New Year’s Eve party ya Drake yawaunganisha Lil Wayne na Birdman, Huenda mwaka mpya wa 2016 ukawa ndio mwisho wa beef kati ya wawili hawa. Rais wa Young Money, Mack Maine amefanya kazi kubwa masaa mawili kabla ya party hiyo kuwakutanisha Lil Wayne na Birdman na kuweza kuzungumza jinsi ya kumaliza tofauti zao. Kwa majubu wa chanzo cha karibu na mastar hawa Mack Maine alitumia simu kuwakutanisha na kuzungumza huku wote wawili wakionyesha utayari wa kumaliza tofauti zao lakini Wyne...
Zinedine Zidane achukua nafasi ya Rafael Benitez kuinoa Real Madrid. Rafael Benitez ametimuliwa katika nafasi ya kuwa meneja wa klabu ya Real Madrid baada ya kushika hatamu ya uongozi katika kipindi cha miezi 7 kabla kibarua kuota nyasi. Mhispania huyu, Benitez, 55 ameanguliwa kwenye nafasi hiyo baada ya kikao cha bodi ya klabu hiyo kukutana na kufikia maamuzi hayo. Zidane, 43, amepandishwa kutoka kwenye nafasi yake ya awali ambapo alikuwa anakinoa kikosi B cha klabu ya Real Madrid Mfaransa...
VYANZO vya kiintelijensia nchini Uingereza vimeiambia BBC kwamba vinaamini wamemtambua mwanaume mwenye asili ya nchi hiyo ambaye anaonekana katika mkanda wa video wa hivi karibuni wenye kupigia chapuo propaganda za kundi la kigaidi la wanamgambo wa Islamic State. Vyanzo hivyo vimemtaja mtu huyo kuwa ni Siddhartha Dhar, ambaye anaaminika alikuwa akiishi Mashariki mwa London. Kwa asili Siddhartha anatajwa kuwa ni Mhindi ambaye aliamua kubadilisha dini yake ya awali na kuwa Mwislamu na inafahamika kuwa baada ya hapo aliamua...
RAIS Barack Obama wa Marekani anatarajiwa kutangaza mpango wa kuhakiki silaha katika masoko ya sihala hii leo wakati atakapotangaza mpango huo. Akizungumza na waandishi wa habari baada ya kukutana na Mwanasheria Mkuu wa nchi hiyo amesema anataka kutumia mamlaka yake ya urais kwa sababu bunge la congress limeshindwa kushughulikia tatizo hilo. Rais Obama ana matumaini kuwa jambo hilo limepokelewa na wamerekani wengi wakiwemo wamiliki wa silaha, wanaounga mkono na...
WAZIRI MKUU Kassim Majaliwa amefungua tawi la Benki ya Posta iliyopo mjini Songea, wakati akiwa katika ziara mkoni Ruvuma inayotarajiwa kumalizika kesho, jumatano. Akizungumza na uongozi na wafanyakazi wa Benki ya Posta pamoja na wateja waliohudhuria ufunguzi wa tawi hilo uliofanyika nje ya benki hiyo, Waziri Mkuu amesema amefarijika kuona benki hiyo iliyokua imekumbwa na matatizo sasa imezaliwa upya na kumpongeza Mkurugenzi wa Benki ya Posta nchini Bwana. Sabasaba Mushindi kwa jitihada zake za kuifufua....
MAHAKAMA kuu ya Tanzania kitengo cha Ardhi leo inatarajia kutoa maamuzi juu ya ombi la dharura la kutaka zoezi la bomoabomoa kusitishwa katika kipindi ambacho kesi hiyo ipo Mahakamani. Wakili wa mshitaki Abubakari Salim amesema kutokana na uwepo wa kesi mahakamani juu ya wananchi kutotendewa haki katika zoezi la kubomoa nyumba za mabondeni iliyofunguliwa na Mbunge wa Jimbo la Kinondoni Maulidi Mtulia waliamua kupeleka hati ya dharura ya kutaka zoezi hilo kusitishwa wakati kesi hiyo ikiendelea mahakamani. Jaji...
Timu ya mpira wa kikapu ya Los Angeles Lakers yafikiria kustaafisha jezi 2 alizovaa Kobe Bryant ndani ya kikosi hicho. Kobe ametangza kustaafu mpira wa kikapu mwishoni mwa msimu huu 2015/16, alisajiliwa na LA Lakers mwaka 1996 na kupewa jezi namba 8 baada ya jezi mbili alizokuwa anazitaka, jezi namba 33 ilikuwa tayari imeshastaafishwa kwa heshima ya Legendary Kareem Abdul- Jabbar na ile ya namba 24 ilikuwa inavaliwa na George McCloud hivyo ilimbidi Kobe avae jezi namba 8, Akiwa anavaa...
BAHRAIN imetangaza kwamba imevunja uhusiao wa kibalozi na Iran, saa chache baada ya Saudi Arabia kuchukua hatua. Saudi Arabia iliwapa maafisa wa ubalozi wa Iran siku mbili kuondoka nchini Saudi Arabia kufuatia mvutano uliotokana na kuuawa kwa muhubiri maarufu wa Kishia. Muhubiri huyo Sheikh Nimr al-Nimr aliuawa pamoja na watu wengine 46 baada ya kupatikana na makosa yanayohusiana na...
CHUO KIKUU cha Garissa kilichofungwa mwaka uliopita baada ya watu 148 kuuawa kwenye shambulio lililotekelezwa na wanamgambo wa al-Shabab, kimefunguliwa tena leo. Wafanyakazi wamefika kazini leo huku usalama ukiwa umeimarishwa. Kila aliyekuwa akiingia katika chuo kikuu hicho kilichoko eneo la kaskazini mashariki mwa Kenya amepekuliwa na maafisa wa usalama. Na Kituo cha polisi, ambacho kitakuwa na maafisa zaidi ya 20 wa kutoa ulinzi, kimejengwa ndani ya chuo kikuu...
MANISPAA ya wilaya ya Ilala, imepanga kukusanya kiasi cha shilingi bilioni kumi na mbili kutokana na kodi ya majengo kiasi kitakacho tumika katika kuboresha huduma za kijamii . Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo, Afisa uhusiano kutoka Manispaa hiyo, TABU SHAIBU amesema Manispaa ya Ilala ina vyanzo vingi vya mapato na moja ya vyanzo vikuu ni kodi ya majengo hivyo imepanga kuzunguka na kupita kila kona ya mtaa ili kuhakikisha ina wanakabiliana na wakwepa kodi ...
IMEELEZWA kuwa licha ya kupungua kwa maambukizi mapya katika baadhi ya Mikoa, kasi ya kukuwa kwa maambukizi ya ugonjwa wa Kipindupindu imeendelea kupanda katika Mikoa ya Mwanza na Arusha ambapo katika Mkoa wa Arusha maambukizi yamepanda kutoka wagonjwa wapya 60 hadi wagonjwa wapya 111 kwa wiki na katika Mkoa wa MWanza maambukizi yamepanda kutoka wagonjwa wapya 45 hadi 66 kwa wiki. Hayo yamesemwa leo na Naibu Waziri wa Afya, Maendeleo ya Jamii,Jinsia, Wazee na Watoto, Dokta Ahmis Kigwangala wakati...