AU KUPELEKA UJUMBE MAALUM BURUNDI
Global News

UMOJA wa Afrika umeamua utapeleka ujumbe maalum nchini Burundi kujaribu kuishinikiza serikali ya nchi hiyo kuridhia jeshi la kulinda amani baada ya rais Nkurunzinza kuipinga hatua hiyo.   Taarifa hizo zimetolewa na afisa wa ngazi ya juu wa Umoja wa Afrika baada ya kumalizika mkutano wa kilele wa Umoja huo hapo jana.   Mwanadiplomasia wa ngazi ya juu kutoka nchi za Magharibi aliyefuatilia mkutano wa jana ameliambia shirika la habari la Reuters kwamba viongozi wa Umoja wa Afrika waliokutana kwa...

Like
186
0
Monday, 01 February 2016
WHO YAKUTANA KWA DHARURA KUJADILI ZIKA
Global News

SHIRIKA la Afya Duniani (WHO) leo linafanya mkutano wa dharura kujadili kuenea kwa virusi vya Zika. Mkutano huo mjini unaofanyika Geneva utajadili iwapo mlipuko wa virusi hivyo unafaa kutangazwa kuwa dharura ya kimataifa. Katika matukio mengi, watu walioambukizwa virusi hivyo vya Zika huwa hawaonyeshi dalili zozote, lakini virusi hivyo vinadaiwa kusababisha maelfu ya watoto kuzaliwa wakiwa na vichwa vidogo Amerika...

Like
205
0
Monday, 01 February 2016
MWONGOZO WA KUANDAA BAJETI WAWASILISHWA BUNGENI LEO
Local News

WIZARA ya Fedha na Mipango leo imewasilisha mapendekezo ya Mpango wa maendeleo ya Taifa pamoja na mwongozo wa kuandaa mpango na bajeti ya serikali ya mwaka 2016/2017 unaolenga utekelezwaji wa vipaumbele mbalimbali vya kuleta maendeleo. Akiwasilisha mapendekezo ya mpango na mwongozo huo Bungeni Mjini Dodoma, Waziri wa Fedha na Mipango dokta Philip Mpango amesema kuwa mpango huo unalenga kuinua kwa kiasi kikubwa uchumi wa Taifa. Awali mpango huo haukuweza kujadiliwa siku chache zilizopita kutokana na serikali kuuwasilisha kimakosa hali...

Like
291
0
Monday, 01 February 2016
WAFANYAKZI KAMPUNI YA CHIKO KUSHINIKIZA KUBORESHEWA MASLAHI YAO
Local News

ZAIDI ya wafanyakazi 800 wa kampuni ya ujenzi ya chiko ya Jamuhuri ya china inayojenga barabara kuu ya Dodoma Babati eneo la mayamaya mpaka mela wamegoma wakishinikiza uongozi wa kampuni hiyo uboreshe maslahi yao kwa kuwapatia mikataba pamoja na kuongeza mishahara  huku wakitaka serikali kuwafukuza wafanyakazi wa kigeni ambao wanapora ajira zinazoweza  kufanywa na wazawa huku wakilipwa mamilioni ya fedha.   Wakizungumza mbele ya waziri wa ujenzi uchukuzi na mawasiliano profesa Makame mbarawa wafanyakazi hao wamesema wamechoshwa na...

Like
188
0
Monday, 01 February 2016
EFM YAKABIDHIWA MICHORO YA MADARASA KUTOKA KWA AFISA ELIMU, KINONDONI
Local News

Efm Radio,katika harakati zakufanikisha ahadi ya kujenga madarasa, imekabidhiwa michoro ya ramani ya madarasa ya sekondari wilaya ya Kinondoni kata ya Kimara, Makabidhiano yaliyofanyika  katika ofisi za Kituo hicho cha Utangazaji kupitia masafa ya 93.7 leo asubuhi. Mkurugenzi Mkuu wa Efm Radio, Francis Siza akipokea ramani ya michoro ya madarasa kutoka kwa Afisa elimu wa wilaya ya Kinondoni Bwana Rogers J. Shemwelekwa. Afisa elimu wa wilaya ya Kinondoni Bw. Rogers J. Shemwelekwa katika picha ya pamoja na uongozi wa Efm...

Like
715
0
Monday, 01 February 2016
70 WAUAWA KWA MABOMU SYRIA
Global News

WATU zaidi ya  70 wameuawa kutokana na mashambulio  ya mabomu ambayo kundi la magaidi wanaoitwa Dola  la  Kiislamu limedai kuyafanya karibu  na sehemu takatifu ya Washia nje ya mji mkuu wa Syria, Damascus.   Kwa mujibu  wa  taarifa  iliyotolewa  na kituo kilichopo mjini London, kinachofuatilia haki za binadamu nchini  Syria, watu  hao waliuawa kutokana  na miripuko miwili ya mabomu karibu na  sehemu hiyo takatifu, Sayyida Zeinab.   Watoto kadhaa walikuwamo miongoni mwa walioangamizwa huku Watu wengine zaidi ya 100...

Like
354
0
Monday, 01 February 2016
NIGERIA YAOMBA MKOPO WA DHARURA
Global News

NIGERIA imeomba mkopo wa dharura wa jumla ya dola bilioni tatu na nusu kutoka Benki ya Dunia ili kujaribu kuziba pengo kwenye bajeti yake. Uchumi wa Nigeria umeathiriwa sana na kushuka kwa bei ya mafuta duniani. Waziri wa fedha nchini humo Kemi Adeosun amesema amekuwa akifanya mazungumzo na maafisa wa Benki ya Dunia. Hata hivyo, hatua ya Nigeria kuomba mkopo wa dharura inashangaza ikizingatiwa kwamba siku chache zilizopita Shirika la Fedha Duniani (IMF) lilisema haihitaji usaidizi wa...

Like
253
0
Monday, 01 February 2016
MACHAFUKO BURUNDI: RAIA 126000 WAKIMBILIA TANZANIA
Local News

IMEELEZWA kuwa zaidi ya raia laki 126,000 wa Burundi wamekimbilia nchini Tanzania tangu mwezi Aprili, 2015, kufuatia machafuko ya kisiasa nchini humo. Huku tayari wakimbizi  elfu 64,000 kutoka Jamhuri ya Kidemokrasi ya Kongo (DRC) wakiwa tayari nchini. Katibu Mkuu wa Umoja wa Mataifa Ban Ki-moon  ametoa dola za Marekani milioni 100, sawa na shilingi za Tanzania bilioni 220 kutoka katika Mfuko Mkuu wa Kushughulikia Dharura wa Umoja wa Mataifa -CERF kwa shughuli za misaada katika maeneo tisa yenye dharura duniani...

Like
222
0
Monday, 01 February 2016
RAIS MAGUFULI ASIKITISHWA NA KIFO CHA RUBANI MUINGEREZA ALIYEUAWA NA MAJANGILI
Local News

RAIS wa Jamhuri ya Mmuungano wa Tanzania Dokta  John Pombe Magufuli amesema amesikitishwa na kitendo cha kuuawa kwa rubani Mwingereza aliyekuwa akisaidiana na maafisa wa Tanzania kupambana na ujangili. Rubani wa helkopta Kapteni Roger Gower, alifariki baada ya majangili kuifyatulia risasi na kuidondosha helkopta aliyokuwa akiiendesha wakati alipoungana na askari wanyamapori waliokuwa wakikabiliana na majangili katika pori la akiba lililopo katika wilaya ya Meatu Mkoani Simiyu. Askari mmoja wa Tanzania alijeruhiwa wakati wa tukio hilo ambapo...

Like
274
0
Monday, 01 February 2016
MAKABURI YA WATU WENGI YAGUNDULIKA BURUNDI
Global News

SHIRIKA la Kimataifa la kutetea haki za binadamu la Amnesty International limesema limeona picha za setilite zinazoonyesha mamia ya raia wa Burundi kuuawa na baadae kuzikwa katika kaburi la watu wengi. Amnesty limesema sehemu za picha hizo zinaonyesha makaburi ya watu wengi yapatayo matano katika eneo la Buringa viungani mwa mji mkuu wa Bujumbura. Shirika hilo limeongeza kuwa uchunguzi wao wa kitaalamu unafanana na ule ambao wameupata kutoka kwa mashahidi kuwa kuna makaburi mengine ya pamoja ya watu waliouwawa siku...

Like
180
0
Friday, 29 January 2016
MAOMBI YA RUHUSA YA KUTOA MIMBA KWA WENYE ZIKA YATUMWA BRAZIL
Global News

KUNDI la mawakili, wanaharakati na wanasayansi nchini Brazil limewasilisha ombi kwa mahakama ya juu nchini humo likitaka wanawake wenye virusi vya Zika waruhusiwe kutoa mimba. Virusi vya Zika vinaaminika kusababisha watoto kuzaliwa wakiwa na vichwa vidogo, na kudumaza ubongo. Utoaji mimba nchini Brazil hauruhusiwi kisheria, ila tu wakati wa dharura ya kiafya au iwapo mimba imetokana na ubakaji hali ambayo kwa Kiingereza inajulikana kama...

Like
210
0
Friday, 29 January 2016
« Previous PageNext Page »