WAZIRI Mkuu Kassim Majaliwa, leo anatarajia kuzitembelea kaya zaidi ya 145 zilizoathiriwa na mafuriko katika kata ya Pawaga, wilayani Iringa kwa lengo la kuzifariji. Katika ziara hiyo Waziri Mkuu anatarajiwa kuambatana na Mbunge wa Jimbo la Isimani ilipo kata hiyo, William Lukuvi ambaye pia ni Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi, ambao kwa pamoja watajionea hali halisi ya maisha ya kaya hizo zinazoendelea kusaidiwa ili zirudi katika maisha yake ya kawaida. Hata hivo mkuu wa wilaya ya Iringa,...
MATOKEO ya awali yaliyotangazwa hii leo nchini Uganda yanaonyesha rais wa muda mrefu wa nchi hiyo amempita mpizani wake mkuu katika uchaguzi wa rais nchini humo. Kwa mujibu wa matokeo ya awali yaliyotangazwa na tume ya uchaguzi ya Uganda, rais Yoweri Kaguta Museveni amejipatia takriban asilimia 62 ya kura, akimpita mpinzani wake mkubwa Kizza Besigye aliyejipatia asili mia 33 ya kura. Matokeo hayo yanahusu asili mia 23 ya vituo vyote vya kupiga kura nchini humo ambapo Matokeo ya...
BAADA ya Baraza la mitiani Tanzania NECTA kutangaza Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2015 ,Wanafunzi wa shule ya sekondari pamba jijini Mwanza wameeleza kufurahishwa kwa mfumo wa ufaulu wa divisheni tofauti na mfumo uliokuwepo wa GPA . Wakizungumza na Efm baadhi ya wananfunzi hao wamesema kuwa matokeo hayo yanaonyesha namna mfumo wa divisheni unavyo pima uwezo wa wanafunzi darasani. Wakizungumzia mfumo wa GPA wamesema mfumo huo ulikuwa unawafanya wanafunzi kuzembea katika masomo yao wakiamini kuwa watafaulu hali ambayo imekuwa kinyume na...
SERIKALI imeombwa kuisaidia jamii ya watu wenye ulemavu wa aina mbalimbali kuhakikisha wanapata elimu kwani hadi sasa ni asilimia 10 pekee ndiyo wanaopata elimu. Akizungumza na kituo hiki Katibu wa Shirikisho la vyama vya watu wenye ulemavu (SHIVYAWATA) amesema kuwa Tanzania ina zaidi ya watu million sita wenye ulemavu mbalimbali hivyo ni vema wakasaidiwa kupata elimu ili kuondokana na tatizo la kuitegemea jamii na serikali kuwasaidia kuyaendesha maisha...
TUME ya Vyuo Vikuu Tanzania TCU leo imevifuta vyuo vikuu vishiriki viwili vya Sayansi za Kilimo na Teknolojia, pamoja na Teknolojia ya Habari vya Chuo cha Mtakatifu Yosefu Tanzania kutokana na kuwepo kwa matatizo ya muda mrefu ya ubora wa elimu, uongozi, ukiukwaji wa sheria na taratibu za uendeshaji wa chuo kikuu ambao hauzingatii matakwa ya Sheria ya Vyuo Vikuu. Katibu Mtendaji wa TCU Profesa Yunus Mgaya amesema kuwa kifungu cha 5(1)cha Sheria ya Vyuo Vikuu , sura ya...
BARAZA la mitiani Tanzania NECTA limetangaza Matokeo ya kidato cha nne mwaka 2015 , ambapo ufaulu unaelezwa kushuka kwa asilimia 1.85 kutoka asilimia 69.75 mwaka 2014 hadi asilimia 67.91 kwa mwaka 2015. Katibu Mtendaji wa NECTA Dokta Charles Msonde ameeleza kuwa takwimu za matokeo zinaonesha kuwa bado ufaulu wa masomo yaliyomengi upo chini ya asilimia hamsini na idadi ya watahiniwa waliopata daraja la kwanza, daraja la pili na daraja la tatu ni takribani robo ya watahiniwa waliofanya mtihani. Aidha, Dokta Msonde...
UMOJA wa Mataifa umetangaza kuwa aliyekuwa Katibu mkuu wa Umoja wa Mataifa, Boutros Boutros-Ghali amefariki dunia akiwa na umri wa miaka 93. Mmisri huyo, aliyekuwa katibu mkuu wa kwanza kutoka Afrika pamoja na Ulimwengu wa Kiarabu, alifariki dunia jana mjini Cairo, kutokana na maradhi yasiyojulikana. Wakati akisifiwa kwa operesheni ya kwanza kubwa ya msaada wa dharura kuwahi kufanywa na Umoja wa Mataifa kwa ajili ya kuwaisaidia waathiriwa wa baa la njaa nchini Somalia, uongozi wake ulikosolewa kutokana na Umoja wa...
KAMPUNI ya Apple imesema itapinga amri ya mahakama ya kuwasaidia wachunguzi wa shirika la kijasusi nchini Marekani FBI kuchukua habari katika simu ya muuaji wa watu 14 katika eneo la San Bernadinho nchini Marekani. Kampuni hiyo ilikuwa imeamrishwa kulisaidia shirika hilo la FBI kuifungua simu ya aina ya iphone ya Farook Syed ambayo wanasema ina habari muhimu. Katika taarifa yake mkurugenzi mkuu wa Apple Tim Cook amesema Serikali ya Marekani inaitaka Apple Kuchukua hatua kama hizo ambazo zinatishia...
WIZARA ya Elimu Sayansi Teknolojia na Ufundi imemtaka Mkurugenzi wa Taasisi ya Elimu ya Watu wazima kuwasimamisha kazi Wakufunzi wakazi wa tatu, kwa kukiuka utaratibu wa kuchagua wanafunzi wa kidato cha kwanza kufuatia upotoshaji uliofanywa kwa makusudi wa kuwadanganya Wanafunzi kuwa wamechaguliwa katika shule ya Serikali jambo ambalo sio kweli. Hatua hiyo imefikiwa kufuatia kuwepo kwa Wakufunzi wakazi katika baadhi ya Mikoa kutangaza kuwa Wanafunzi hao wamechaguliwa kujiunga na kidato cha kwanza kama Wanafunzi wa chaguo la pili na...
RAIS Barack Obama wa Marekani amesema anaamini mgombea urais wa Chama cha Republican Donald Trump hatakuwa rais wa Marekani. Bwana Trump, Mfanyabiashara tajiri kutoka New York, anaongoza kwenye kura za maoni katika kinyang’anyiro cha kuteua mgombea wa chama cha Republican na tayari ameshindakatika Uchaguzi wa mchujo jimbo moja. Akiongea wakati wa Mkutano Mkuu wa Kiuchumi wa nchi za Kusini Mashariki mwa Asia unaofanyika katika jimbo la California, alitoa kauli hiyo baada ya mwandishi wa Habari Mmoja kumuuliza swali lililomhusu...
RAIS wa Kenya Uhuru Kenyatta amesema Nchi hiyo itajenga jela mpya ya kuwafunga wafungwa wenye makossa ya itikadi kali. Kiongozi huyo amesema hatua hiyo itazuia wafungwa hao kutoeneza itikadi hizo kwa wafungwa wengine. Kwa sasa ni wafungwa waliohukumiwa pekee ambao hutengwa na wafungwa wengine gerezani nchini...