga Ndassa Mbunge wa Sumve (CCM) Mhandisi Godwin Ngonyani amesema katika mwaka wa fedha 2014/2015 na...

Like
237
0
Thursday, 28 January 2016
SERIKALI YATOLEA UFAFANUZI TAARIFA YA URUSHAJI WA MATANGAZO YA BUNGE
Local News

SERIKALI imetolea ufafanuzi kuhusu taarifa za upotoshaji kwa umma kuwa imefuta vipindi vya shughuli za Bunge kuoneshwa katika televisheni ya Shirika la Utangazaji la Tanzania (TBC) zilizoenea katika maeneo mbalimbali.   Hayo yamesemwa leo Mjini Dodoma na Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo Mheshimiwa Nape Nnauye wakati akizungumza na wananchi moja kwa moja kupitia vyombo mbalimbali vya habari nchini kutolea ufafanuzi taarifa hizo.   Mheshimiwa Nape amesema Serikali haijafuta vipindi vya Bunge bali ilichofanya ni kubadilisha...

Like
205
0
Thursday, 28 January 2016
SERIKALI YATOA UFAFANUZI WA URUSHAJI WA MATANGAZO YA BUNGE
Local News

SERIKALI imesema kuwa kusitishwa kwa baadhi ya matangazo ya moja kwa moja ya vikao vya Bunge haina maana kuwa matangazo hayo hayataoneshwa bali matangazo yataendelea kwa muda husika uliopendekezwa ili kuruhusu Kituo cha matangazo cha Taifa TBC kuendelea na majukumu mengine hata kabla ya kikao cha Bunge kukamilika. Akijibu swali la mheshimiwa Freeman Mbowe leo Bungeni mjini Dodoma katika kipindi cha maswali ya moja kwa moja kwa waziri mkuu, Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania mheshimiwa Kassim Majaliwa...

Like
296
0
Thursday, 28 January 2016
MALYSIA: KESI YA UFISADI YA RAZAK KUKATIWA RUFAA
Global News

SHIRIKA la kukabiliana na ufisadi nchini Malaysia limesema kuwa litakata rufaa kuhusu uamuzi wa kuondoa tuhuma za ufisadi dhidi ya waziri mkuuu, Najib Razak. Siku ya jumanne, mkuu wa sheria amesema kuwa uchunguzi haukupata ushahidi kwamba Najib alivunja sheria. Kesi hiyo imeitikisa nchi ya Malaysia na kutishia kumwondoa madarakani ikichangiwa na Uamuzi wa kumuondelea mashtaka hali iliyozua hisia kali kwa...

Like
215
0
Wednesday, 27 January 2016
AL-SHABAB WADHIBITI MIJI ILIYOKUWA IKISHIKILIWA NA MAJESHI YA KENYA
Global News

WAPIGANAJI wa kundi la Al-Shabab wameingia na kudhibiti miji ambayo majeshi ya Kenya yaliondoka jana nchini Somalia. Wakazi wa maeneo ya jirani na miji hiyo wamewaambia waandishi wa habari kwamba wapiganaji wa kundi hilo la Kiislamu wameingia kwenye miji ya Al-Adde, Hosingoh na Badhaadhe. Katika mji wa Hosingoh, mamia ya wapiganaji wanaripotiwa kuingia na kuhutubia wakazi na kisha wakamteua kiongozi wa kusimamia eneo...

Like
242
0
Wednesday, 27 January 2016
MRADI WA KUCHAKATA TAKA KUJENGWA KINONDONI
Local News

HALMASHAURI ya Manispaa ya Kinondoni inatarajia kujenga mradi wa kuchakata taka hususani zile zinazozalishwa kwenye masoko yanayopatikana kwenye manispaa hiyo lengo ikiwa ni kuondoa taka hizo ili manispaa iwe safi. Akizungumza na waandishi wa habari Jijini Dar Es Salaam leo Meya wa Manispaa ya kinondoni Boniface Jacob amesema kuwa mradi huo unaogharimu zaidi ya shilingi bilioni 2 za kitanzania utajengwa kwa ushirikiano kati ya serikali ya Ujerumani, Halmashauri ya Hambag na Halmashauri ya Manispaa ya kinondoni. Boniface ameeleza kuwa kutokana...

Like
267
0
Wednesday, 27 January 2016
MKUU WA MKOA WA PWANI ATOA SIKU 7 ZA KUTUMBUA MAJIPU
Local News

MKUU wa Mkoa wa Pwani Mhandisi Evarist Ndikilo ametoa muda wa siku saba kwa watendaji wa mitaa, watendaji wa kata na  wazazi wenye watoto waliofaulu kuingia kidato cha kwanza lakini hadi sasa wameshindwa  kuwapeleka shule wanafunzi hao, kuwapeleka shule haraka watoto wanafunzi hao.   Mhandisi Ndikilo ametoa agizo hilo wakati wa ziara yake ya siku moja katika halmashauri ya mji wa Kibaha  wakati akizungumza na watumishi na watendaji mbalimbali wa serikali na vyama vya siasa ambapo amesema kuwa mzazi ambaye...

Like
252
0
Wednesday, 27 January 2016
« Previous PageNext Page »