MGOMBEA Urais wa Marekani anayeongoza katika chama cha Republican Donald Trump, amejiongezea ushawishi kama mgombea mkuu kufuatia ushindi wake katika majimbo ya Michigan na Mississippi. Wadadisi wa masuala ya kisiasa wamesema kuwa ushindi huo mara mbili umezima uvumi wa mwishoni mwa wiki kuwa kampeni yake Trump ilikuwa imepoteza kasi. Baada ya kupata ushindi huo, Trump amesema kuwa anakiongezea umaarufu chama cha Republican ingawa Mshindani wake mkuu Seneta Ted Cruz naye amepata ushindi katika jimbo dogo la...
WAZIRI wa Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano Profesa Makame Mbarawa amezitaka taasisi za Serikali na binafsi kukitumia kituo cha kisasa cha kuhifadhi taarifa kutunza taarifa zao ili kuzihakikishia usalama na uhakika wa kuzitumia wakati wote. Akizungumza baada ya kukagua kituo hicho kinachosimamiwa na Wizara ya Ujenzi, Uchukuzi na Mawasiliano, sekta ya Mawasiliano Profesa Mbarawa amesema asilimia 75 ya kituo imetengwa kwa ajili ya kutunza taarifa kutoka sekta binafsi na asilimia 25 itatunza taarifa za Serikali. Mbali na hayo amezitaka...
RAIS wa Vietnam Truong Tan Sang tayari ameanza ziara yake ya siku tatu nchini ambapo leo amekutana na kufanya mazungumzo na Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania dokta John Pombe Magufuli Ikulu Jijini Dar es salaam. Katika ziara yake Rais Truong Tan Sang atapata nafasi ya kuonana na Rais mstaafu wa awamu ya nne ambaye pia ni mwenyekiti wa Chama cha mapinduzi-CCM-dokta Jakaya Mrisho Kikwete katika ofisi za chama hicho zilizopo Lumumba. Lengo la ziara hiyo ni kuimarisha zaidi...
Tanzania iliwakilishwa vyema na Single Mtambalike (Richie) pamoja na Elizabeth Michael (LULU) waliong’aa kwenye usiku wa kilele cha tuzo za Africa Magic Viewers Choice zilizoandaliwa na Multchoice| Dstv . Lulu alitwaa tuzo ya Best Movie East Africa kupitia filam ya Mapenzi ya Mungu wakati Richie akibeba tuzo ya Best Local Language Movie/TV Series (Swahili) kupitia filam ya Kitendawali. Alipowasili katika uwanja wa ndege wa kimataifa Wa Jk Nyerere Wema Sepetu aliposhuka kwenye gari kwenda kumvisha taji Lulu MKUTANO NA WAANDISHI...
Polisi nchini India wamemfungulia mashtaka ya mauaji mtu mmoja aliyemdunga chupa rafiki yake huku chanzo cha ugomvi kikiwa ni mabishano kuhusu nani kati ya Lionel Messi na Cristiano Ronaldo ndiye mchezaji bora duniani. Michael Chukwuma, 21 ambae ni raia wa Nigeria alimdunga kisu mwezake vilevile mnigeria ambaye walikuwa wakibishana naye. Tukio hilo limetokea katika kitongoji cha Nallasopara Kwa mujibu wa shirika la habari la AFP limeeleza kuwa Michael Chukwuma ameshtakiwa kwa kuua katika mji wa Mumbai ambapo Chukwuma na...
Katika kuelekea siku ya wanamke duniani EFM radio yakutanisha wanawake kutoka vikundi mbalimbali vya ujasiliamali na VICOBA kutoka jiji la Dar es Salaam na Pwani katika ukumbi wa litostar park Salasala, kwa lengo la kuwapa wanawake elimu ya ujasiliamali na kujitambua kama mwanamke, pia kuambiana changamoto tofauti zinazowakabili wanawake katika biashara zao na maisha kwa ujumla. Mgeni rasmi akiwa raisi wa VICOBA mhe.Devotha Likokola. Mgeni rasmi mhe. Devotha Likokola akiongea na wanawake wa vikundi mbalimbali kuwapa ...
Waigizaji wa filam Kutoka Tanzania Elizabeth Michael (Lulu) na Single Mtambalike Richie wamefanikiwa kubeba tuzo moja moja kwenye kilele cha Africa Magic Viewers Choice awards. Richie ndie alikuwa wa kwanza kuwainua watanzania pale alipotangaza kutwaa tuzo kwenye kipengere cha BEST INDIGENOUS LANGUAGE MOVIE/TV SERIES – SWAHILI kupitia filam ya KITENDAWILI huku Lulu akinyakuwa tuzo ya Best Movie East Africa kupitia filam ya Mapenzi ya Mungu. Tuzo hizo zilifanyika Nchini Nigria katika jiji la Lagosa na kuwakutanisha mastar mbalimbali kutoka...
Ligi kuu ya England iliendelea tena mwisho wa wiki kwa michezo miwili kuchezwa. Majogoo wa Anfield Liverpool wakicheza ugeni kwenye dimba la Selhurst Park waliibuka na ushindi wa mabao 2-1 dhidi ya Crystal Palace. Crystal Palace ndio walianza kuandika bao la kwanza kwa bao la Joe Ledley kisha Liverpool wakachomoa bao hilo kupitia kwa mshambuliaji wake Roberto Frimino, katika dakika za lala salama Christian Benteke akawapa ushindi kwa bao la mkwaju wa penati. Nao Mashetani Wekundu wa Man United wakachapwa...
Ligi kuu ya Tanzania itaendelea tena mwisho wa wiki hii kwa nyasi za viwanja mbalimbali kuwaka moto. Hapo kesho katika dimba la taifa Jijini Dar es Salaam kutachezwa mchezo wa wababe wawili wa soka Azam Fc watakaowakabili vinara wa ligi hiyo Yanga. Huku African Sport wakiwa nyumbani katika uwanja wa mkwakwani kukipiga na Majimaji. Toto Africans,watakua katika uwanja wa Kirumba, kupepetana na Ndanda FC. Kagera Sugar wao watakuwa na kibarua kizito dhidi ya Mgambo JKT. Kikosi cha JKT Ruvu kitawaalika...
POLISI waliopo Mashariki mwa Pakistan wamewakamata watu wanne wanaotuhumiwa kupanga ndoa kati ya mvulana mwenye umri wa miaka 14 na msichana mwenye umri wa miaka 10 pekee suala ambalo ni kinyume cha sheria. Imeelezwa kwamba ndoa hiyo ilikuwa imepangwa kama njia ya kusuluhisha mzozo baina ya familia hizo mbili. Tabia ya kuendeleza ndoa za mapema pamoja na kutatua mizozo ya nyumbani kupitia ndoa, ni hatia kwa mujibu wa sheria za...
MAAFISA wa polisi nchini Brazil wamemkamata aliyekuwa rais wa nchi hiyo Luiz Inacio da Silva ikiwa ni miongoni mwa mpango wa kuchunguza ufisadi dhidi yake. Mali zote zinazohusishwa naye ikiwemo nyumba yake na taasisi ya yake ya Lula zimevamiwa na Maafisa hao ili kuzuia shughuli yoyote ya uhujumu kufanyika. Da Silva atahojiwa kuhusu madai kwamba amefaidika na mpango wa rushwa uliokuwa ukiendeshwa na kampuni...